< Mithali 27 >

1 Usijisifu kwa ajili ya kesho, kwa kuwa hujui ni nini kitakachozaliwa kwa siku moja.
May not you boast in a day tomorrow for not you know what? will it bring forth a day.
2 Mwache mwingine akusifu, wala si kinywa chako mwenyewe; mtu mwingine afanye hivyo na si midomo yako mwenyewe.
May he praise you a stranger and not own mouth your a foreigner and may not own lips your.
3 Jiwe ni zito na mchanga ni mzigo, lakini kukasirishwa na mpumbavu ni kuzito kuliko vyote viwili.
[the] heaviness of A stone and [the] weight of sand and [the] provocation of a fool [is] heavy more than both of them.
4 Hasira ni ukatili na ghadhabu kali ni gharika, lakini ni nani awezaye kusimama mbele ya wivu?
[the] cruelty of Rage and [the] flood of anger and who? will he stand before jealousy.
5 Afadhali karipio la wazi kuliko upendo uliofichika.
[is] good Rebuke uncovered more than love hidden.
6 Majeraha kutoka kwa rafiki yaonyesha uaminifu, bali kubusu kwa adui ni kwingi sana.
[are] reliable [the] wounds of [one who] loves And [are] abundant [the] kisses of [one who] hates.
7 Yeye aliyeshiba huchukia kabisa asali, bali kwa mwenye njaa hata kile kilicho kichungu kwake ni kitamu.
An appetite satisfied it treads down honey and an appetite hungry every bitter [thing] [is] sweet.
8 Kama ndege atangatangavyo mbali na kiota chake, ndivyo alivyo mtu atangatangaye mbali na nyumbani mwake.
Like a bird [which] wanders from nest its so a person [who] wanders from own place his.
9 Manukato na uvumba huleta furaha moyoni, nao uzuri wa rafiki huchipuka kutoka kwenye ushauri wake wa uaminifu.
Oil and perfume it makes glad a heart and [the] sweetness of friend his more than [the] counsel of a person.
10 Usimwache rafiki yako wala rafiki wa baba yako, tena usiende nyumbani mwa ndugu yako wakati umepatwa na maafa. Bora jirani wa karibu kuliko ndugu aliye mbali.
Friend your (and [the] neighbor of *Q(K)*) father your may not you forsake and [the] house of brother your may not you go on [the] day of calamity your [is] good a neighbor near more than a brother far away.
11 Mwanangu, uwe na hekima, nawe ulete furaha moyoni mwangu, ndipo nitakapoweza kumjibu yeyote anitendaye kwa dharau.
Be wise O son my and make glad heart my so let me bring back [one who] taunts me a word.
12 Mtu mwenye busara huona hatari na kujificha, bali mjinga huendelea mbele nayo ikamtesa.
A sensible [person] he sees evil he hides himself naive people they pass on they are punished.
13 Chukua vazi la yule awekaye dhamana kwa ajili ya mgeni; lishikilie iwe dhamana kama anafanya hivyo kwa ajili ya mwanamke mpotovu.
Take garment his for he stands surety for a stranger and for a foreign [woman] hold in pledge it.
14 Kama mtu akimbariki jirani yake kwa sauti kuu asubuhi na mapema, itahesabiwa kama ni laana.
[one who] blesses Neighbor his - with a voice great in the morning rising early a curse it is reckoned to him.
15 Mke mgomvi ni kama matone yasiyokoma ya siku ya mvua.
A dripping continuous on a day of persistent rain and a wife of (contentions *Q(K)*) she is like.
16 Kumzuia yeye ni kama kuuzuia upepo au kukamata mafuta kwa kiganja cha mkono.
[those who] hide Her he hides [the] wind and oil right [hand] his it meets.
17 Kama vile chuma kinoavyo chuma, ndivyo mtu amnoavyo mwenzake.
Iron by iron it grows sharp and each he sharpens [the] face of neighbor his.
18 Yeye autunzaye mtini atakula tunda lake, naye amtunzaye bwana wake ataheshimiwa.
[one who] keeps A fig tree he will eat fruit its and [one who] protects master his he will be honored.
19 Kama uso uonekanavyo kwenye maji, ndivyo hivyo moyo wa mtu humwonyesha alivyo.
Like water the face to the face so [the] heart of the person to the person.
20 Kuzimu na Uharibifu havishibi kadhalika macho ya mwanadamu. (Sheol h7585)
Sheol (and destruction its *Q(K)*) not they are satisfied and [the] eyes of person not they are satisfied. (Sheol h7585)
21 Kalibu ni kwa ajili ya fedha na tanuru kwa ajili ya dhahabu, bali mtu hupimwa kwa sifa azipokeazo.
A crucible for silver and a smelting furnace for gold and a person to [the] mouth of praise his.
22 Hata ukimtwanga mpumbavu kwenye kinu, ukimtwanga kama nafaka kwa mchi, hutauondoa upumbavu wake.
If you will pound the fool - in mortar in among the grain with the pestle not it will depart from with him foolishness his.
23 Hakikisha kuwa unajua hali ya makundi yako ya kondoo na mbuzi, angalia kwa bidii ngʼombe zako.
Certainly you will know [the] face of flock your set heart your to [the] herds.
24 Kwa kuwa utajiri haudumu milele, nayo taji haidumu vizazi vyote.
For not [is] for ever wealth and if a crown to a generation (and a generation. *Q(K)*)
25 Wakati majani makavu yameondolewa na mapya yamechipua, nayo majani toka milimani yamekusanywa,
It disappears grass and it appears grass and they are gathered [the] vegetation of [the] mountains.
26 wana-kondoo watakupatia mavazi na mbuzi thamani ya shamba.
Lambs [are] for clothing your and [the] price of a field goats.
27 Utakuwa na maziwa mengi ya mbuzi kukulisha wewe na jamaa yako, na kuwalisha watumishi wako wa kike.
And a sufficiency of - [the] milk of goats for food your for [the] food of household your and life of maids your.

< Mithali 27 >