< Mithali 27 >

1 Usijisifu kwa ajili ya kesho, kwa kuwa hujui ni nini kitakachozaliwa kwa siku moja.
不要為明日自誇, 因為一日要生何事,你尚且不能知道。
2 Mwache mwingine akusifu, wala si kinywa chako mwenyewe; mtu mwingine afanye hivyo na si midomo yako mwenyewe.
要別人誇獎你,不可用口自誇; 等外人稱讚你,不可用嘴自稱。
3 Jiwe ni zito na mchanga ni mzigo, lakini kukasirishwa na mpumbavu ni kuzito kuliko vyote viwili.
石頭重,沙土沉, 愚妄人的惱怒比這兩樣更重。
4 Hasira ni ukatili na ghadhabu kali ni gharika, lakini ni nani awezaye kusimama mbele ya wivu?
忿怒為殘忍,怒氣為狂瀾, 惟有嫉妒,誰能敵得住呢?
5 Afadhali karipio la wazi kuliko upendo uliofichika.
當面的責備強如背地的愛情。
6 Majeraha kutoka kwa rafiki yaonyesha uaminifu, bali kubusu kwa adui ni kwingi sana.
朋友加的傷痕出於忠誠; 仇敵連連親嘴卻是多餘。
7 Yeye aliyeshiba huchukia kabisa asali, bali kwa mwenye njaa hata kile kilicho kichungu kwake ni kitamu.
人吃飽了,厭惡蜂房的蜜; 人飢餓了,一切苦物都覺甘甜。
8 Kama ndege atangatangavyo mbali na kiota chake, ndivyo alivyo mtu atangatangaye mbali na nyumbani mwake.
人離本處飄流, 好像雀鳥離窩遊飛。
9 Manukato na uvumba huleta furaha moyoni, nao uzuri wa rafiki huchipuka kutoka kwenye ushauri wake wa uaminifu.
膏油與香料使人心喜悅; 朋友誠實的勸教也是如此甘美。
10 Usimwache rafiki yako wala rafiki wa baba yako, tena usiende nyumbani mwa ndugu yako wakati umepatwa na maafa. Bora jirani wa karibu kuliko ndugu aliye mbali.
你的朋友和父親的朋友, 你都不可離棄。 你遭難的日子,不要上弟兄的家去; 相近的鄰舍強如遠方的弟兄。
11 Mwanangu, uwe na hekima, nawe ulete furaha moyoni mwangu, ndipo nitakapoweza kumjibu yeyote anitendaye kwa dharau.
我兒,你要作智慧人,好叫我的心歡喜, 使我可以回答那譏誚我的人。
12 Mtu mwenye busara huona hatari na kujificha, bali mjinga huendelea mbele nayo ikamtesa.
通達人見禍藏躲; 愚蒙人前往受害。
13 Chukua vazi la yule awekaye dhamana kwa ajili ya mgeni; lishikilie iwe dhamana kama anafanya hivyo kwa ajili ya mwanamke mpotovu.
誰為生人作保,就拿誰的衣服; 誰為外女作保,誰就承當。
14 Kama mtu akimbariki jirani yake kwa sauti kuu asubuhi na mapema, itahesabiwa kama ni laana.
清晨起來,大聲給朋友祝福的, 就算是咒詛他。
15 Mke mgomvi ni kama matone yasiyokoma ya siku ya mvua.
大雨之日連連滴漏, 和爭吵的婦人一樣;
16 Kumzuia yeye ni kama kuuzuia upepo au kukamata mafuta kwa kiganja cha mkono.
想攔阻她的,便是攔阻風, 也是右手抓油。
17 Kama vile chuma kinoavyo chuma, ndivyo mtu amnoavyo mwenzake.
鐵磨鐵,磨出刃來; 朋友相感也是如此。
18 Yeye autunzaye mtini atakula tunda lake, naye amtunzaye bwana wake ataheshimiwa.
看守無花果樹的,必吃樹上的果子; 敬奉主人的,必得尊榮。
19 Kama uso uonekanavyo kwenye maji, ndivyo hivyo moyo wa mtu humwonyesha alivyo.
水中照臉,彼此相符; 人與人,心也相對。
20 Kuzimu na Uharibifu havishibi kadhalika macho ya mwanadamu. (Sheol h7585)
陰間和滅亡永不滿足; 人的眼目也是如此。 (Sheol h7585)
21 Kalibu ni kwa ajili ya fedha na tanuru kwa ajili ya dhahabu, bali mtu hupimwa kwa sifa azipokeazo.
鼎為煉銀,爐為煉金, 人的稱讚也試煉人。
22 Hata ukimtwanga mpumbavu kwenye kinu, ukimtwanga kama nafaka kwa mchi, hutauondoa upumbavu wake.
你雖用杵將愚妄人與打碎的麥子一同搗在臼中, 他的愚妄還是離不了他。
23 Hakikisha kuwa unajua hali ya makundi yako ya kondoo na mbuzi, angalia kwa bidii ngʼombe zako.
你要詳細知道你羊群的景況, 留心料理你的牛群;
24 Kwa kuwa utajiri haudumu milele, nayo taji haidumu vizazi vyote.
因為資財不能永有, 冠冕豈能存到萬代?
25 Wakati majani makavu yameondolewa na mapya yamechipua, nayo majani toka milimani yamekusanywa,
乾草割去,嫩草發現, 山上的菜蔬也被收斂。
26 wana-kondoo watakupatia mavazi na mbuzi thamani ya shamba.
羊羔之毛是為你作衣服; 山羊是為作田地的價值,
27 Utakuwa na maziwa mengi ya mbuzi kukulisha wewe na jamaa yako, na kuwalisha watumishi wako wa kike.
並有母山羊奶夠你吃, 也夠你的家眷吃, 且夠養你的婢女。

< Mithali 27 >