< Mithali 26 >
1 Kama theluji wakati wa kiangazi au mvua wakati wa mavuno, ndivyo asivyostahili heshima mpumbavu.
Jak śnieg w lecie i jak deszcz we żniwa, tak głupiemu nie przystoi chwała.
2 Kama shomoro apigapigavyo mabawa yake au mbayuwayu katika kuruka kwake kasi, ndivyo ilivyo laana isiyo na sababu haimpati mtu.
Jak ptak się tuła [i] jak jaskółka lata, tak nie przyjdzie niezasłużone przekleństwo.
3 Mjeledi kwa farasi, lijamu kwa punda, nayo fimbo kwa migongo ya wapumbavu!
Bicz na konia, wędzidło na osła, a kij na grzbiet głupiego.
4 Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, ama wewe mwenyewe utakuwa kama yeye.
Nie odpowiadaj głupiemu według jego głupoty, abyś i ty nie był do niego podobny.
5 Mjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, ama atakuwa mwenye hekima machoni pake mwenyewe.
Odpowiedz głupiemu według jego głupoty, aby nie był mądry we własnych oczach.
6 Kama vile ilivyo kujikata miguu au kunywa hasara, ndivyo ilivyo kutuma ujumbe kwa mkono wa mpumbavu.
Kto powierza głupiemu posłannictwo, odcina sobie nogi i pije na własną szkodę.
7 Kama miguu ya kiwete inavyoningʼinia ndivyo ilivyo mithali katika kinywa cha mpumbavu.
[Jak] nierówne są nogi chromego, tak przysłowie w ustach głupich.
8 Kama kufunga jiwe kwenye kombeo, ndivyo ilivyo kumpa mpumbavu heshima.
Jaki jest ten, kto przywiązuje kamień do procy, taki ten, kto oddaje cześć głupiemu.
9 Kama mwiba kwenye mkono wa mlevi ndivyo ilivyo mithali kinywani mwa mpumbavu.
Jak cierń wbija się w rękę pijaka, tak przysłowie w ustach głupców.
10 Kama mpiga upinde ambaye hujeruhi ovyo, ndivyo alivyo yeye aajiriye mpumbavu au yeyote apitaye njiani.
Wielki [Bóg] stworzył wszystko i odpłaca głupiemu, odpłaca również przestępcom.
11 Kama mbwa ayarudiavyo matapiko yake, ndivyo mpumbavu arudiavyo upumbavu wake.
[Jak] pies powraca do swoich wymiocin, tak głupi powtarza swoją głupotę.
12 Je, unamwona mtu ajionaye mwenye hekima machoni pake mwenyewe? Liko tumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwake.
Widzisz człowieka, co mądry w swoich oczach? Więcej nadziei dla głupca niż dla niego.
13 Mvivu husema, “Yuko simba barabarani, simba mkali anazunguka mitaa!”
Leniwy mówi: Lew na drodze, lew na ulicach.
14 Kama vile mlango ugeukavyo kwenye bawaba zake, ndivyo mvivu ajigeuzavyo kitandani mwake.
Jak drzwi się obracają na swoich zawiasach, tak leniwy na swoim łóżku.
15 Mtu mvivu hutumbukiza mkono wake kwenye sahani, naye huchoka kuupeleka kwenye kinywa chake.
Leniwy kryje rękę pod pachę, a ciężko mu ją podnosić do ust.
16 Mtu mvivu ni mwenye hekima machoni pake mwenyewe, kuliko watu saba wawezao kujibu kwa busara.
Leniwy uważa się za mądrzejszego niż siedmiu odpowiadających rozsądnie.
17 Kama yeye amkamataye mbwa kwa masikio, ndivyo alivyo mtu apitaye njiani na kujiingiza kwenye ugomvi usiomhusu.
Kto przechodzi i wtrąca się w cudzy spór, jest jak ten, który łapie psa za uszy.
18 Kama mtu mwendawazimu atupaye vijinga vya moto au mishale ya kufisha,
Jak szalony wypuszcza iskry, strzały i śmierć;
19 ndivyo alivyo mtu amdanganyaye jirani yake na kusema, “Nilikuwa nikifanya mzaha tu!”
Taki jest każdy, kto zwodzi swego bliźniego i mówi: Czy nie żartowałem?
20 Bila kuni moto huzimika; pasipo uchongezi ugomvi humalizika.
Gdy nie ma drew, ogień gaśnie; tak gdy nie ma plotkarza, ustaje spór.
21 Kama makaa juu ya makaa yanayowaka, na kama kuni kwenye moto, ndivyo alivyo mtu mgomvi kwa kuchochea ugomvi.
Jak węgiel dla żaru i drwa do ognia, tak kłótliwy człowiek do wzniecenia sporu.
22 Maneno ya mchongezi ni kama chakula kitamu; huingia sehemu za ndani sana za mtu.
Słowa plotkarzy są [jak] rany; przenikają do głębi wnętrzności.
23 Kama rangi ingʼaayo iliyopakwa kwenye vyombo vya udongo ndivyo ilivyo midomo laini pamoja na moyo mbaya.
Palące wargi i złe serce [są jak] gliniana skorupa pokryta żużlem srebrnym.
24 Mtu mwenye nia ya kudhuru wengine hujificha kwa maneno ya midomo yake, lakini moyoni mwake huficha udanganyifu.
Ten, kto nienawidzi, udaje wargami, lecz w sercu knuje podstęp.
25 Ingawa maneno yake huvutia, usimwamini, kwa maana machukizo saba hujaza moyo wake.
Gdy mówi miłym głosem, nie wierz mu, bo siedem obrzydliwości ma w swoim sercu.
26 Nia yake ya kudhuru wengine inaweza kufichwa na udanganyifu, lakini uovu wake utafichuliwa kwenye kusanyiko.
Nienawiść [człowieka] bywa pokryta podstępem, [ale] jego niegodziwość będzie odkryta na zgromadzeniu.
27 Kama mtu akichimba shimo, atatumbukia ndani yake, kama mtu akivingirisha jiwe, litamrudia.
Kto kopie dół, wpadnie w niego; kto kamień toczy, na niego się on obróci.
28 Ulimi wa uongo, huwachukia wale unaowaumiza, nacho kinywa cha kujipendekeza hutenda uharibifu.
Kłamliwy język nienawidzi [tych, których] uciska, a usta pochlebcze prowadzą do zguby.