< Mithali 25 >
1 Hizi ni mithali zaidi za Solomoni, zilizonakiliwa na watu wa Hezekia mfalme wa Yuda:
И ово су приче Соломунове које сабраше људи Језекије цара Јудиног.
2 Ni Utukufu wa Mungu kuficha jambo, bali ni utukufu wa wafalme kuchunguza jambo.
Слава је Божија скривати ствар, а слава је царска истраживати ствар.
3 Kama mbingu zilivyo juu na nchi ilivyo chini, ndivyo ambavyo mioyo ya wafalme haichunguziki.
Висина небу и дубина земљи и срце царевима не може се досегнути.
4 Ondoa takataka kwenye madini ya fedha, nako ndani yake kutatokea chombo cha mfua fedha.
Узми од сребра троску, и изаћи ће ливцу заклад.
5 Ondoa waovu mbele ya mfalme, nacho kiti chake cha enzi kitaimarishwa kwa njia ya haki.
Узми безбожника испред цара, и утврдиће се правдом престо његов.
6 Usijikweze mwenyewe mbele ya mfalme, wala usidai nafasi miongoni mwa watu wakuu;
Не величај се пред царем и не стај на место где стоје властељи.
7 ni afadhali yeye akuambie, “Njoo huku juu,” kuliko yeye kukuaibisha mbele ya mkuu. Kile ulichokiona kwa macho yako
Јер је боље да ти се каже: Ходи горе, него да те понизе пред кнезом да видиш својим очима.
8 usiharakishe kukipeleka mahakamani, maana utafanya nini mwishoni kama jirani yako atakuaibisha?
Не иди одмах да се преш, гледај шта би чинио напослетку ако би те осрамотио ближњи твој.
9 Kama ukifanya shauri na jirani yako, usisaliti siri ya mtu mwingine,
Расправи ствар своју с ближњим својим, али туђе тајне не откривај,
10 ama yeye aisikiaye aweza kukuaibisha na kamwe sifa yako mbaya haitaondoka.
Да те не би псовао ко чује, и срамота твоја да не би остала на теби.
11 Neno lisemwalo kwa wakati ufaao ni kama matunda ya mtofaa ya dhahabu yaliyowekwa kwenye vijalizo vya fedha.
Златне јабуке у сребрним судима јесу згодне речи.
12 Kama vile kipuli cha dhahabu au pambo la dhahabu safi, ndivyo lilivyo karipio la mtu mwenye hekima kwa sikio lisikilizalo.
Златна је гривна и накит од најбољег злата мудри карач ономе који слуша.
13 Kama vile ubaridi wa theluji wakati wa mavuno ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwa wale wamtumao, huburudisha roho za bwana zake.
Веран је посланик као студен снежна о жетви онима који га пошаљу, и расхлађује душу својим господарима.
14 Kama vile mawingu na upepo pasipo mvua ndivyo alivyo mtu ajisifuye kwa zawadi ambazo hatoi.
Ко се хвали даром лажним, он је као облаци и ветар без дажда.
15 Kwa njia ya uvumilivu mtawala aweza kushawishiwa, nao ulimi laini waweza kuvunja mfupa.
Стрпљењем се ублажава кнез, и мек језик ломи кости.
16 Ukipata asali, kula kiasi tu cha kukutosha, ukila zaidi, utatapika.
Кад нађеш мед, једи колико ти је доста, да не би наједавши га се избљувао га.
17 Ingiza mguu wako nyumbani kwa jirani yako mara chache, ukizidisha, atakukinai na atakuchukia.
Ретко нека ти нога ступа у кућу ближњег твог, да не би наситивши се тебе омрзао на те.
18 Kama vile rungu au upanga au mshale mkali ndivyo alivyo mtu atoaye ushuhuda wa uongo dhidi ya jirani yake.
Ко год говори лажно сведочанство на ближњег свог, он је као маљ и мач и оштра стрела.
19 Kama vile jino bovu au mguu uliolemaa, ndivyo ilivyo kumtegemea mtu asiye mwaminifu wakati wa shida.
Уздање је у неверника у невољи зуб сломљен и нога уганута.
20 Kama vile avuaye mavazi siku ya baridi, au kama siki iliyomwagwa juu ya magadi, ndivyo alivyo yeye amuimbiaye nyimbo mtu mwenye moyo mzito.
Ко пева песме жалосном срцу, он је као онај који свлачи хаљину на зими, и као оцат на салитру.
21 Kama adui yako ana njaa, mpe chakula ale; kama ana kiu, mpe maji anywe.
Ако је гладан ненавидник твој, нахрани га хлеба, и ако је жедан напој га воде.
22 Kwa kufanya hivyo, unaweka makaa ya moto yanayowaka kichwani pake, naye Bwana atakupa thawabu.
Јер ћеш живо угљевље згрнути на главу његову, и Господ ће ти платити.
23 Kama vile upepo wa kaskazini uletavyo mvua, ndivyo ulimi usingiziao uletavyo uso wa hasira.
Северни ветар носи дажд, а потајни језик лице срдито.
24 Ni afadhali kuishi pembeni mwa paa la nyumba, kuliko kuishi nyumba moja na mke mgomvi.
Боље је седети у углу од крова него са женом свадљивом у кући заједничкој.
25 Kama vile maji baridi kwa nafsi iliyochoka ndivyo zilivyo habari njema kutoka nchi ya mbali.
Добар је глас из далеке земље као студена вода жедној души.
26 Kama vile chemchemi iliyotibuliwa matope au kisima kilichotiwa taka ndivyo alivyo mtu mwenye haki akishiriki na waovu.
Праведник који пада пред безбожником јесте као извор ногама замућен и као студенац покварен.
27 Si vyema kula asali nyingi sana, wala si heshima kujitafutia heshima yako mwenyewe.
Јести много меда није добро, и истраживати славу није славно.
28 Kama vile mji ambao kuta zake zimebomoka ndivyo alivyo mtu ambaye hawezi kujitawala mwenyewe.
Ко нема власти над духом својим, он је град разваљен без зидова.