< Mithali 26 >
1 Kama theluji wakati wa kiangazi au mvua wakati wa mavuno, ndivyo asivyostahili heshima mpumbavu.
Como a neve no verão, e como a chuva na sega, assim não convem ao louco a honra.
2 Kama shomoro apigapigavyo mabawa yake au mbayuwayu katika kuruka kwake kasi, ndivyo ilivyo laana isiyo na sababu haimpati mtu.
Como ao passaro o vaguear, como á andorinha o voar, assim a maldição sem causa não virá.
3 Mjeledi kwa farasi, lijamu kwa punda, nayo fimbo kwa migongo ya wapumbavu!
O açoite para o cavallo, o freio para o jumento, e a vara para as costas dos tolos.
4 Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, ama wewe mwenyewe utakuwa kama yeye.
Não respondas ao tolo segundo a sua estulticia; para que tambem te não faças similhante a elle.
5 Mjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, ama atakuwa mwenye hekima machoni pake mwenyewe.
Responde ao tolo segundo a sua estulticia; para que não seja sabio aos seus olhos.
6 Kama vile ilivyo kujikata miguu au kunywa hasara, ndivyo ilivyo kutuma ujumbe kwa mkono wa mpumbavu.
Os pés corta, e o damno bebe, quem manda mensagens pela mão d'um tolo.
7 Kama miguu ya kiwete inavyoningʼinia ndivyo ilivyo mithali katika kinywa cha mpumbavu.
Como as pernas do côxo, que pendem frouxas, assim é o proverbio na bocca dos tolos.
8 Kama kufunga jiwe kwenye kombeo, ndivyo ilivyo kumpa mpumbavu heshima.
Como o que ata a pedra preciosa na funda, assim é aquelle que dá honra ao tolo.
9 Kama mwiba kwenye mkono wa mlevi ndivyo ilivyo mithali kinywani mwa mpumbavu.
Como o espinho que entra na mão do bebado, assim é o proverbio na bocca dos tolos.
10 Kama mpiga upinde ambaye hujeruhi ovyo, ndivyo alivyo yeye aajiriye mpumbavu au yeyote apitaye njiani.
Os grandes molestam a todos, e alugam os tolos e transgressores.
11 Kama mbwa ayarudiavyo matapiko yake, ndivyo mpumbavu arudiavyo upumbavu wake.
Como o cão que torna ao seu vomito, assim é o tolo que reitera a sua estulticia.
12 Je, unamwona mtu ajionaye mwenye hekima machoni pake mwenyewe? Liko tumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwake.
Tens visto a um homem que é sabio a seus proprios olhos? maior esperança ha do tolo do que d'elle.
13 Mvivu husema, “Yuko simba barabarani, simba mkali anazunguka mitaa!”
Diz o preguiçoso: Um leão está no caminho; um leão está nas ruas
14 Kama vile mlango ugeukavyo kwenye bawaba zake, ndivyo mvivu ajigeuzavyo kitandani mwake.
Como a porta se revolve nos seus gonzos, assim o preguiçoso na sua cama.
15 Mtu mvivu hutumbukiza mkono wake kwenye sahani, naye huchoka kuupeleka kwenye kinywa chake.
O preguiçoso esconde a sua mão no seio: enfada-se de tornal-a á sua bocca.
16 Mtu mvivu ni mwenye hekima machoni pake mwenyewe, kuliko watu saba wawezao kujibu kwa busara.
Mais sabio é o preguiçoso a seus olhos do que sete homens que bem respondem.
17 Kama yeye amkamataye mbwa kwa masikio, ndivyo alivyo mtu apitaye njiani na kujiingiza kwenye ugomvi usiomhusu.
O que, passando, se entremette em pleito alheio é como aquelle que toma um cão pelas orelhas.
18 Kama mtu mwendawazimu atupaye vijinga vya moto au mishale ya kufisha,
Como o louco que lança de si faiscas, frechas, e mortandades,
19 ndivyo alivyo mtu amdanganyaye jirani yake na kusema, “Nilikuwa nikifanya mzaha tu!”
Assim é o homem que engana o seu proximo, e diz: Não o fiz eu por brincar?
20 Bila kuni moto huzimika; pasipo uchongezi ugomvi humalizika.
Sem lenha, o fogo se apagará; e, não havendo murmurador, cessará a contenda.
21 Kama makaa juu ya makaa yanayowaka, na kama kuni kwenye moto, ndivyo alivyo mtu mgomvi kwa kuchochea ugomvi.
Como o carvão é para as brazas, e a lenha para o fogo, assim é o homem contencioso para accender rixas.
22 Maneno ya mchongezi ni kama chakula kitamu; huingia sehemu za ndani sana za mtu.
As palavras do murmurador são como as palavras do espancado, e ellas descem ao intimo do ventre.
23 Kama rangi ingʼaayo iliyopakwa kwenye vyombo vya udongo ndivyo ilivyo midomo laini pamoja na moyo mbaya.
Como o caco coberto d'escorias de prata, assim são os labios ardentes com o coração maligno.
24 Mtu mwenye nia ya kudhuru wengine hujificha kwa maneno ya midomo yake, lakini moyoni mwake huficha udanganyifu.
Aquelle que aborrece se contrafaz pelos seus beiços, mas no seu interior encobre o engano.
25 Ingawa maneno yake huvutia, usimwamini, kwa maana machukizo saba hujaza moyo wake.
Quando te supplicar com a sua voz, não te fies n'elle, porque sete abominações ha no seu coração.
26 Nia yake ya kudhuru wengine inaweza kufichwa na udanganyifu, lakini uovu wake utafichuliwa kwenye kusanyiko.
Cujo odio se encobre com engano; a sua malicia se descobrirá na congregação.
27 Kama mtu akichimba shimo, atatumbukia ndani yake, kama mtu akivingirisha jiwe, litamrudia.
O que cava uma cova n'ella cairá; e o que revolve a pedra esta sobre elle tornará.
28 Ulimi wa uongo, huwachukia wale unaowaumiza, nacho kinywa cha kujipendekeza hutenda uharibifu.
A lingua falsa aborrece aos que ella afflige, e a bocca lubrica obra a ruina.