< Mithali 26 >
1 Kama theluji wakati wa kiangazi au mvua wakati wa mavuno, ndivyo asivyostahili heshima mpumbavu.
Som snø um sumaren og regn i skurden, so høver ikkje æra for ein dåre.
2 Kama shomoro apigapigavyo mabawa yake au mbayuwayu katika kuruka kwake kasi, ndivyo ilivyo laana isiyo na sababu haimpati mtu.
Som sporven flaksar burt og svala flyg, so råkar ikkje grunnlaus forbanning.
3 Mjeledi kwa farasi, lijamu kwa punda, nayo fimbo kwa migongo ya wapumbavu!
Svipa til hesten, taum til asnet, og ris til ryggen på dårar.
4 Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, ama wewe mwenyewe utakuwa kama yeye.
Svar ikkje dåren etter hans dårskap, so du ei skal verta lik han, du og!
5 Mjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, ama atakuwa mwenye hekima machoni pake mwenyewe.
Svara dåren etter hans dårskap, so han ei skal tykkja han sjølv er vis!
6 Kama vile ilivyo kujikata miguu au kunywa hasara, ndivyo ilivyo kutuma ujumbe kwa mkono wa mpumbavu.
Føterne høgg han av seg, og vald fær han drikka, han som sender bod med ein dåre.
7 Kama miguu ya kiwete inavyoningʼinia ndivyo ilivyo mithali katika kinywa cha mpumbavu.
Visne heng vanfør manns føter, so og ordtak i munnen på dårar
8 Kama kufunga jiwe kwenye kombeo, ndivyo ilivyo kumpa mpumbavu heshima.
som å binda ein stein i slyngja, soleis er det å gjeva ein dåre æra.
9 Kama mwiba kwenye mkono wa mlevi ndivyo ilivyo mithali kinywani mwa mpumbavu.
Som klungergrein i handi på drukken mann, so er ordtak i munnen på dårar.
10 Kama mpiga upinde ambaye hujeruhi ovyo, ndivyo alivyo yeye aajiriye mpumbavu au yeyote apitaye njiani.
Som ein skyttar som sårar alle, so er den som leiger dåren og kvar som fer framum.
11 Kama mbwa ayarudiavyo matapiko yake, ndivyo mpumbavu arudiavyo upumbavu wake.
Som hund som snur seg til si eigi spya, so er ein dåre som kjem att til narreskapen sin.
12 Je, unamwona mtu ajionaye mwenye hekima machoni pake mwenyewe? Liko tumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwake.
Ser du ein mann som tykkjer sjølv at han er vis, då er det større von for dåren enn for honom.
13 Mvivu husema, “Yuko simba barabarani, simba mkali anazunguka mitaa!”
Letingen segjer: «D’er villdyr på vegen, ei løva i gatorne.»
14 Kama vile mlango ugeukavyo kwenye bawaba zake, ndivyo mvivu ajigeuzavyo kitandani mwake.
Døri snur seg på gjengi, og letingen snur seg i sengi.
15 Mtu mvivu hutumbukiza mkono wake kwenye sahani, naye huchoka kuupeleka kwenye kinywa chake.
Stikk den late si hand i fatet, han evast med å ta ho upp til munnen att.
16 Mtu mvivu ni mwenye hekima machoni pake mwenyewe, kuliko watu saba wawezao kujibu kwa busara.
Letingen tykkjest visare vera enn sju som gjev vituge svar.
17 Kama yeye amkamataye mbwa kwa masikio, ndivyo alivyo mtu apitaye njiani na kujiingiza kwenye ugomvi usiomhusu.
Han triv i øyro på framumfarande hund, han som ryk upp i sinne for trætta som ikkje kjem han ved.
18 Kama mtu mwendawazimu atupaye vijinga vya moto au mishale ya kufisha,
Som ein galen som skyt med brennende pilar - drepande skot -
19 ndivyo alivyo mtu amdanganyaye jirani yake na kusema, “Nilikuwa nikifanya mzaha tu!”
so er ein mann som svik sin næste og segjer: «Eg gjorde det berre på gaman.»
20 Bila kuni moto huzimika; pasipo uchongezi ugomvi humalizika.
Når veden tryt, so sloknar elden, er baktalar burte, stoggar striden.
21 Kama makaa juu ya makaa yanayowaka, na kama kuni kwenye moto, ndivyo alivyo mtu mgomvi kwa kuchochea ugomvi.
Som kol vert til gløder og ved til eld, so kveikjer kranglaren kiv.
22 Maneno ya mchongezi ni kama chakula kitamu; huingia sehemu za ndani sana za mtu.
Baktalar-ord er som lostemat, dei glid so godt ned i livet.
23 Kama rangi ingʼaayo iliyopakwa kwenye vyombo vya udongo ndivyo ilivyo midomo laini pamoja na moyo mbaya.
Som sylv-glasering på skålbrot er brennande lippor når hjarta er vondt.
24 Mtu mwenye nia ya kudhuru wengine hujificha kwa maneno ya midomo yake, lakini moyoni mwake huficha udanganyifu.
Med lipporne skaper ein uven seg til, men inni seg gøymer han svik.
25 Ingawa maneno yake huvutia, usimwamini, kwa maana machukizo saba hujaza moyo wake.
Gjer han seg blidmælt, tru honom ei, for sju slag styggedom bur i hans hjarta.
26 Nia yake ya kudhuru wengine inaweza kufichwa na udanganyifu, lakini uovu wake utafichuliwa kwenye kusanyiko.
Hatet dyl seg i svik, men lyt syna sin vondskap i folkemugen.
27 Kama mtu akichimba shimo, atatumbukia ndani yake, kama mtu akivingirisha jiwe, litamrudia.
Den som grev ei grav, skal stupa nedi, den som velter ein stein, skal få han yver seg att.
28 Ulimi wa uongo, huwachukia wale unaowaumiza, nacho kinywa cha kujipendekeza hutenda uharibifu.
Den falske tunga hatar deim som ho hev krasa, og den sleipe munnen fører til fall.