< Mithali 25 >

1 Hizi ni mithali zaidi za Solomoni, zilizonakiliwa na watu wa Hezekia mfalme wa Yuda:
Estas son palabras sabias de Salomón, copiadas por los hombres de Ezequías, rey de Judá.
2 Ni Utukufu wa Mungu kuficha jambo, bali ni utukufu wa wafalme kuchunguza jambo.
Es la gloria de Dios guardar una cosa en secreto; pero la gloria de los reyes es escudriñarlos.
3 Kama mbingu zilivyo juu na nchi ilivyo chini, ndivyo ambavyo mioyo ya wafalme haichunguziki.
La altura del cielo y la profundidad de la tierra, no se pueden buscar, como el corazón de los reyes.
4 Ondoa takataka kwenye madini ya fedha, nako ndani yake kutatokea chombo cha mfua fedha.
Quita el deshecho de la plata, y una vasija saldrá para el obrero de la plata.
5 Ondoa waovu mbele ya mfalme, nacho kiti chake cha enzi kitaimarishwa kwa njia ya haki.
Quita a los malvados de delante del rey, y el trono de su poder se fortalecerá en justicia.
6 Usijikweze mwenyewe mbele ya mfalme, wala usidai nafasi miongoni mwa watu wakuu;
No te glorifiques delante del rey, ni te pongas en el lugar de los grandes:
7 ni afadhali yeye akuambie, “Njoo huku juu,” kuliko yeye kukuaibisha mbele ya mkuu. Kile ulichokiona kwa macho yako
Porque mejor es que te diga: Sube acá; que para que seas puesto en un lugar inferior ante el gobernante.
8 usiharakishe kukipeleka mahakamani, maana utafanya nini mwishoni kama jirani yako atakuaibisha?
No te apures en ir a la ley sobre lo que has visto, porque ¿qué harás al final, cuando tu prójimo te avergüence?
9 Kama ukifanya shauri na jirani yako, usisaliti siri ya mtu mwingine,
Habla con tu prójimo acerca de tu causa, pero no des reveles el secreto de otro:
10 ama yeye aisikiaye aweza kukuaibisha na kamwe sifa yako mbaya haitaondoka.
O tu oyente puede decir mal de ti, y tu vergüenza no podrá repararse.
11 Neno lisemwalo kwa wakati ufaao ni kama matunda ya mtofaa ya dhahabu yaliyowekwa kwenye vijalizo vya fedha.
Una palabra en el momento correcto es como manzanas de oro en una red de plata.
12 Kama vile kipuli cha dhahabu au pambo la dhahabu safi, ndivyo lilivyo karipio la mtu mwenye hekima kwa sikio lisikilizalo.
Como un anillo en la nariz de oro y un adorno del mejor oro, es un hombre sabio que da palabras de corrección a un oído listo para prestar atención.
13 Kama vile ubaridi wa theluji wakati wa mavuno ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwa wale wamtumao, huburudisha roho za bwana zake.
Como el frío de la nieve en el tiempo de cortar el grano, así es un verdadero siervo de los que lo envían; porque da nueva vida al alma de su maestro.
14 Kama vile mawingu na upepo pasipo mvua ndivyo alivyo mtu ajisifuye kwa zawadi ambazo hatoi.
Como nubes y viento sin lluvia, así es el que toma el crédito de una ofrenda que no ha dado.
15 Kwa njia ya uvumilivu mtawala aweza kushawishiwa, nao ulimi laini waweza kuvunja mfupa.
Un juez es movido por uno que durante mucho tiempo sufre errores sin protestar, y con palabras suaves incluso el hueso se rompe.
16 Ukipata asali, kula kiasi tu cha kukutosha, ukila zaidi, utatapika.
Si tienes miel, toma solo lo que sea suficiente para ti; por temor a que, al estar lleno de eso, la vomites.
17 Ingiza mguu wako nyumbani kwa jirani yako mara chache, ukizidisha, atakukinai na atakuchukia.
No pongas tu pie con frecuencia en la casa de tu prójimo, o él puede cansarse de ti, y su sentimiento se convertirá en odio.
18 Kama vile rungu au upanga au mshale mkali ndivyo alivyo mtu atoaye ushuhuda wa uongo dhidi ya jirani yake.
El que da falso testimonio contra su prójimo es un martillo, una espada y una flecha filosa.
19 Kama vile jino bovu au mguu uliolemaa, ndivyo ilivyo kumtegemea mtu asiye mwaminifu wakati wa shida.
Poner la fe en un hombre falso en tiempo de angustia es como un diente roto y un pie tembloroso.
20 Kama vile avuaye mavazi siku ya baridi, au kama siki iliyomwagwa juu ya magadi, ndivyo alivyo yeye amuimbiaye nyimbo mtu mwenye moyo mzito.
Como el que se quita la ropa en clima frío y como el ácido en una herida, es el que hace melodía a un corazón triste.
21 Kama adui yako ana njaa, mpe chakula ale; kama ana kiu, mpe maji anywe.
Si tu enemigo tiene necesidad de alimento, dale pan; y si tiene necesidad de beber, dale agua;
22 Kwa kufanya hivyo, unaweka makaa ya moto yanayowaka kichwani pake, naye Bwana atakupa thawabu.
porque así pondrás brasas de fuego sobre su cabeza, y el Señor te dará tu recompensa.
23 Kama vile upepo wa kaskazini uletavyo mvua, ndivyo ulimi usingiziao uletavyo uso wa hasira.
Como el viento del norte da a luz a la lluvia, así es un rostro enojado causado por una lengua que dice mal en secreto.
24 Ni afadhali kuishi pembeni mwa paa la nyumba, kuliko kuishi nyumba moja na mke mgomvi.
Es mejor vivir en un ángulo de la parte superior de la casa, que con una mujer de lengua amarga en una casa amplia.
25 Kama vile maji baridi kwa nafsi iliyochoka ndivyo zilivyo habari njema kutoka nchi ya mbali.
Como agua fría para un alma cansada, también lo son las buenas noticias de un país lejano.
26 Kama vile chemchemi iliyotibuliwa matope au kisima kilichotiwa taka ndivyo alivyo mtu mwenye haki akishiriki na waovu.
Como una fuente turbulenta y una fuente sucia, es un hombre recto que tiene que ceder ante los malvados.
27 Si vyema kula asali nyingi sana, wala si heshima kujitafutia heshima yako mwenyewe.
No es bueno comer mucha miel: así que el que no está buscando honor será honrado.
28 Kama vile mji ambao kuta zake zimebomoka ndivyo alivyo mtu ambaye hawezi kujitawala mwenyewe.
Aquel cuyo espíritu está descontrolado es como una ciudad sin muro que ha sido quebrantada.

< Mithali 25 >