< Mithali 26 >

1 Kama theluji wakati wa kiangazi au mvua wakati wa mavuno, ndivyo asivyostahili heshima mpumbavu.
Il y a des rosées pendant la moisson, et des pluies pendant l'été; mais il n'est point de gloire pour l'insensé.
2 Kama shomoro apigapigavyo mabawa yake au mbayuwayu katika kuruka kwake kasi, ndivyo ilivyo laana isiyo na sababu haimpati mtu.
Les oiseaux s'envolent et même les autruches: ainsi les vanités s'évanouissent sans arriver à rien.
3 Mjeledi kwa farasi, lijamu kwa punda, nayo fimbo kwa migongo ya wapumbavu!
Comme est le fouet au cheval, l'aiguillon à l'âne, ainsi est la verge à une nature déréglée.
4 Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, ama wewe mwenyewe utakuwa kama yeye.
Ne réponds point au fou selon sa folie, de peur que tu ne deviennes semblable à lui.
5 Mjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, ama atakuwa mwenye hekima machoni pake mwenyewe.
Mais réponds au fou selon sa folie, de peur qu'il ne semble sage à tes dépens.
6 Kama vile ilivyo kujikata miguu au kunywa hasara, ndivyo ilivyo kutuma ujumbe kwa mkono wa mpumbavu.
Celui qui envoie ses paroles par un messager imprudent expose ses propres voies à un affront.
7 Kama miguu ya kiwete inavyoningʼinia ndivyo ilivyo mithali katika kinywa cha mpumbavu.
Interdis aux insensés l'usage de leurs jambes, et empêche l'iniquité de sortir de leur bouche.
8 Kama kufunga jiwe kwenye kombeo, ndivyo ilivyo kumpa mpumbavu heshima.
Celui qui attache la pierre à sa fronde ressemble à celui qui glorifie un insensé.
9 Kama mwiba kwenye mkono wa mlevi ndivyo ilivyo mithali kinywani mwa mpumbavu.
Des épines poussent dans la main d'un homme ivre, et la servitude dans la main des insensés.
10 Kama mpiga upinde ambaye hujeruhi ovyo, ndivyo alivyo yeye aajiriye mpumbavu au yeyote apitaye njiani.
La chair des insensés est pleine de trouble; car leurs passions se brisent dans leur choc.
11 Kama mbwa ayarudiavyo matapiko yake, ndivyo mpumbavu arudiavyo upumbavu wake.
Comme le chien, lorsqu'il revient à son vomissement, inspire le dégoût; ainsi est l'insensé qui, en sa malice, retourne à son péché. Il est une honte qui conduit au mal; il est une honte pleine de gloire et de grâce.
12 Je, unamwona mtu ajionaye mwenye hekima machoni pake mwenyewe? Liko tumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwake.
J'ai vu un homme qui, lui-même, s'estimait sage; cependant l'insensé a plus de confiance que lui.
13 Mvivu husema, “Yuko simba barabarani, simba mkali anazunguka mitaa!”
Le paresseux que l'on envoie en voyage dit: Il y a un lion sur le chemin et des assassins dans les rues.
14 Kama vile mlango ugeukavyo kwenye bawaba zake, ndivyo mvivu ajigeuzavyo kitandani mwake.
Comme la porte tourne sur ses gonds, ainsi fait le paresseux sur son lit.
15 Mtu mvivu hutumbukiza mkono wake kwenye sahani, naye huchoka kuupeleka kwenye kinywa chake.
Le paresseux, s'il a caché sa main sous son manteau, n'aura pas le courage de la porter à sa bouche.
16 Mtu mvivu ni mwenye hekima machoni pake mwenyewe, kuliko watu saba wawezao kujibu kwa busara.
Le paresseux se croit plus sage que celui qui rapporte une dépêche et en reçoit un salaire abondant.
17 Kama yeye amkamataye mbwa kwa masikio, ndivyo alivyo mtu apitaye njiani na kujiingiza kwenye ugomvi usiomhusu.
Se mettre en avant pour la querelle d'autrui, c'est comme prendre un chien par la queue.
18 Kama mtu mwendawazimu atupaye vijinga vya moto au mishale ya kufisha,
On lance parmi les hommes des paroles comme des traits; celui qu'elles atteignent le premier succombe.
19 ndivyo alivyo mtu amdanganyaye jirani yake na kusema, “Nilikuwa nikifanya mzaha tu!”
C'est ce qui arrive à tous ceux qui dressent des embûches à leurs amis; et si l'on s'en aperçoit, ils disent: Je l'ai fait en jouant.
20 Bila kuni moto huzimika; pasipo uchongezi ugomvi humalizika.
Le feu s'active, s'il y a beaucoup de bois; où il n'y a point de contradicteur, les querelles s'apaisent.
21 Kama makaa juu ya makaa yanayowaka, na kama kuni kwenye moto, ndivyo alivyo mtu mgomvi kwa kuchochea ugomvi.
Le charbon et le bois dans le foyer animent le feu; le médisant entretient le trouble des querelles.
22 Maneno ya mchongezi ni kama chakula kitamu; huingia sehemu za ndani sana za mtu.
Les paroles du trompeur sont douces; mais elles blessent jusqu'au fond des entrailles.
23 Kama rangi ingʼaayo iliyopakwa kwenye vyombo vya udongo ndivyo ilivyo midomo laini pamoja na moyo mbaya.
L'argent donné pour tromper ne vaut pas mieux qu'un coquillage. Des lèvres frivoles cachent un mauvais cœur.
24 Mtu mwenye nia ya kudhuru wengine hujificha kwa maneno ya midomo yake, lakini moyoni mwake huficha udanganyifu.
Un ennemi que l'on voit pleurer promet beaucoup des lèvres; mais en son cœur il trame quelque fraude.
25 Ingawa maneno yake huvutia, usimwamini, kwa maana machukizo saba hujaza moyo wake.
Si ton ennemi te prie à grands cris, ne te laisse pas persuader; car il a sept méchancetés dans l'âme.
26 Nia yake ya kudhuru wengine inaweza kufichwa na udanganyifu, lakini uovu wake utafichuliwa kwenye kusanyiko.
Celui qui dissimule sa haine cherche à tromper; mais il a beau cacher ses fautes, le monde le connaît bien.
27 Kama mtu akichimba shimo, atatumbukia ndani yake, kama mtu akivingirisha jiwe, litamrudia.
Celui qui creuse une fosse pour son prochain y tombera; celui qui roule une pierre la roule sur lui-même.
28 Ulimi wa uongo, huwachukia wale unaowaumiza, nacho kinywa cha kujipendekeza hutenda uharibifu.
Une langue trompeuse hait la vérité; une bouche indiscrète est une cause de ruines.

< Mithali 26 >