< Mithali 26 >

1 Kama theluji wakati wa kiangazi au mvua wakati wa mavuno, ndivyo asivyostahili heshima mpumbavu.
Якоже роса в жатву и якоже дождь в лете, тако несть безумному чести.
2 Kama shomoro apigapigavyo mabawa yake au mbayuwayu katika kuruka kwake kasi, ndivyo ilivyo laana isiyo na sababu haimpati mtu.
Якоже птицы отлетают и врабиеве, тако клятва суетная не найдет ни на когоже.
3 Mjeledi kwa farasi, lijamu kwa punda, nayo fimbo kwa migongo ya wapumbavu!
Якоже бичь коню и остен ослу, тако жезл языку законопреступну.
4 Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, ama wewe mwenyewe utakuwa kama yeye.
Не отвещай безумному по безумию его, да не подобен ему будеши:
5 Mjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, ama atakuwa mwenye hekima machoni pake mwenyewe.
но отвещай безумному по безумию его, да не явится мудр у себе.
6 Kama vile ilivyo kujikata miguu au kunywa hasara, ndivyo ilivyo kutuma ujumbe kwa mkono wa mpumbavu.
От путий своих поношение творит, иже посла вестником безумным слово.
7 Kama miguu ya kiwete inavyoningʼinia ndivyo ilivyo mithali katika kinywa cha mpumbavu.
Отими шествие от глезн и законопреступление от уст безумных.
8 Kama kufunga jiwe kwenye kombeo, ndivyo ilivyo kumpa mpumbavu heshima.
Иже привязует камень в пращи, подобен есть дающему безумному славу.
9 Kama mwiba kwenye mkono wa mlevi ndivyo ilivyo mithali kinywani mwa mpumbavu.
Терния прозябают в руце пияницы, и порабощение в руце безумных.
10 Kama mpiga upinde ambaye hujeruhi ovyo, ndivyo alivyo yeye aajiriye mpumbavu au yeyote apitaye njiani.
Многими волнуется всяка плоть безумных, сокрушается бо изступление их.
11 Kama mbwa ayarudiavyo matapiko yake, ndivyo mpumbavu arudiavyo upumbavu wake.
Якоже пес, егда возвратится на своя блевотины, и мерзок бывает, тако безумный своею злобою возвращься на свой грех. Есть стыд наводяй грех, и есть стыд слава и благодать.
12 Je, unamwona mtu ajionaye mwenye hekima machoni pake mwenyewe? Liko tumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwake.
Видех мужа непщевавша себе мудра быти, упование же имать безумный паче его.
13 Mvivu husema, “Yuko simba barabarani, simba mkali anazunguka mitaa!”
Глаголет ленивый послан на путь: лев на путех, на стогнах же разбойницы.
14 Kama vile mlango ugeukavyo kwenye bawaba zake, ndivyo mvivu ajigeuzavyo kitandani mwake.
Якоже дверь обращается на пяте, тако ленивый на ложи своем.
15 Mtu mvivu hutumbukiza mkono wake kwenye sahani, naye huchoka kuupeleka kwenye kinywa chake.
Скрыв ленивый руку в недро свое не возможет принести ко устом.
16 Mtu mvivu ni mwenye hekima machoni pake mwenyewe, kuliko watu saba wawezao kujibu kwa busara.
Мудрейший себе ленивый является, паче во изюбилии износящаго весть.
17 Kama yeye amkamataye mbwa kwa masikio, ndivyo alivyo mtu apitaye njiani na kujiingiza kwenye ugomvi usiomhusu.
Якоже держай за ошиб пса, тако председателствуяй чуждему суду.
18 Kama mtu mwendawazimu atupaye vijinga vya moto au mishale ya kufisha,
Якоже врачуемии мещут словеса на человеки, сретаяй же словом первый запнется:
19 ndivyo alivyo mtu amdanganyaye jirani yake na kusema, “Nilikuwa nikifanya mzaha tu!”
тако вси коварствующии над своими други: егда же увидени будут, глаголют, яко играя содеях.
20 Bila kuni moto huzimika; pasipo uchongezi ugomvi humalizika.
Во мнозех древех растет огнь: а идеже несть разгневляюща, умолкает свар.
21 Kama makaa juu ya makaa yanayowaka, na kama kuni kwenye moto, ndivyo alivyo mtu mgomvi kwa kuchochea ugomvi.
Огнище углию, и дрова огневи: муж же клеветлив в мятеж свара.
22 Maneno ya mchongezi ni kama chakula kitamu; huingia sehemu za ndani sana za mtu.
Словеса ласкателей мягка: сия же ударяют в сокровища утроб.
23 Kama rangi ingʼaayo iliyopakwa kwenye vyombo vya udongo ndivyo ilivyo midomo laini pamoja na moyo mbaya.
Сребро даемо с лестию, якоже скудель вменяемо: устне гладки сердце покрывают прискорбно.
24 Mtu mwenye nia ya kudhuru wengine hujificha kwa maneno ya midomo yake, lakini moyoni mwake huficha udanganyifu.
Устнама вся обещавает плачай враг, в сердцы же содевает лесть.
25 Ingawa maneno yake huvutia, usimwamini, kwa maana machukizo saba hujaza moyo wake.
Аще тя молит враг велиим гласом, не веруй ему, седмь бо есть лукавствий в души его.
26 Nia yake ya kudhuru wengine inaweza kufichwa na udanganyifu, lakini uovu wake utafichuliwa kwenye kusanyiko.
Таяй вражду составляет лесть: открывает же своя грехи благоразумный на сонмищих.
27 Kama mtu akichimba shimo, atatumbukia ndani yake, kama mtu akivingirisha jiwe, litamrudia.
Изрываяй яму искреннему впадется в ню: валяяй же камень на себе валит.
28 Ulimi wa uongo, huwachukia wale unaowaumiza, nacho kinywa cha kujipendekeza hutenda uharibifu.
Язык лжив ненавидит истины, уста же непокровенна творят нестроение.

< Mithali 26 >