< Mithali 25 >

1 Hizi ni mithali zaidi za Solomoni, zilizonakiliwa na watu wa Hezekia mfalme wa Yuda:
These are more wise sayings of Solomon, copied out by the men of Hezekiah, king of Judah.
2 Ni Utukufu wa Mungu kuficha jambo, bali ni utukufu wa wafalme kuchunguza jambo.
It is the glory of God to keep a thing secret: but the glory of kings is to have it searched out.
3 Kama mbingu zilivyo juu na nchi ilivyo chini, ndivyo ambavyo mioyo ya wafalme haichunguziki.
The heaven is high and the earth is deep, and the hearts of kings may not be searched out.
4 Ondoa takataka kwenye madini ya fedha, nako ndani yake kutatokea chombo cha mfua fedha.
Take away the waste from silver, and a vessel will come out for the silver-worker.
5 Ondoa waovu mbele ya mfalme, nacho kiti chake cha enzi kitaimarishwa kwa njia ya haki.
Take away evil-doers from before the king, and the seat of his power will be made strong in righteousness.
6 Usijikweze mwenyewe mbele ya mfalme, wala usidai nafasi miongoni mwa watu wakuu;
Do not take glory for yourself before the king, and do not put yourself in the place of the great:
7 ni afadhali yeye akuambie, “Njoo huku juu,” kuliko yeye kukuaibisha mbele ya mkuu. Kile ulichokiona kwa macho yako
For it is better to have it said to you, Come up here; than for you to be put down in a lower place before the ruler.
8 usiharakishe kukipeleka mahakamani, maana utafanya nini mwishoni kama jirani yako atakuaibisha?
Do not be quick to go to law about what you have seen, for what will you do in the end, when your neighbour has put you to shame?
9 Kama ukifanya shauri na jirani yako, usisaliti siri ya mtu mwingine,
Have a talk with your neighbour himself about your cause, but do not give away the secret of another:
10 ama yeye aisikiaye aweza kukuaibisha na kamwe sifa yako mbaya haitaondoka.
Or your hearer may say evil of you, and your shame will not be turned away.
11 Neno lisemwalo kwa wakati ufaao ni kama matunda ya mtofaa ya dhahabu yaliyowekwa kwenye vijalizo vya fedha.
A word at the right time is like apples of gold in a network of silver.
12 Kama vile kipuli cha dhahabu au pambo la dhahabu safi, ndivyo lilivyo karipio la mtu mwenye hekima kwa sikio lisikilizalo.
Like a nose-ring of gold and an ornament of the best gold, is a wise man who says sharp words to an ear ready to give attention.
13 Kama vile ubaridi wa theluji wakati wa mavuno ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwa wale wamtumao, huburudisha roho za bwana zake.
As the cold of snow in the time of grain-cutting, so is a true servant to those who send him; for he gives new life to the soul of his master.
14 Kama vile mawingu na upepo pasipo mvua ndivyo alivyo mtu ajisifuye kwa zawadi ambazo hatoi.
As clouds and wind without rain, so is one who takes credit for an offering he has not given.
15 Kwa njia ya uvumilivu mtawala aweza kushawishiwa, nao ulimi laini waweza kuvunja mfupa.
A judge is moved by one who for a long time undergoes wrongs without protest, and by a soft tongue even bone is broken.
16 Ukipata asali, kula kiasi tu cha kukutosha, ukila zaidi, utatapika.
If you have honey, take only as much as is enough for you; for fear that, being full of it, you may not be able to keep it down.
17 Ingiza mguu wako nyumbani kwa jirani yako mara chache, ukizidisha, atakukinai na atakuchukia.
Let not your foot be frequently in your neighbour's house, or he may get tired of you, and his feeling be turned to hate.
18 Kama vile rungu au upanga au mshale mkali ndivyo alivyo mtu atoaye ushuhuda wa uongo dhidi ya jirani yake.
One who gives false witness against his neighbour is a hammer and a sword and a sharp arrow.
19 Kama vile jino bovu au mguu uliolemaa, ndivyo ilivyo kumtegemea mtu asiye mwaminifu wakati wa shida.
Putting one's faith in a false man in time of trouble is like a broken tooth and a shaking foot.
20 Kama vile avuaye mavazi siku ya baridi, au kama siki iliyomwagwa juu ya magadi, ndivyo alivyo yeye amuimbiaye nyimbo mtu mwenye moyo mzito.
Like one who takes off clothing in cold weather and like acid on a wound, is he who makes melody to a sad heart.
21 Kama adui yako ana njaa, mpe chakula ale; kama ana kiu, mpe maji anywe.
If your hater is in need of food, give him bread; and if he is in need of drink, give him water:
22 Kwa kufanya hivyo, unaweka makaa ya moto yanayowaka kichwani pake, naye Bwana atakupa thawabu.
For so you will put coals of fire on his head, and the Lord will give you your reward.
23 Kama vile upepo wa kaskazini uletavyo mvua, ndivyo ulimi usingiziao uletavyo uso wa hasira.
As the north wind gives birth to rain, so is an angry face caused by a tongue saying evil secretly.
24 Ni afadhali kuishi pembeni mwa paa la nyumba, kuliko kuishi nyumba moja na mke mgomvi.
It is better to be living in an angle of the house-top, than with a bitter-tongued woman in a wide house.
25 Kama vile maji baridi kwa nafsi iliyochoka ndivyo zilivyo habari njema kutoka nchi ya mbali.
As cold water to a tired soul, so is good news from a far country.
26 Kama vile chemchemi iliyotibuliwa matope au kisima kilichotiwa taka ndivyo alivyo mtu mwenye haki akishiriki na waovu.
Like a troubled fountain and a dirty spring, is an upright man who has to give way before evil-doers.
27 Si vyema kula asali nyingi sana, wala si heshima kujitafutia heshima yako mwenyewe.
It is not good to take much honey: so he who is not looking for honour will be honoured.
28 Kama vile mji ambao kuta zake zimebomoka ndivyo alivyo mtu ambaye hawezi kujitawala mwenyewe.
He whose spirit is uncontrolled is like an unwalled town which has been broken into.

< Mithali 25 >