< Mithali 27 >

1 Usijisifu kwa ajili ya kesho, kwa kuwa hujui ni nini kitakachozaliwa kwa siku moja.
Ne hvali se danom sutrašnjim jer ne znaš što danas može donijeti.
2 Mwache mwingine akusifu, wala si kinywa chako mwenyewe; mtu mwingine afanye hivyo na si midomo yako mwenyewe.
Neka te hvali drugi, a ne tvoja usta, tuđinac, a ne tvoje usne.
3 Jiwe ni zito na mchanga ni mzigo, lakini kukasirishwa na mpumbavu ni kuzito kuliko vyote viwili.
Težak je kamen i pijesak je težak, ali je od obojega teži bezumnikov bijes.
4 Hasira ni ukatili na ghadhabu kali ni gharika, lakini ni nani awezaye kusimama mbele ya wivu?
Jarost je okrutna i srdžba žestoka a tko će odoljeti ljubomoru?
5 Afadhali karipio la wazi kuliko upendo uliofichika.
Bolji je javni ukor nego lažna ljubav.
6 Majeraha kutoka kwa rafiki yaonyesha uaminifu, bali kubusu kwa adui ni kwingi sana.
Čestiti su udarci prijateljevi, a lažni poljupci neprijateljevi.
7 Yeye aliyeshiba huchukia kabisa asali, bali kwa mwenye njaa hata kile kilicho kichungu kwake ni kitamu.
Sito grlo prezire i med samotok, a gladnu je i sve gorko - slatko.
8 Kama ndege atangatangavyo mbali na kiota chake, ndivyo alivyo mtu atangatangaye mbali na nyumbani mwake.
Kao ptica daleko od gnijezda svog, takav je čovjek daleko od svojeg zavičaja.
9 Manukato na uvumba huleta furaha moyoni, nao uzuri wa rafiki huchipuka kutoka kwenye ushauri wake wa uaminifu.
Kao što ulje i kad vesele srce, tako i slatkoća prijateljstva tješi dušu.
10 Usimwache rafiki yako wala rafiki wa baba yako, tena usiende nyumbani mwa ndugu yako wakati umepatwa na maafa. Bora jirani wa karibu kuliko ndugu aliye mbali.
Ne ostavljaj prijatelja svoga ni prijatelja očeva i ne dolazi u kuću bratovu kad si u nesreći; bolji je susjed blizu nego brat daleko.
11 Mwanangu, uwe na hekima, nawe ulete furaha moyoni mwangu, ndipo nitakapoweza kumjibu yeyote anitendaye kwa dharau.
Budi mudar, sine moj, i obraduj mi srce da mogu odgovoriti onome koji me grdi.
12 Mtu mwenye busara huona hatari na kujificha, bali mjinga huendelea mbele nayo ikamtesa.
Pametan čovjek opazi zlo i skrije se, a glupaci idu bezbrižno i trpe kaznu.
13 Chukua vazi la yule awekaye dhamana kwa ajili ya mgeni; lishikilie iwe dhamana kama anafanya hivyo kwa ajili ya mwanamke mpotovu.
Uzmi haljinu onomu tko je jamčio za drugoga i oplijeni ga mjesto tuđinca.
14 Kama mtu akimbariki jirani yake kwa sauti kuu asubuhi na mapema, itahesabiwa kama ni laana.
Tko pozdravlja svoga prijatelja naglas, a rano ujutro, prima mu se blagoslov za kletvu.
15 Mke mgomvi ni kama matone yasiyokoma ya siku ya mvua.
Streha što prokišnjava za žestoke kiše i svadljiva žena - jedno su te isto.
16 Kumzuia yeye ni kama kuuzuia upepo au kukamata mafuta kwa kiganja cha mkono.
Tko nju zaustavlja, zaustavlja vjetar i desnicom hvata ulje.
17 Kama vile chuma kinoavyo chuma, ndivyo mtu amnoavyo mwenzake.
Željezo se željezom oštri i čovjek oštri jedan drugoga.
18 Yeye autunzaye mtini atakula tunda lake, naye amtunzaye bwana wake ataheshimiwa.
Tko čuva smokvu, jede od njena ploda, i tko čuva svoga gospodara, poštiva se.
19 Kama uso uonekanavyo kwenye maji, ndivyo hivyo moyo wa mtu humwonyesha alivyo.
Kao što se u vodi različito odražava lice od lica, tako i u srcu čovjek od čovjeka.
20 Kuzimu na Uharibifu havishibi kadhalika macho ya mwanadamu. (Sheol h7585)
Carstvo Smrti i Propast ne mogu se zasititi, tako ni oči čovječje. (Sheol h7585)
21 Kalibu ni kwa ajili ya fedha na tanuru kwa ajili ya dhahabu, bali mtu hupimwa kwa sifa azipokeazo.
Taljika je za srebro i peć za zlato, a čovjek se poznaje po ustima koja ga hvale.
22 Hata ukimtwanga mpumbavu kwenye kinu, ukimtwanga kama nafaka kwa mchi, hutauondoa upumbavu wake.
Da bezumnika stučeš tučkom u stupi, ne bi ga ostavila ludost njegova.
23 Hakikisha kuwa unajua hali ya makundi yako ya kondoo na mbuzi, angalia kwa bidii ngʼombe zako.
Brižno pazi na stoku svoju i srcem se brini o stadima,
24 Kwa kuwa utajiri haudumu milele, nayo taji haidumu vizazi vyote.
jer blago ne traje dovijeka; i baštini li se kruna od koljena do koljena?
25 Wakati majani makavu yameondolewa na mapya yamechipua, nayo majani toka milimani yamekusanywa,
Kad trava nikne i zelen se pokaže i bilje se kupi planinsko,
26 wana-kondoo watakupatia mavazi na mbuzi thamani ya shamba.
tad su ti janjci za odijelo i jarci za kupovinu polja;
27 Utakuwa na maziwa mengi ya mbuzi kukulisha wewe na jamaa yako, na kuwalisha watumishi wako wa kike.
tad imaš izobilje kozjega mlijeka sebi za jelo, i za hranu kući svojoj i za prehranu sluškinjama svojim.

< Mithali 27 >