< Mithali 25 >

1 Hizi ni mithali zaidi za Solomoni, zilizonakiliwa na watu wa Hezekia mfalme wa Yuda:
Voici encore des Proverbes de Salomon, recueillis par les gens d'Ézéchias, roi de Juda.
2 Ni Utukufu wa Mungu kuficha jambo, bali ni utukufu wa wafalme kuchunguza jambo.
La gloire de Dieu, c'est de cacher les choses; la gloire des rois, c'est de les examiner.
3 Kama mbingu zilivyo juu na nchi ilivyo chini, ndivyo ambavyo mioyo ya wafalme haichunguziki.
Le ciel dans sa hauteur, la terre dans sa profondeur, et le cœur des rois sont impénétrables.
4 Ondoa takataka kwenye madini ya fedha, nako ndani yake kutatokea chombo cha mfua fedha.
Ote les scories de l'argent, et il en sortira un vase pour le fondeur.
5 Ondoa waovu mbele ya mfalme, nacho kiti chake cha enzi kitaimarishwa kwa njia ya haki.
Ote le méchant de devant le roi, et son trône s'affermira dans la justice.
6 Usijikweze mwenyewe mbele ya mfalme, wala usidai nafasi miongoni mwa watu wakuu;
Ne prends pas des airs superbes devant le roi, et ne te mets pas à la place des grands;
7 ni afadhali yeye akuambie, “Njoo huku juu,” kuliko yeye kukuaibisha mbele ya mkuu. Kile ulichokiona kwa macho yako
car il vaut mieux qu'on te dise: « Monte ici », que si l'on t'humilie devant le prince que tes yeux ont vu.
8 usiharakishe kukipeleka mahakamani, maana utafanya nini mwishoni kama jirani yako atakuaibisha?
Ne pars pas trop vite en contestation, de peur qu'à la fin tu ne saches que faire.
9 Kama ukifanya shauri na jirani yako, usisaliti siri ya mtu mwingine,
Lorsque ton prochain t'aura outragé, défends ta cause contre ton prochain, mais ne révèle pas le secret d'un autre,
10 ama yeye aisikiaye aweza kukuaibisha na kamwe sifa yako mbaya haitaondoka.
de peur que celui qui l'apprendra ne te couvre de honte, et que ton ignominie ne s'efface pas.
11 Neno lisemwalo kwa wakati ufaao ni kama matunda ya mtofaa ya dhahabu yaliyowekwa kwenye vijalizo vya fedha.
Comme des pommes d'or sur des ciselures d'argent, ainsi est une parole dite à propos.
12 Kama vile kipuli cha dhahabu au pambo la dhahabu safi, ndivyo lilivyo karipio la mtu mwenye hekima kwa sikio lisikilizalo.
Comme un anneau d'or et un ornement d'or fin, ainsi est le sage qui reprend une oreille docile.
13 Kama vile ubaridi wa theluji wakati wa mavuno ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwa wale wamtumao, huburudisha roho za bwana zake.
Comme la fraîcheur de la neige au temps de la moisson, ainsi est le messager fidèle pour ceux qui l'envoient; il réjouit l'âme de son maître.
14 Kama vile mawingu na upepo pasipo mvua ndivyo alivyo mtu ajisifuye kwa zawadi ambazo hatoi.
Des nuages et du vent sans pluie, tel est l'homme qui se glorifie de présents mensongers.
15 Kwa njia ya uvumilivu mtawala aweza kushawishiwa, nao ulimi laini waweza kuvunja mfupa.
Par la patience le juge se laisse persuader, et une langue douce peut briser des os.
16 Ukipata asali, kula kiasi tu cha kukutosha, ukila zaidi, utatapika.
Si tu trouves du miel, n'en mange que ce qui te suffit, de peur que, rassasié, tu ne le vomisses.
17 Ingiza mguu wako nyumbani kwa jirani yako mara chache, ukizidisha, atakukinai na atakuchukia.
Mets rarement le pied dans la maison de ton prochain, de peur que, fatigué de toi, il ne te haïsse.
18 Kama vile rungu au upanga au mshale mkali ndivyo alivyo mtu atoaye ushuhuda wa uongo dhidi ya jirani yake.
Une massue, une épée et une flèche aiguë, tel est l'homme qui porte un faux témoignage contre son prochain.
19 Kama vile jino bovu au mguu uliolemaa, ndivyo ilivyo kumtegemea mtu asiye mwaminifu wakati wa shida.
Une dent cassée et un pied qui glisse, c'est la confiance qu'inspire un perfide au jour du malheur.
20 Kama vile avuaye mavazi siku ya baridi, au kama siki iliyomwagwa juu ya magadi, ndivyo alivyo yeye amuimbiaye nyimbo mtu mwenye moyo mzito.
Oter son manteau un jour de froid, répandre du vinaigre sur du nitre, ainsi fait celui qui dit des chansons à un cœur affligé.
21 Kama adui yako ana njaa, mpe chakula ale; kama ana kiu, mpe maji anywe.
Si ton ennemi a faim, donne-lui du pain à manger; s'il a soif, donne-lui de l'eau à boire;
22 Kwa kufanya hivyo, unaweka makaa ya moto yanayowaka kichwani pake, naye Bwana atakupa thawabu.
car tu amasses ainsi des charbons sur sa tête, et Yahweh te récompensera.
23 Kama vile upepo wa kaskazini uletavyo mvua, ndivyo ulimi usingiziao uletavyo uso wa hasira.
Le vent du nord enfante la pluie, et la langue qui médit en secret, un visage irrité.
24 Ni afadhali kuishi pembeni mwa paa la nyumba, kuliko kuishi nyumba moja na mke mgomvi.
Mieux vaut habiter à l'angle d'un toit, que de rester avec une femme querelleuse.
25 Kama vile maji baridi kwa nafsi iliyochoka ndivyo zilivyo habari njema kutoka nchi ya mbali.
De l'eau fraîche pour une personne altérée, telle est une bonne nouvelle venant d'une terre lointaine.
26 Kama vile chemchemi iliyotibuliwa matope au kisima kilichotiwa taka ndivyo alivyo mtu mwenye haki akishiriki na waovu.
Une fontaine troublée et une source corrompue, tel est le juste qui chancelle devant le méchant.
27 Si vyema kula asali nyingi sana, wala si heshima kujitafutia heshima yako mwenyewe.
Il n'est pas bon de manger beaucoup de miel; ainsi celui qui veut sonder la majesté divine sera accablé par sa gloire.
28 Kama vile mji ambao kuta zake zimebomoka ndivyo alivyo mtu ambaye hawezi kujitawala mwenyewe.
Une ville forcée qui n'a plus de murailles, tel est l'homme qui ne peut se contenir.

< Mithali 25 >