< Mithali 26 >

1 Kama theluji wakati wa kiangazi au mvua wakati wa mavuno, ndivyo asivyostahili heshima mpumbavu.
Yazda qar yéghish, Orma waqtida yamghur yéghish qamlashmighandek, Izzet-hörmet exmeqqe layiq emestur.
2 Kama shomoro apigapigavyo mabawa yake au mbayuwayu katika kuruka kwake kasi, ndivyo ilivyo laana isiyo na sababu haimpati mtu.
Leylep uchup yürgen quchqachtek, Uchqan qarlighach yerge qonmighandek, Sewebsiz qarghish kishige ziyan keltürelmes.
3 Mjeledi kwa farasi, lijamu kwa punda, nayo fimbo kwa migongo ya wapumbavu!
Atqa qamcha, éshekke noxta lazim bolghinidek, Exmeqning dümbisige tayaq layiqtur.
4 Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, ama wewe mwenyewe utakuwa kama yeye.
Exmeqning exmiqane gépi boyiche uninggha jawab bermigin, Jawab berseng özüng uninggha oxshap qélishing mumkin.
5 Mjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, ama atakuwa mwenye hekima machoni pake mwenyewe.
Exmeqning exmiqane gépi boyiche uninggha jawab bergin, Jawab bermiseng u özining exmeqliqini eqilliq dep chaghlar.
6 Kama vile ilivyo kujikata miguu au kunywa hasara, ndivyo ilivyo kutuma ujumbe kwa mkono wa mpumbavu.
Öz putini késiwetkendek, Öz béshigha zulmet tiligendek, Exmeqtin xewer yollashmu shundaq bir ishtur.
7 Kama miguu ya kiwete inavyoningʼinia ndivyo ilivyo mithali katika kinywa cha mpumbavu.
Tokurning kargha kelmigen putliridek, Exmeqning aghzigha sélin’ghan pend-nesihetmu bikar bolur.
8 Kama kufunga jiwe kwenye kombeo, ndivyo ilivyo kumpa mpumbavu heshima.
Salghigha tashni baghlap atqandek, Exmeqqe hörmet bildürüshmu exmiqane ishtur.
9 Kama mwiba kwenye mkono wa mlevi ndivyo ilivyo mithali kinywani mwa mpumbavu.
Exmeqning aghzigha sélin’ghan pend-nesihet, Mestning qoligha sanjilghan tikendektur.
10 Kama mpiga upinde ambaye hujeruhi ovyo, ndivyo alivyo yeye aajiriye mpumbavu au yeyote apitaye njiani.
Öz yéqinlirini qarisigha zeximlendürgen oqyachidek, Exmeqni yaki udul kelgen ademni yallap ishletken xojayinmu oxshashla zeximlendürgüchidur.
11 Kama mbwa ayarudiavyo matapiko yake, ndivyo mpumbavu arudiavyo upumbavu wake.
It aylinip kélip öz qusuqini yalighandek, Exmeq exmeqliqini qaytilar.
12 Je, unamwona mtu ajionaye mwenye hekima machoni pake mwenyewe? Liko tumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwake.
Özini dana chaghlap memnun bolghan kishini kördüngmu? Uninggha ümid baghlimaqtin exmeqqe ümid baghlimaq ewzeldur.
13 Mvivu husema, “Yuko simba barabarani, simba mkali anazunguka mitaa!”
Hurun adem: — «Tashqirida dehshetlik bir shir turidu, Kochida bir shir yüridu!» — dep [öydin chiqmas].
14 Kama vile mlango ugeukavyo kwenye bawaba zake, ndivyo mvivu ajigeuzavyo kitandani mwake.
Öz mujuqida échilip-yépilip turghan ishikke oxshash, Hurun kariwatta yétip u yaq-bu yaqqa örülmekte.
15 Mtu mvivu hutumbukiza mkono wake kwenye sahani, naye huchoka kuupeleka kwenye kinywa chake.
Hurun qolini sunup qachigha tiqqini bilen, Ghizani aghzigha sélishtinmu ériner.
16 Mtu mvivu ni mwenye hekima machoni pake mwenyewe, kuliko watu saba wawezao kujibu kwa busara.
Hurun özini pem bilen jawab bergüchi yette kishidinmu dana sanar.
17 Kama yeye amkamataye mbwa kwa masikio, ndivyo alivyo mtu apitaye njiani na kujiingiza kwenye ugomvi usiomhusu.
Kochida kéliwétip, özige munasiwetsiz majiragha arilashqan kishi, Itning quliqini tutup sozghan’gha oxshash xeterge duchar bolar.
18 Kama mtu mwendawazimu atupaye vijinga vya moto au mishale ya kufisha,
Öz yéqinlirini aldap «Peqet chaqchaq qilip qoydum!» deydighan kishi, Otqashlarni, oqlarni, herxil ejellik qorallarni atqan telwige oxshaydu.
19 ndivyo alivyo mtu amdanganyaye jirani yake na kusema, “Nilikuwa nikifanya mzaha tu!”
20 Bila kuni moto huzimika; pasipo uchongezi ugomvi humalizika.
Otun bolmisa ot öcher; Gheywet bolmisa, jédel bésilar.
21 Kama makaa juu ya makaa yanayowaka, na kama kuni kwenye moto, ndivyo alivyo mtu mgomvi kwa kuchochea ugomvi.
Choghlar üstige chachqan kömürdek, Ot üstige qoyghan otundek, jédelchi jédelni ulghaytar.
22 Maneno ya mchongezi ni kama chakula kitamu; huingia sehemu za ndani sana za mtu.
Gheywetxorning sözliri herxil nazunémetlerdek, Kishining qelbige chongqur singdürüler.
23 Kama rangi ingʼaayo iliyopakwa kwenye vyombo vya udongo ndivyo ilivyo midomo laini pamoja na moyo mbaya.
Yalqunluq lewler rezil köngüllerge qoshulghanda, Sapal qachigha kümüsh hel bergen’ge oxshashtur.
24 Mtu mwenye nia ya kudhuru wengine hujificha kwa maneno ya midomo yake, lakini moyoni mwake huficha udanganyifu.
Adawet saqlaydighan adem öchini gepliri bilen yapsimu, Könglide qat-qat suyiqest saqlaydu.
25 Ingawa maneno yake huvutia, usimwamini, kwa maana machukizo saba hujaza moyo wake.
Uning sözi chirayliq bolsimu, ishinip ketmigin; Qelbide yette qat iplasliq bardur.
26 Nia yake ya kudhuru wengine inaweza kufichwa na udanganyifu, lakini uovu wake utafichuliwa kwenye kusanyiko.
U öchmenlikini chirayliq gep bilen yapsimu, Lékin rezilliki jamaetning aldida ashkarilinar.
27 Kama mtu akichimba shimo, atatumbukia ndani yake, kama mtu akivingirisha jiwe, litamrudia.
Kishige ora kolighan özi chüsher; Tashni domilatqan kishini tash dumilap qaytip kélip uni yanjar.
28 Ulimi wa uongo, huwachukia wale unaowaumiza, nacho kinywa cha kujipendekeza hutenda uharibifu.
Saxta til özi ziyankeshlik qilghan kishilerge nepretliner; Xushamet qilghuchi éghiz ademni halaketke ittirer.

< Mithali 26 >