< Mithali 26 >

1 Kama theluji wakati wa kiangazi au mvua wakati wa mavuno, ndivyo asivyostahili heshima mpumbavu.
Yhtä vähän kuin lumi kesällä ja sade elonaikana soveltuu tyhmälle kunnia.
2 Kama shomoro apigapigavyo mabawa yake au mbayuwayu katika kuruka kwake kasi, ndivyo ilivyo laana isiyo na sababu haimpati mtu.
Kuin liitävä lintu, kuin lentävä pääskynen on aiheeton kirous: ei se toteen käy.
3 Mjeledi kwa farasi, lijamu kwa punda, nayo fimbo kwa migongo ya wapumbavu!
Hevoselle ruoska, aasille suitset, tyhmille vitsa selkään!
4 Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, ama wewe mwenyewe utakuwa kama yeye.
Älä vastaa tyhmälle hänen hulluutensa mukaan, ettet olisi hänen kaltaisensa sinäkin.
5 Mjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, ama atakuwa mwenye hekima machoni pake mwenyewe.
Vastaa tyhmälle hänen hulluutensa mukaan, ettei hän itseänsä viisaana pitäisi.
6 Kama vile ilivyo kujikata miguu au kunywa hasara, ndivyo ilivyo kutuma ujumbe kwa mkono wa mpumbavu.
Jalat altaan katkaisee ja vääryyttä saa juoda, joka sanan lähettää tyhmän mukana.
7 Kama miguu ya kiwete inavyoningʼinia ndivyo ilivyo mithali katika kinywa cha mpumbavu.
Velttoina riippuvat halvatun sääret; samoin sananlasku tyhmäin suussa.
8 Kama kufunga jiwe kwenye kombeo, ndivyo ilivyo kumpa mpumbavu heshima.
Yhtä kuin sitoisi kiven linkoon kiinni, on antaa kunniaa tyhmälle.
9 Kama mwiba kwenye mkono wa mlevi ndivyo ilivyo mithali kinywani mwa mpumbavu.
Kuin ohdake, joka on osunut juopuneen käteen, on sananlasku tyhmäin suussa.
10 Kama mpiga upinde ambaye hujeruhi ovyo, ndivyo alivyo yeye aajiriye mpumbavu au yeyote apitaye njiani.
Kuin jousimies, joka kaikkia haavoittaa, on se, joka tyhmän pestaa, kulkureita pestaa.
11 Kama mbwa ayarudiavyo matapiko yake, ndivyo mpumbavu arudiavyo upumbavu wake.
Kuin koira, joka palajaa oksennuksilleen, on tyhmä, joka yhä uusii hulluuksiansa.
12 Je, unamwona mtu ajionaye mwenye hekima machoni pake mwenyewe? Liko tumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwake.
Näet miehen, viisaan omissa silmissään-enemmän on toivoa tyhmästä kuin hänestä.
13 Mvivu husema, “Yuko simba barabarani, simba mkali anazunguka mitaa!”
Laiska sanoo: "Tuolla tiellä on leijona, jalopeura torien vaiheilla".
14 Kama vile mlango ugeukavyo kwenye bawaba zake, ndivyo mvivu ajigeuzavyo kitandani mwake.
Ovi saranoillaan kääntyilee, laiska vuoteellansa.
15 Mtu mvivu hutumbukiza mkono wake kwenye sahani, naye huchoka kuupeleka kwenye kinywa chake.
Laiska pistää kätensä vatiin; ei viitsi sitä viedä suuhunsa jälleen.
16 Mtu mvivu ni mwenye hekima machoni pake mwenyewe, kuliko watu saba wawezao kujibu kwa busara.
Laiska on omissa silmissään viisaampi kuin seitsemän, jotka vastaavat taitavasti.
17 Kama yeye amkamataye mbwa kwa masikio, ndivyo alivyo mtu apitaye njiani na kujiingiza kwenye ugomvi usiomhusu.
Kulkukoiraa korviin tarttuu se, joka syrjäisten riidasta suuttuu.
18 Kama mtu mwendawazimu atupaye vijinga vya moto au mishale ya kufisha,
Kuin mieletön, joka ammuskelee tulisia surmannuolia,
19 ndivyo alivyo mtu amdanganyaye jirani yake na kusema, “Nilikuwa nikifanya mzaha tu!”
on mies, joka pettää lähimmäisensä ja sanoo: "Leikillähän minä sen tein".
20 Bila kuni moto huzimika; pasipo uchongezi ugomvi humalizika.
Halkojen loppuessa sammuu tuli, ja panettelijan poistuessa taukoaa tora.
21 Kama makaa juu ya makaa yanayowaka, na kama kuni kwenye moto, ndivyo alivyo mtu mgomvi kwa kuchochea ugomvi.
Hehkuksi hiilet, tuleksi halot, riidan lietsomiseksi toraisa mies.
22 Maneno ya mchongezi ni kama chakula kitamu; huingia sehemu za ndani sana za mtu.
Panettelijan puheet ovat kuin herkkupalat ja painuvat sisusten kammioihin asti.
23 Kama rangi ingʼaayo iliyopakwa kwenye vyombo vya udongo ndivyo ilivyo midomo laini pamoja na moyo mbaya.
Kuin hopeasilaus saviastian pinnalla ovat hehkuvat huulet ja paha sydän.
24 Mtu mwenye nia ya kudhuru wengine hujificha kwa maneno ya midomo yake, lakini moyoni mwake huficha udanganyifu.
Vihamies teeskentelee huulillaan, mutta hautoo petosta sydämessänsä.
25 Ingawa maneno yake huvutia, usimwamini, kwa maana machukizo saba hujaza moyo wake.
Jos hän muuttaa suloiseksi äänensä, älä häntä usko, sillä seitsemän kauhistusta hänellä on sydämessä.
26 Nia yake ya kudhuru wengine inaweza kufichwa na udanganyifu, lakini uovu wake utafichuliwa kwenye kusanyiko.
Vihamielisyys kätkeytyy kavalasti, mutta seurakunnan kokouksessa sen pahuus paljastuu.
27 Kama mtu akichimba shimo, atatumbukia ndani yake, kama mtu akivingirisha jiwe, litamrudia.
Joka kuopan kaivaa, se itse siihen lankeaa; ja joka kiveä vierittää, sen päälle se takaisin vyörähtää.
28 Ulimi wa uongo, huwachukia wale unaowaumiza, nacho kinywa cha kujipendekeza hutenda uharibifu.
Valheellinen kieli vihaa omia ruhjomiansa, ja liukas suu saa turmiota aikaan.

< Mithali 26 >