< Mithali 26 >

1 Kama theluji wakati wa kiangazi au mvua wakati wa mavuno, ndivyo asivyostahili heshima mpumbavu.
Como la nieve en el verano, y la lluvia en la siega, así conviene al loco la honra.
2 Kama shomoro apigapigavyo mabawa yake au mbayuwayu katika kuruka kwake kasi, ndivyo ilivyo laana isiyo na sababu haimpati mtu.
Como el gorrión en su vagar, y como la golondrina en su vuelo, así la maldición sin causa nunca vendrá.
3 Mjeledi kwa farasi, lijamu kwa punda, nayo fimbo kwa migongo ya wapumbavu!
El látigo para el caballo, y el cabestro para el asno, y la vara para el cuerpo del loco.
4 Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, ama wewe mwenyewe utakuwa kama yeye.
Nunca respondas al loco en conformidad a su locura, para que no seas tú también como él.
5 Mjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, ama atakuwa mwenye hekima machoni pake mwenyewe.
Responde al loco mostrándole su locura, para que no se estime sabio en su opinión.
6 Kama vile ilivyo kujikata miguu au kunywa hasara, ndivyo ilivyo kutuma ujumbe kwa mkono wa mpumbavu.
El que da un cargo al que no tiene facultad para ejercitarlo, es el que envía algo por mano del loco; y beberá el daño.
7 Kama miguu ya kiwete inavyoningʼinia ndivyo ilivyo mithali katika kinywa cha mpumbavu.
Así como camina el cojo; es el proverbio en la boca del loco.
8 Kama kufunga jiwe kwenye kombeo, ndivyo ilivyo kumpa mpumbavu heshima.
Como quien liga la piedra en la honda, así es el que da honra al loco.
9 Kama mwiba kwenye mkono wa mlevi ndivyo ilivyo mithali kinywani mwa mpumbavu.
Espinas hincadas en mano del embriagado, tal es el proverbio en la boca de los locos.
10 Kama mpiga upinde ambaye hujeruhi ovyo, ndivyo alivyo yeye aajiriye mpumbavu au yeyote apitaye njiani.
El gran Dios cría todas las cosas; y al loco da la paga, y a los transgresores da el salario.
11 Kama mbwa ayarudiavyo matapiko yake, ndivyo mpumbavu arudiavyo upumbavu wake.
Como perro que vuelve a su vómito, así el loco que repite su locura.
12 Je, unamwona mtu ajionaye mwenye hekima machoni pake mwenyewe? Liko tumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwake.
¿Has visto hombre sabio en su propia opinión? Más esperanza hay del loco que de él.
13 Mvivu husema, “Yuko simba barabarani, simba mkali anazunguka mitaa!”
Dice el perezoso: El león está en el camino; el león está en las calles.
14 Kama vile mlango ugeukavyo kwenye bawaba zake, ndivyo mvivu ajigeuzavyo kitandani mwake.
Las puertas se revuelven en sus quicios; así el perezoso en su cama.
15 Mtu mvivu hutumbukiza mkono wake kwenye sahani, naye huchoka kuupeleka kwenye kinywa chake.
Esconde el perezoso su mano en el seno; se cansa de volverla a su boca.
16 Mtu mvivu ni mwenye hekima machoni pake mwenyewe, kuliko watu saba wawezao kujibu kwa busara.
Más sabio es el perezoso en su propia opinión que siete que le den consejo.
17 Kama yeye amkamataye mbwa kwa masikio, ndivyo alivyo mtu apitaye njiani na kujiingiza kwenye ugomvi usiomhusu.
El que pasando se deja llevar de la ira en pleito ajeno, es como el que toma al perro por las orejas.
18 Kama mtu mwendawazimu atupaye vijinga vya moto au mishale ya kufisha,
Como el que enloquece, y echa llamas, y saetas, y muerte,
19 ndivyo alivyo mtu amdanganyaye jirani yake na kusema, “Nilikuwa nikifanya mzaha tu!”
tal es el hombre que daña a su amigo, y dice: Ciertamente lo hice por broma.
20 Bila kuni moto huzimika; pasipo uchongezi ugomvi humalizika.
Sin leña se apaga el fuego; y donde no hay chismoso, cesa la contienda.
21 Kama makaa juu ya makaa yanayowaka, na kama kuni kwenye moto, ndivyo alivyo mtu mgomvi kwa kuchochea ugomvi.
El carbón para brasas, y la leña para el fuego; y el hombre rencilloso para encender contienda.
22 Maneno ya mchongezi ni kama chakula kitamu; huingia sehemu za ndani sana za mtu.
Las palabras del chismoso parecen blandas; mas ellas entran hasta lo secreto del vientre.
23 Kama rangi ingʼaayo iliyopakwa kwenye vyombo vya udongo ndivyo ilivyo midomo laini pamoja na moyo mbaya.
Como escoria de plata echada sobre el tiesto, son los labios enardecidos y el corazón malo.
24 Mtu mwenye nia ya kudhuru wengine hujificha kwa maneno ya midomo yake, lakini moyoni mwake huficha udanganyifu.
El que odia disimula con sus labios; mas en su interior maquina engaño.
25 Ingawa maneno yake huvutia, usimwamini, kwa maana machukizo saba hujaza moyo wake.
Cuando hablare amigablemente, no le creas; porque siete abominaciones hay en su corazón.
26 Nia yake ya kudhuru wengine inaweza kufichwa na udanganyifu, lakini uovu wake utafichuliwa kwenye kusanyiko.
Aunque su odio se encubre en el desierto; su malicia será descubierta en la congregación.
27 Kama mtu akichimba shimo, atatumbukia ndani yake, kama mtu akivingirisha jiwe, litamrudia.
El que cavare sima, caerá en ella; y el que revuelva la piedra, a él volverá.
28 Ulimi wa uongo, huwachukia wale unaowaumiza, nacho kinywa cha kujipendekeza hutenda uharibifu.
La falsa lengua aborrece al que atormenta; y la boca lisonjera hace resbaladero.

< Mithali 26 >