< Mithali 27 >
1 Usijisifu kwa ajili ya kesho, kwa kuwa hujui ni nini kitakachozaliwa kwa siku moja.
Haue thou not glorie on the morewe, `not knowynge what thing the dai to comynge schal bringe forth.
2 Mwache mwingine akusifu, wala si kinywa chako mwenyewe; mtu mwingine afanye hivyo na si midomo yako mwenyewe.
Another man, and not thi mouth preise thee; a straunger, and not thi lippis `preise thee.
3 Jiwe ni zito na mchanga ni mzigo, lakini kukasirishwa na mpumbavu ni kuzito kuliko vyote viwili.
A stoon is heuy, and grauel is chariouse; but the ire of a fool is heuyere than euer eithir.
4 Hasira ni ukatili na ghadhabu kali ni gharika, lakini ni nani awezaye kusimama mbele ya wivu?
Ire hath no merci, and woodnesse brekynge out `hath no merci; and who mai suffre the fersnesse of a spirit stirid?
5 Afadhali karipio la wazi kuliko upendo uliofichika.
Betere is opyn repreuyng, than loue hid.
6 Majeraha kutoka kwa rafiki yaonyesha uaminifu, bali kubusu kwa adui ni kwingi sana.
Betere ben the woundis of hym that loueth, than the gileful cossis of hym that hatith.
7 Yeye aliyeshiba huchukia kabisa asali, bali kwa mwenye njaa hata kile kilicho kichungu kwake ni kitamu.
A man fillid schal dispise an hony coomb; but an hungri man schal take, yhe, bittir thing for swete.
8 Kama ndege atangatangavyo mbali na kiota chake, ndivyo alivyo mtu atangatangaye mbali na nyumbani mwake.
As a brid passinge ouer fro his nest, so is a man that forsakith his place.
9 Manukato na uvumba huleta furaha moyoni, nao uzuri wa rafiki huchipuka kutoka kwenye ushauri wake wa uaminifu.
The herte delitith in oynement, and dyuerse odours; and a soule is maad swete bi the good counsels of a frend.
10 Usimwache rafiki yako wala rafiki wa baba yako, tena usiende nyumbani mwa ndugu yako wakati umepatwa na maafa. Bora jirani wa karibu kuliko ndugu aliye mbali.
Forsake thou not thi frend, and the frend of thi fadir; and entre thou not in to the hous of thi brothir, in the dai of thi turment. Betere is a neiybore nyy, than a brothir afer.
11 Mwanangu, uwe na hekima, nawe ulete furaha moyoni mwangu, ndipo nitakapoweza kumjibu yeyote anitendaye kwa dharau.
Mi sone, studie thou a boute wisdom, and make thou glad myn herte; that thou maist answere a word to a dispisere.
12 Mtu mwenye busara huona hatari na kujificha, bali mjinga huendelea mbele nayo ikamtesa.
A fel man seynge yuel was hid; litle men of wit passinge forth suffriden harmes.
13 Chukua vazi la yule awekaye dhamana kwa ajili ya mgeni; lishikilie iwe dhamana kama anafanya hivyo kwa ajili ya mwanamke mpotovu.
Take thou awei his clooth, that bihiyte for a straunger; and take thou awei a wed fro hym for an alien man.
14 Kama mtu akimbariki jirani yake kwa sauti kuu asubuhi na mapema, itahesabiwa kama ni laana.
He that blessith his neiybore with greet vois; and risith bi niyt, schal be lijk hym that cursith.
15 Mke mgomvi ni kama matone yasiyokoma ya siku ya mvua.
Roouys droppynge in the dai of coold, and a womman ful of chidyng ben comparisond.
16 Kumzuia yeye ni kama kuuzuia upepo au kukamata mafuta kwa kiganja cha mkono.
He that withholdith hir, as if he holdith wynd; and auoidith the oile of his riyt hond.
17 Kama vile chuma kinoavyo chuma, ndivyo mtu amnoavyo mwenzake.
Yrun is whettid bi irun; and a man whettith the face of his frend.
18 Yeye autunzaye mtini atakula tunda lake, naye amtunzaye bwana wake ataheshimiwa.
He that kepith a fige tre, schal ete the fruytis therof; and he that is a kepere of his lord, schal be glorified.
19 Kama uso uonekanavyo kwenye maji, ndivyo hivyo moyo wa mtu humwonyesha alivyo.
As the cheris of men biholdinge schynen in watris; so the hertis of men ben opyn to prudent men.
20 Kuzimu na Uharibifu havishibi kadhalika macho ya mwanadamu. (Sheol )
Helle and perdicioun schulen not be fillid; so and the iyen of men moun not be fillid. (Sheol )
21 Kalibu ni kwa ajili ya fedha na tanuru kwa ajili ya dhahabu, bali mtu hupimwa kwa sifa azipokeazo.
As siluer is preuyd in a wellyng place, and gold `is preued in a furneys; so a man is preued bi the mouth of preyseris. The herte of a wickid man sekith out yuels; but a riytful herte sekith out kunnyng.
22 Hata ukimtwanga mpumbavu kwenye kinu, ukimtwanga kama nafaka kwa mchi, hutauondoa upumbavu wake.
Thouy thou beetist a fool in a morter, as with a pestel smytynge aboue dried barli; his foli schal not be don awei fro him.
23 Hakikisha kuwa unajua hali ya makundi yako ya kondoo na mbuzi, angalia kwa bidii ngʼombe zako.
Knowe thou diligentli the cheere of thi beeste; and biholde thou thi flockis.
24 Kwa kuwa utajiri haudumu milele, nayo taji haidumu vizazi vyote.
For thou schalt not haue power contynueli; but a coroun schal be youun to thee in generacioun and in to generacioun.
25 Wakati majani makavu yameondolewa na mapya yamechipua, nayo majani toka milimani yamekusanywa,
Medewis ben openyd, and greene eerbis apperiden; and hey is gaderid fro hillis.
26 wana-kondoo watakupatia mavazi na mbuzi thamani ya shamba.
Lambren be to thi clothing; and kidis be to the prijs of feeld.
27 Utakuwa na maziwa mengi ya mbuzi kukulisha wewe na jamaa yako, na kuwalisha watumishi wako wa kike.
The mylke of geete suffice to thee for thi meetis; in to the necessarie thingis of thin hous, and to lijflode to thin handmaidis.