< Mithali 26 >
1 Kama theluji wakati wa kiangazi au mvua wakati wa mavuno, ndivyo asivyostahili heshima mpumbavu.
Quomodo nix in æstate, et pluviæ in messe: sic indecens est stulto gloria.
2 Kama shomoro apigapigavyo mabawa yake au mbayuwayu katika kuruka kwake kasi, ndivyo ilivyo laana isiyo na sababu haimpati mtu.
Sicut avis ad alia transvolans, et passer quo libet vadens: sic maledictum frustra prolatum in quempiam superveniet.
3 Mjeledi kwa farasi, lijamu kwa punda, nayo fimbo kwa migongo ya wapumbavu!
Flagellum equo, et camus asino, et virga in dorso imprudentium.
4 Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, ama wewe mwenyewe utakuwa kama yeye.
Ne respondeas stulto iuxta stultitiam suam, ne efficiaris ei similis.
5 Mjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, ama atakuwa mwenye hekima machoni pake mwenyewe.
Responde stulto iuxta stultitiam suam, ne sibi sapiens esse videatur.
6 Kama vile ilivyo kujikata miguu au kunywa hasara, ndivyo ilivyo kutuma ujumbe kwa mkono wa mpumbavu.
Claudus pedibus, et iniquitatem bibens, qui mittit verba per nuncium stultum.
7 Kama miguu ya kiwete inavyoningʼinia ndivyo ilivyo mithali katika kinywa cha mpumbavu.
Quomodo pulchras frustra habet claudus tibias: sic indecens est in ore stultorum parabola.
8 Kama kufunga jiwe kwenye kombeo, ndivyo ilivyo kumpa mpumbavu heshima.
Sicut qui mittit lapidem in acervum Mercurii: ita qui tribuit insipienti honorem.
9 Kama mwiba kwenye mkono wa mlevi ndivyo ilivyo mithali kinywani mwa mpumbavu.
Quomodo si spina nascatur in manu temulenti: sic parabola in ore stultorum.
10 Kama mpiga upinde ambaye hujeruhi ovyo, ndivyo alivyo yeye aajiriye mpumbavu au yeyote apitaye njiani.
Iudicium determinat causas: et qui imponit stulto silentium, iras mitigat.
11 Kama mbwa ayarudiavyo matapiko yake, ndivyo mpumbavu arudiavyo upumbavu wake.
Sicut canis, qui revertitur ad vomitum suum, sic imprudens, qui iterat stultitiam suam.
12 Je, unamwona mtu ajionaye mwenye hekima machoni pake mwenyewe? Liko tumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwake.
Vidisti hominem sapientem sibi videri? magis illo spem habebit insipiens.
13 Mvivu husema, “Yuko simba barabarani, simba mkali anazunguka mitaa!”
Dicit piger: Leo est in via, et leæna in itineribus:
14 Kama vile mlango ugeukavyo kwenye bawaba zake, ndivyo mvivu ajigeuzavyo kitandani mwake.
sicut ostium vertitur in cardine suo, ita piger in lectulo suo.
15 Mtu mvivu hutumbukiza mkono wake kwenye sahani, naye huchoka kuupeleka kwenye kinywa chake.
Abscondit piger manum sub ascella sua, et laborat si ad os suum eam converterit.
16 Mtu mvivu ni mwenye hekima machoni pake mwenyewe, kuliko watu saba wawezao kujibu kwa busara.
Sapientior sibi piger videtur septem viris loquentibus sententias.
17 Kama yeye amkamataye mbwa kwa masikio, ndivyo alivyo mtu apitaye njiani na kujiingiza kwenye ugomvi usiomhusu.
Sicut qui apprehendit auribus canem, sic qui transit impatiens, et commiscetur rixæ alterius.
18 Kama mtu mwendawazimu atupaye vijinga vya moto au mishale ya kufisha,
Sicut noxius est qui mittit sagittas, et lanceas in mortem:
19 ndivyo alivyo mtu amdanganyaye jirani yake na kusema, “Nilikuwa nikifanya mzaha tu!”
ita vir, fraudulenter nocet amico suo: et cum fuerit deprehensus, dicit: Ludens feci.
20 Bila kuni moto huzimika; pasipo uchongezi ugomvi humalizika.
Cum defecerint ligna, extinguetur ignis: et susurrone subtracto, iurgia conquiescent.
21 Kama makaa juu ya makaa yanayowaka, na kama kuni kwenye moto, ndivyo alivyo mtu mgomvi kwa kuchochea ugomvi.
Sicut carbones ad prunas, et ligna ad ignem, sic homo iracundus suscitat rixas.
22 Maneno ya mchongezi ni kama chakula kitamu; huingia sehemu za ndani sana za mtu.
Verba susurronis quasi simplicia, et ipsa perveniunt ad intima ventris.
23 Kama rangi ingʼaayo iliyopakwa kwenye vyombo vya udongo ndivyo ilivyo midomo laini pamoja na moyo mbaya.
Quomodo si argento sordido ornare velis vas fictile, sic labia tumentia cum pessimo corde sociata.
24 Mtu mwenye nia ya kudhuru wengine hujificha kwa maneno ya midomo yake, lakini moyoni mwake huficha udanganyifu.
Labiis suis intelligitur inimicus, cum in corde tractaverit dolos.
25 Ingawa maneno yake huvutia, usimwamini, kwa maana machukizo saba hujaza moyo wake.
Quando submiserit vocem suam, ne credideris ei: quoniam septem nequitiæ sunt in corde illius.
26 Nia yake ya kudhuru wengine inaweza kufichwa na udanganyifu, lakini uovu wake utafichuliwa kwenye kusanyiko.
Qui operit odium fraudulenter, revelabitur malitia eius in consilio.
27 Kama mtu akichimba shimo, atatumbukia ndani yake, kama mtu akivingirisha jiwe, litamrudia.
Qui fodit foveam, incidet in eam: et qui volvit lapidem, revertetur ad eum.
28 Ulimi wa uongo, huwachukia wale unaowaumiza, nacho kinywa cha kujipendekeza hutenda uharibifu.
Lingua fallax non amat veritatem: et os lubricum operatur ruinas.