< Mithali 26 >

1 Kama theluji wakati wa kiangazi au mvua wakati wa mavuno, ndivyo asivyostahili heshima mpumbavu.
Assim como a neve no verão, como a chuva na colheita, assim também não convém a honra para o tolo.
2 Kama shomoro apigapigavyo mabawa yake au mbayuwayu katika kuruka kwake kasi, ndivyo ilivyo laana isiyo na sababu haimpati mtu.
Como um pássaro a vaguear, como a andorinha a voar, assim também a maldição não virá sem causa.
3 Mjeledi kwa farasi, lijamu kwa punda, nayo fimbo kwa migongo ya wapumbavu!
Açoite para o cavalo, cabresto para o asno; e vara para as costas dos tolos.
4 Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, ama wewe mwenyewe utakuwa kama yeye.
Não respondas ao tolo conforme sua loucura; para que não te faças semelhante a ele.
5 Mjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, ama atakuwa mwenye hekima machoni pake mwenyewe.
Responde ao tolo conforme sua loucura, para que ele não seja sábio aos seus próprios olhos.
6 Kama vile ilivyo kujikata miguu au kunywa hasara, ndivyo ilivyo kutuma ujumbe kwa mkono wa mpumbavu.
Quem manda mensagens pelas mãos do tolo é como quem corta os pés e bebe violência.
7 Kama miguu ya kiwete inavyoningʼinia ndivyo ilivyo mithali katika kinywa cha mpumbavu.
[Assim] como não funcionam as pernas do aleijado, assim também é o provérbio na boca dos tolos.
8 Kama kufunga jiwe kwenye kombeo, ndivyo ilivyo kumpa mpumbavu heshima.
Dar honra ao tolo é como amarrar uma pedra numa funda.
9 Kama mwiba kwenye mkono wa mlevi ndivyo ilivyo mithali kinywani mwa mpumbavu.
Como espinho na mão do bêbado, assim é o provérbio na boca dos tolos.
10 Kama mpiga upinde ambaye hujeruhi ovyo, ndivyo alivyo yeye aajiriye mpumbavu au yeyote apitaye njiani.
[Como] um flecheiro que atira para todo lado, [assim] é aquele que contrata um tolo [ou] que contrata alguém que vai passando.
11 Kama mbwa ayarudiavyo matapiko yake, ndivyo mpumbavu arudiavyo upumbavu wake.
Como um cão que volta a seu vômito, [assim] é o tolo que repete sua loucura.
12 Je, unamwona mtu ajionaye mwenye hekima machoni pake mwenyewe? Liko tumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwake.
Viste algum homem sábio aos seus próprios olhos? Mais esperança há para o tolo do que para ele.
13 Mvivu husema, “Yuko simba barabarani, simba mkali anazunguka mitaa!”
O preguiçoso diz: Há uma fera no caminho; há um leão nas ruas.
14 Kama vile mlango ugeukavyo kwenye bawaba zake, ndivyo mvivu ajigeuzavyo kitandani mwake.
[Como] a porta se vira em torno de suas dobradiças, [assim] o preguiçoso [se vira] em sua cama.
15 Mtu mvivu hutumbukiza mkono wake kwenye sahani, naye huchoka kuupeleka kwenye kinywa chake.
O preguiçoso põe sua mão no prato, e acha cansativo demais trazê-la de volta a sua boca.
16 Mtu mvivu ni mwenye hekima machoni pake mwenyewe, kuliko watu saba wawezao kujibu kwa busara.
O preguiçoso se acha mais sábio aos próprios olhos do que sete que respondem com prudência.
17 Kama yeye amkamataye mbwa kwa masikio, ndivyo alivyo mtu apitaye njiani na kujiingiza kwenye ugomvi usiomhusu.
Aquele que, enquanto está passando, [se envolve] em briga que não é sua, é [como] o que pega um cão pelas orelhas.
18 Kama mtu mwendawazimu atupaye vijinga vya moto au mishale ya kufisha,
Como o louco que lança faíscas, flechas e coisas mortíferas,
19 ndivyo alivyo mtu amdanganyaye jirani yake na kusema, “Nilikuwa nikifanya mzaha tu!”
Assim é o homem que engana a seu próximo, e diz: Não estava eu [só] brincando?
20 Bila kuni moto huzimika; pasipo uchongezi ugomvi humalizika.
Sem lenha, o fogo se apaga; e sem fofoqueiro, a briga termina.
21 Kama makaa juu ya makaa yanayowaka, na kama kuni kwenye moto, ndivyo alivyo mtu mgomvi kwa kuchochea ugomvi.
O carvão é para as brasas, e a lenha para o fogo; e o homem difamador para acender brigas.
22 Maneno ya mchongezi ni kama chakula kitamu; huingia sehemu za ndani sana za mtu.
As palavras do fofoqueiro são como alimentos deliciosos, que descem ao interior do ventre.
23 Kama rangi ingʼaayo iliyopakwa kwenye vyombo vya udongo ndivyo ilivyo midomo laini pamoja na moyo mbaya.
Como um vaso de fundição coberto de restos de prata, [assim] são os lábios inflamados e o coração maligno.
24 Mtu mwenye nia ya kudhuru wengine hujificha kwa maneno ya midomo yake, lakini moyoni mwake huficha udanganyifu.
Aquele que odeia dissimula em seus lábios, mas seu interior abriga o engano;
25 Ingawa maneno yake huvutia, usimwamini, kwa maana machukizo saba hujaza moyo wake.
Quando ele [te] falar agradavelmente com sua voz, não acredites nele; porque há sete abominações em seu coração;
26 Nia yake ya kudhuru wengine inaweza kufichwa na udanganyifu, lakini uovu wake utafichuliwa kwenye kusanyiko.
Cujo ódio está encoberto pelo engano; sua maldade será descoberta na congregação.
27 Kama mtu akichimba shimo, atatumbukia ndani yake, kama mtu akivingirisha jiwe, litamrudia.
Quem cava uma cova, nela cairá; e quem rola uma pedra, esta voltará sobre ele.
28 Ulimi wa uongo, huwachukia wale unaowaumiza, nacho kinywa cha kujipendekeza hutenda uharibifu.
A língua falsa odeia aos que ela atormenta; e a boca lisonjeira opera ruína.

< Mithali 26 >