< Mithali 25 >

1 Hizi ni mithali zaidi za Solomoni, zilizonakiliwa na watu wa Hezekia mfalme wa Yuda:
Also these are the proverbs of Solomon, which the men of Hezekiah the king of Judah have collected.
2 Ni Utukufu wa Mungu kuficha jambo, bali ni utukufu wa wafalme kuchunguza jambo.
It is the honor of God to conceal a thing; but the honor of kings is to search out a matter.
3 Kama mbingu zilivyo juu na nchi ilivyo chini, ndivyo ambavyo mioyo ya wafalme haichunguziki.
As are the heavens for height, and the earth is for depth, so should the heart of kings be unsearchable.
4 Ondoa takataka kwenye madini ya fedha, nako ndani yake kutatokea chombo cha mfua fedha.
Take away the dross from the silver, and there will come forth a vessel for the melter.
5 Ondoa waovu mbele ya mfalme, nacho kiti chake cha enzi kitaimarishwa kwa njia ya haki.
Take away the wicked from before the king, and his throne will be firmly established in righteousness.
6 Usijikweze mwenyewe mbele ya mfalme, wala usidai nafasi miongoni mwa watu wakuu;
Do not glorify thyself in the presence of the king, and force thyself not into the place of great men;
7 ni afadhali yeye akuambie, “Njoo huku juu,” kuliko yeye kukuaibisha mbele ya mkuu. Kile ulichokiona kwa macho yako
For better it is that it be said unto thee, “Come up hither,” than that thou shouldst be put lower in the presence of the prince, which thy own eyes have [often] seen.
8 usiharakishe kukipeleka mahakamani, maana utafanya nini mwishoni kama jirani yako atakuaibisha?
Do not proceed to a contest hastily, lest [thou know not] what thou wilt have to do at its end, when thy neighbor hath put thee to confusion.
9 Kama ukifanya shauri na jirani yako, usisaliti siri ya mtu mwingine,
Carry on thy cause with thy neighbor; but lay not open the secret of another:
10 ama yeye aisikiaye aweza kukuaibisha na kamwe sifa yako mbaya haitaondoka.
Lest he that heareth it put thee to shame, and thy infamy never be removed.
11 Neno lisemwalo kwa wakati ufaao ni kama matunda ya mtofaa ya dhahabu yaliyowekwa kwenye vijalizo vya fedha.
Like apples of gold among figures of silver is a word spoken in a proper manner.
12 Kama vile kipuli cha dhahabu au pambo la dhahabu safi, ndivyo lilivyo karipio la mtu mwenye hekima kwa sikio lisikilizalo.
As an earring of gold, and a pendant of fine gold, so is a wise reprover toward an ear that listeneth.
13 Kama vile ubaridi wa theluji wakati wa mavuno ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwa wale wamtumao, huburudisha roho za bwana zake.
As the cooling of snow on a harvest-day, so is a faithful messenger to those that send him; for he refresheth the soul of his master.
14 Kama vile mawingu na upepo pasipo mvua ndivyo alivyo mtu ajisifuye kwa zawadi ambazo hatoi.
Like clouds and wind without rain, so is a man that vaunteth falsely of a gift.
15 Kwa njia ya uvumilivu mtawala aweza kushawishiwa, nao ulimi laini waweza kuvunja mfupa.
By long forbearing is a prince persuaded, and a soft tongue breaketh bones.
16 Ukipata asali, kula kiasi tu cha kukutosha, ukila zaidi, utatapika.
Hast thou found honey: eat so much as is sufficient for thee: lest thou consume too much of it, and have to vomit it forth.
17 Ingiza mguu wako nyumbani kwa jirani yako mara chache, ukizidisha, atakukinai na atakuchukia.
Make thy foot scarce in the house of thy friend: lest he have too much of thee, and so hate thee.
18 Kama vile rungu au upanga au mshale mkali ndivyo alivyo mtu atoaye ushuhuda wa uongo dhidi ya jirani yake.
A battle-axe, and a sword, and a sharpened arrow is a man that testifieth as a false witness against his neighbor.
19 Kama vile jino bovu au mguu uliolemaa, ndivyo ilivyo kumtegemea mtu asiye mwaminifu wakati wa shida.
Like a broken tooth and a foot out of joint, is confidence in a treacherous man in a time of distress.
20 Kama vile avuaye mavazi siku ya baridi, au kama siki iliyomwagwa juu ya magadi, ndivyo alivyo yeye amuimbiaye nyimbo mtu mwenye moyo mzito.
[As] he that taketh off his garment on a cold day, [as] vinegar is upon natron: so is he that singeth songs before an unhappy heart.
21 Kama adui yako ana njaa, mpe chakula ale; kama ana kiu, mpe maji anywe.
If thy enemy be hungry, give him bread to eat; and if he be thirsty, give him water to drink;
22 Kwa kufanya hivyo, unaweka makaa ya moto yanayowaka kichwani pake, naye Bwana atakupa thawabu.
For though thou gatherest coals of fire upon his head, yet will the Lord repay it unto thee.
23 Kama vile upepo wa kaskazini uletavyo mvua, ndivyo ulimi usingiziao uletavyo uso wa hasira.
The north wind bringeth forth rain: so doth secret talking, angry countenances.
24 Ni afadhali kuishi pembeni mwa paa la nyumba, kuliko kuishi nyumba moja na mke mgomvi.
It is better to dwell in the corner of a roof, than with a quarrelsome woman even in a roomy house.
25 Kama vile maji baridi kwa nafsi iliyochoka ndivyo zilivyo habari njema kutoka nchi ya mbali.
As cold water is to a fainting soul, so are good news from a far-off country.
26 Kama vile chemchemi iliyotibuliwa matope au kisima kilichotiwa taka ndivyo alivyo mtu mwenye haki akishiriki na waovu.
Like a turbid spring and a corrupt fountain, is a righteous man that giveth way before the wicked.
27 Si vyema kula asali nyingi sana, wala si heshima kujitafutia heshima yako mwenyewe.
To eat too much honey is not good: so is it honor to set a limit to men's honor.
28 Kama vile mji ambao kuta zake zimebomoka ndivyo alivyo mtu ambaye hawezi kujitawala mwenyewe.
Like a city that is broken in, and is without walls: so is the man that hath no control over his spirit.

< Mithali 25 >