< Mithali 25 >

1 Hizi ni mithali zaidi za Solomoni, zilizonakiliwa na watu wa Hezekia mfalme wa Yuda:
These are additional proverbs of Solomon, which were copied by the men of Hezekiah king of Judah:
2 Ni Utukufu wa Mungu kuficha jambo, bali ni utukufu wa wafalme kuchunguza jambo.
It is the glory of God to conceal a matter and the glory of kings to search it out.
3 Kama mbingu zilivyo juu na nchi ilivyo chini, ndivyo ambavyo mioyo ya wafalme haichunguziki.
As the heavens are high and the earth is deep, so the hearts of kings cannot be searched.
4 Ondoa takataka kwenye madini ya fedha, nako ndani yake kutatokea chombo cha mfua fedha.
Remove the dross from the silver, and a vessel for a silversmith will come forth.
5 Ondoa waovu mbele ya mfalme, nacho kiti chake cha enzi kitaimarishwa kwa njia ya haki.
Remove the wicked from the king’s presence, and his throne will be established in righteousness.
6 Usijikweze mwenyewe mbele ya mfalme, wala usidai nafasi miongoni mwa watu wakuu;
Do not exalt yourself in the presence of the king, and do not stand in the place of great men;
7 ni afadhali yeye akuambie, “Njoo huku juu,” kuliko yeye kukuaibisha mbele ya mkuu. Kile ulichokiona kwa macho yako
for it is better that he says to you, “Come up here!” than that you should be demoted in the presence of the prince. Even what you have seen with your own eyes,
8 usiharakishe kukipeleka mahakamani, maana utafanya nini mwishoni kama jirani yako atakuaibisha?
do not bring hastily to court. Otherwise, what will you do in the end when your neighbor puts you to shame?
9 Kama ukifanya shauri na jirani yako, usisaliti siri ya mtu mwingine,
Argue your case with your neighbor without betraying another’s confidence,
10 ama yeye aisikiaye aweza kukuaibisha na kamwe sifa yako mbaya haitaondoka.
lest the one who hears may disgrace you, and your infamy never go away.
11 Neno lisemwalo kwa wakati ufaao ni kama matunda ya mtofaa ya dhahabu yaliyowekwa kwenye vijalizo vya fedha.
A word fitly spoken is like apples of gold in settings of silver.
12 Kama vile kipuli cha dhahabu au pambo la dhahabu safi, ndivyo lilivyo karipio la mtu mwenye hekima kwa sikio lisikilizalo.
Like an earring of gold or an ornament of fine gold is a wise man’s rebuke to a listening ear.
13 Kama vile ubaridi wa theluji wakati wa mavuno ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwa wale wamtumao, huburudisha roho za bwana zake.
Like the cold of snow in the time of harvest is a trustworthy messenger to those who send him; he refreshes the soul of his masters.
14 Kama vile mawingu na upepo pasipo mvua ndivyo alivyo mtu ajisifuye kwa zawadi ambazo hatoi.
Like clouds and wind without rain is the man who boasts of gifts never given.
15 Kwa njia ya uvumilivu mtawala aweza kushawishiwa, nao ulimi laini waweza kuvunja mfupa.
Through patience a ruler can be persuaded, and a gentle tongue can break a bone.
16 Ukipata asali, kula kiasi tu cha kukutosha, ukila zaidi, utatapika.
If you find honey, eat just what you need, lest you have too much and vomit it up.
17 Ingiza mguu wako nyumbani kwa jirani yako mara chache, ukizidisha, atakukinai na atakuchukia.
Seldom set foot in your neighbor’s house, lest he grow weary and hate you.
18 Kama vile rungu au upanga au mshale mkali ndivyo alivyo mtu atoaye ushuhuda wa uongo dhidi ya jirani yake.
Like a club or sword or sharp arrow is a man who bears false witness against his neighbor.
19 Kama vile jino bovu au mguu uliolemaa, ndivyo ilivyo kumtegemea mtu asiye mwaminifu wakati wa shida.
Like a broken tooth or a foot out of joint is confidence in a faithless man in time of trouble.
20 Kama vile avuaye mavazi siku ya baridi, au kama siki iliyomwagwa juu ya magadi, ndivyo alivyo yeye amuimbiaye nyimbo mtu mwenye moyo mzito.
Like one who removes a garment on a cold day or vinegar poured on a wound is one who sings songs to a heavy heart.
21 Kama adui yako ana njaa, mpe chakula ale; kama ana kiu, mpe maji anywe.
If your enemy is hungry, give him food to eat, and if he is thirsty, give him water to drink.
22 Kwa kufanya hivyo, unaweka makaa ya moto yanayowaka kichwani pake, naye Bwana atakupa thawabu.
For in so doing, you will heap burning coals on his head, and the LORD will reward you.
23 Kama vile upepo wa kaskazini uletavyo mvua, ndivyo ulimi usingiziao uletavyo uso wa hasira.
As the north wind brings forth rain, so a backbiting tongue brings angry looks.
24 Ni afadhali kuishi pembeni mwa paa la nyumba, kuliko kuishi nyumba moja na mke mgomvi.
Better to live on a corner of the roof than to share a house with a quarrelsome wife.
25 Kama vile maji baridi kwa nafsi iliyochoka ndivyo zilivyo habari njema kutoka nchi ya mbali.
Like cold water to a weary soul is good news from a distant land.
26 Kama vile chemchemi iliyotibuliwa matope au kisima kilichotiwa taka ndivyo alivyo mtu mwenye haki akishiriki na waovu.
Like a muddied spring or a polluted well is a righteous man who gives way to the wicked.
27 Si vyema kula asali nyingi sana, wala si heshima kujitafutia heshima yako mwenyewe.
It is not good to eat too much honey or to search out one’s own glory.
28 Kama vile mji ambao kuta zake zimebomoka ndivyo alivyo mtu ambaye hawezi kujitawala mwenyewe.
Like a city whose walls are broken down is a man who does not control his temper.

< Mithali 25 >