< Mithali 27 >
1 Usijisifu kwa ajili ya kesho, kwa kuwa hujui ni nini kitakachozaliwa kwa siku moja.
Ne vous vantez pas du lendemain; car vous ne savez pas ce qu'un jour peut apporter.
2 Mwache mwingine akusifu, wala si kinywa chako mwenyewe; mtu mwingine afanye hivyo na si midomo yako mwenyewe.
Qu'un autre homme te loue, et pas votre propre bouche; un étranger, et non vos propres lèvres.
3 Jiwe ni zito na mchanga ni mzigo, lakini kukasirishwa na mpumbavu ni kuzito kuliko vyote viwili.
Une pierre est lourde, et le sable est un fardeau; mais la provocation d'un idiot est plus lourde que les deux.
4 Hasira ni ukatili na ghadhabu kali ni gharika, lakini ni nani awezaye kusimama mbele ya wivu?
La colère est cruelle, et la colère est écrasante; mais qui est capable de résister à la jalousie?
5 Afadhali karipio la wazi kuliko upendo uliofichika.
Mieux vaut une réprimande ouverte que l'amour caché.
6 Majeraha kutoka kwa rafiki yaonyesha uaminifu, bali kubusu kwa adui ni kwingi sana.
Les blessures d'un ami sont fidèles, bien que les baisers d'un ennemi soient profonds.
7 Yeye aliyeshiba huchukia kabisa asali, bali kwa mwenye njaa hata kile kilicho kichungu kwake ni kitamu.
Une âme rassasiée a horreur du rayon de miel; mais pour une âme affamée, toute chose amère est douce.
8 Kama ndege atangatangavyo mbali na kiota chake, ndivyo alivyo mtu atangatangaye mbali na nyumbani mwake.
Comme un oiseau qui s'éloigne de son nid, ainsi est un homme qui erre loin de sa maison.
9 Manukato na uvumba huleta furaha moyoni, nao uzuri wa rafiki huchipuka kutoka kwenye ushauri wake wa uaminifu.
Le parfum et l'encens apportent de la joie au cœur; tout comme les conseils sérieux de l'ami d'un homme.
10 Usimwache rafiki yako wala rafiki wa baba yako, tena usiende nyumbani mwa ndugu yako wakati umepatwa na maafa. Bora jirani wa karibu kuliko ndugu aliye mbali.
N'abandonne pas ton ami et l'ami de ton père. N'allez pas chez votre frère le jour de votre catastrophe. Un voisin proche vaut mieux qu'un frère éloigné.
11 Mwanangu, uwe na hekima, nawe ulete furaha moyoni mwangu, ndipo nitakapoweza kumjibu yeyote anitendaye kwa dharau.
Sois sage, mon fils, et apporte la joie dans mon cœur, alors je pourrai répondre à mon tourmenteur.
12 Mtu mwenye busara huona hatari na kujificha, bali mjinga huendelea mbele nayo ikamtesa.
L'homme prudent voit le danger et se réfugie; mais les simples passent, et en souffrent.
13 Chukua vazi la yule awekaye dhamana kwa ajili ya mgeni; lishikilie iwe dhamana kama anafanya hivyo kwa ajili ya mwanamke mpotovu.
Prenez son vêtement quand il met en gage un étranger. Tenez-le pour une femme rebelle!
14 Kama mtu akimbariki jirani yake kwa sauti kuu asubuhi na mapema, itahesabiwa kama ni laana.
Celui qui bénit son prochain avec une voix forte, tôt le matin, il sera pris comme une malédiction par lui.
15 Mke mgomvi ni kama matone yasiyokoma ya siku ya mvua.
Une goutte continue un jour de pluie et une épouse contestataire se ressemblent:
16 Kumzuia yeye ni kama kuuzuia upepo au kukamata mafuta kwa kiganja cha mkono.
La retenir, c'est comme retenir le vent, ou comme de saisir de l'huile dans sa main droite.
17 Kama vile chuma kinoavyo chuma, ndivyo mtu amnoavyo mwenzake.
Le fer aiguise le fer; ainsi un homme aiguise le visage de son ami.
18 Yeye autunzaye mtini atakula tunda lake, naye amtunzaye bwana wake ataheshimiwa.
Celui qui soigne le figuier mangera son fruit. Celui qui s'occupe de son maître sera honoré.
19 Kama uso uonekanavyo kwenye maji, ndivyo hivyo moyo wa mtu humwonyesha alivyo.
Comme l'eau reflète un visage, donc le cœur d'un homme reflète l'homme.
20 Kuzimu na Uharibifu havishibi kadhalika macho ya mwanadamu. (Sheol )
Sheol et Abaddon ne sont jamais satisfaits; et les yeux d'un homme ne sont jamais satisfaits. (Sheol )
21 Kalibu ni kwa ajili ya fedha na tanuru kwa ajili ya dhahabu, bali mtu hupimwa kwa sifa azipokeazo.
Le creuset est pour l'argent, et le fourneau pour l'or; mais l'homme est raffiné par ses louanges.
22 Hata ukimtwanga mpumbavu kwenye kinu, ukimtwanga kama nafaka kwa mchi, hutauondoa upumbavu wake.
Bien que tu broies un fou dans un mortier avec un pilon, avec le grain, mais sa folie ne lui sera pas enlevée.
23 Hakikisha kuwa unajua hali ya makundi yako ya kondoo na mbuzi, angalia kwa bidii ngʼombe zako.
Connaissez bien l'état de vos troupeaux, et faites attention à vos troupeaux,
24 Kwa kuwa utajiri haudumu milele, nayo taji haidumu vizazi vyote.
car les richesses ne sont pas éternelles, et la couronne ne perdure pas à travers les générations.
25 Wakati majani makavu yameondolewa na mapya yamechipua, nayo majani toka milimani yamekusanywa,
On enlève le foin, et la nouvelle pousse apparaît, les herbes des collines sont rassemblées.
26 wana-kondoo watakupatia mavazi na mbuzi thamani ya shamba.
Les agneaux servent à te vêtir, et les chèvres sont le prix d'un champ.
27 Utakuwa na maziwa mengi ya mbuzi kukulisha wewe na jamaa yako, na kuwalisha watumishi wako wa kike.
Il yaura du lait de chèvre en abondance pour votre nourriture, pour la nourriture de votre famille, et pour la nourriture de vos servantes.