< Mithali 26 >

1 Kama theluji wakati wa kiangazi au mvua wakati wa mavuno, ndivyo asivyostahili heshima mpumbavu.
Kao snijeg u ljeto i dažd o žetvi, tako ne dolikuje bezumnome èast.
2 Kama shomoro apigapigavyo mabawa yake au mbayuwayu katika kuruka kwake kasi, ndivyo ilivyo laana isiyo na sababu haimpati mtu.
Kao vrabac kad prhne i lasta kad odleti, tako kletva nezaslužena neæe doæi.
3 Mjeledi kwa farasi, lijamu kwa punda, nayo fimbo kwa migongo ya wapumbavu!
Biè konju, uzda magarcu, a batina bezumnicima na leða.
4 Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, ama wewe mwenyewe utakuwa kama yeye.
Ne odgovaraj bezumniku po bezumlju njegovu, da ne budeš i ti kao on.
5 Mjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, ama atakuwa mwenye hekima machoni pake mwenyewe.
Odgovori bezumniku prema bezumlju njegovu, da ne misli da je mudar.
6 Kama vile ilivyo kujikata miguu au kunywa hasara, ndivyo ilivyo kutuma ujumbe kwa mkono wa mpumbavu.
Ko šalje bezumnika da mu što svrši, on otsijeca sebi noge i pije nepravdu.
7 Kama miguu ya kiwete inavyoningʼinia ndivyo ilivyo mithali katika kinywa cha mpumbavu.
Kako hromi hramlje nogama svojim, taka je besjeda u ustima bezumnijeh.
8 Kama kufunga jiwe kwenye kombeo, ndivyo ilivyo kumpa mpumbavu heshima.
Kao da baca dragi kamen u gomilu kamenja, tako radi ko èini èast bezumnome.
9 Kama mwiba kwenye mkono wa mlevi ndivyo ilivyo mithali kinywani mwa mpumbavu.
Kao trn kad doðe u ruku pijanome, taka je besjeda u ustima bezumnijeh.
10 Kama mpiga upinde ambaye hujeruhi ovyo, ndivyo alivyo yeye aajiriye mpumbavu au yeyote apitaye njiani.
Mnogo muke zadaje svjema ko plaæa bezumniku i ko plaæa prestupnicima.
11 Kama mbwa ayarudiavyo matapiko yake, ndivyo mpumbavu arudiavyo upumbavu wake.
Kao što se pas povraæa na svoju bljuvotinu, tako bezumnik ponavlja svoje bezumlje.
12 Je, unamwona mtu ajionaye mwenye hekima machoni pake mwenyewe? Liko tumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwake.
Jesi li vidio èovjeka koji misli da je mudar? više ima nadanja od bezumnoga nego od njega.
13 Mvivu husema, “Yuko simba barabarani, simba mkali anazunguka mitaa!”
Ljenivac govori: ljuti je lav na putu, lav je na ulicama.
14 Kama vile mlango ugeukavyo kwenye bawaba zake, ndivyo mvivu ajigeuzavyo kitandani mwake.
Kao što se vrata obræu na èepovima svojim, tako ljenivac na postelji svojoj.
15 Mtu mvivu hutumbukiza mkono wake kwenye sahani, naye huchoka kuupeleka kwenye kinywa chake.
Ljenivac krije ruku svoju u njedra, teško mu je prinijeti je k ustima.
16 Mtu mvivu ni mwenye hekima machoni pake mwenyewe, kuliko watu saba wawezao kujibu kwa busara.
Ljenivac misli da je mudriji od sedmorice koji odgovaraju razumno.
17 Kama yeye amkamataye mbwa kwa masikio, ndivyo alivyo mtu apitaye njiani na kujiingiza kwenye ugomvi usiomhusu.
Psa za uši hvata ko se prolazeæi žesti za tuðu raspru.
18 Kama mtu mwendawazimu atupaye vijinga vya moto au mishale ya kufisha,
Kakav je bezumnik koji baca iskre i strijele smrtne,
19 ndivyo alivyo mtu amdanganyaye jirani yake na kusema, “Nilikuwa nikifanya mzaha tu!”
Taki je svaki koji prevari bližnjega svojega pa onda veli: šalio sam se.
20 Bila kuni moto huzimika; pasipo uchongezi ugomvi humalizika.
Kad nestane drva, ugasi se oganj; tako kad nema opadaèa, prestaje raspra.
21 Kama makaa juu ya makaa yanayowaka, na kama kuni kwenye moto, ndivyo alivyo mtu mgomvi kwa kuchochea ugomvi.
Ugalj je za žeravicu, drva za oganj, a èovjek svadljivac da raspaljuje svaðu.
22 Maneno ya mchongezi ni kama chakula kitamu; huingia sehemu za ndani sana za mtu.
Rijeèi su opadaèeve kao rijeèi izbijenijeh, ali slaze unutra u trbuh.
23 Kama rangi ingʼaayo iliyopakwa kwenye vyombo vya udongo ndivyo ilivyo midomo laini pamoja na moyo mbaya.
Kao srebrna pjena kojom se obloži crijep, take su usne neprijateljske i zlo srce.
24 Mtu mwenye nia ya kudhuru wengine hujificha kwa maneno ya midomo yake, lakini moyoni mwake huficha udanganyifu.
Nenavidnik se pretvara ustima svojim, a u srcu slaže prijevaru.
25 Ingawa maneno yake huvutia, usimwamini, kwa maana machukizo saba hujaza moyo wake.
Kad govori umiljatijem glasom, ne vjeruj mu, jer mu je u srcu sedam gadova.
26 Nia yake ya kudhuru wengine inaweza kufichwa na udanganyifu, lakini uovu wake utafichuliwa kwenye kusanyiko.
Mržnja se pokriva lukavstvom, ali se zloæa njezina otkriva na zboru.
27 Kama mtu akichimba shimo, atatumbukia ndani yake, kama mtu akivingirisha jiwe, litamrudia.
Ko jamu kopa, u nju æe pasti; i ko kamen valja, na njega æe se prevaliti.
28 Ulimi wa uongo, huwachukia wale unaowaumiza, nacho kinywa cha kujipendekeza hutenda uharibifu.
Jezik lažan mrzi na one koje satire, i usta koja laskaju grade pogibao.

< Mithali 26 >