< Mithali 25 >

1 Hizi ni mithali zaidi za Solomoni, zilizonakiliwa na watu wa Hezekia mfalme wa Yuda:
Jaké i tato jsou přísloví Šalomounova, kteráž shromáždili muži Ezechiáše, krále Judského:
2 Ni Utukufu wa Mungu kuficha jambo, bali ni utukufu wa wafalme kuchunguza jambo.
Sláva Boží jest skrývati věc, ale sláva králů zpytovati věc.
3 Kama mbingu zilivyo juu na nchi ilivyo chini, ndivyo ambavyo mioyo ya wafalme haichunguziki.
Vysokosti nebes, a hlubokosti země, a srdce králů není žádného vystižení.
4 Ondoa takataka kwenye madini ya fedha, nako ndani yake kutatokea chombo cha mfua fedha.
Jako když bys odjal trůsku od stříbra, ukáže se slevači nádoba čistá:
5 Ondoa waovu mbele ya mfalme, nacho kiti chake cha enzi kitaimarishwa kwa njia ya haki.
Tak když odejmeš bezbožného od oblíčeje králova, tedy utvrzen bude v spravedlnosti trůn jeho.
6 Usijikweze mwenyewe mbele ya mfalme, wala usidai nafasi miongoni mwa watu wakuu;
Nestavěj se za znamenitého před králem, a na místě velikých nestůj.
7 ni afadhali yeye akuambie, “Njoo huku juu,” kuliko yeye kukuaibisha mbele ya mkuu. Kile ulichokiona kwa macho yako
Nebo lépe jest, aťby řečeno bylo: Vstup sem, nežli abys snížen byl před knížetem; což vídávají oči tvé.
8 usiharakishe kukipeleka mahakamani, maana utafanya nini mwishoni kama jirani yako atakuaibisha?
Nevcházej v svár kvapně, tak abys naposledy něčeho se nedopustil, kdyby tě zahanbil bližní tvůj.
9 Kama ukifanya shauri na jirani yako, usisaliti siri ya mtu mwingine,
Srovnej při svou s bližním svým, a tajné věci jiného nevyjevuj,
10 ama yeye aisikiaye aweza kukuaibisha na kamwe sifa yako mbaya haitaondoka.
Aťby lehkosti neučinil ten, kdož by to slyšel, až by i zlá pověst tvá nemohla jíti nazpět.
11 Neno lisemwalo kwa wakati ufaao ni kama matunda ya mtofaa ya dhahabu yaliyowekwa kwenye vijalizo vya fedha.
Jablka zlatá s řezbami stříbrnými jest slovo propověděné případně.
12 Kama vile kipuli cha dhahabu au pambo la dhahabu safi, ndivyo lilivyo karipio la mtu mwenye hekima kwa sikio lisikilizalo.
Náušnice zlatá a ozdoba z ryzího zlata jest trestatel moudrý u toho, jenž poslouchá.
13 Kama vile ubaridi wa theluji wakati wa mavuno ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwa wale wamtumao, huburudisha roho za bwana zake.
Jako studenost sněžná v čas žně, tak jest posel věrný těm, kteříž jej posílají; nebo duši pánů svých očerstvuje.
14 Kama vile mawingu na upepo pasipo mvua ndivyo alivyo mtu ajisifuye kwa zawadi ambazo hatoi.
Jako oblakové a vítr bez deště, tak člověk, kterýž se chlubí darem lživým.
15 Kwa njia ya uvumilivu mtawala aweza kushawishiwa, nao ulimi laini waweza kuvunja mfupa.
Snášelivostí nakloněn bývá vývoda, a jazyk měkký láme kosti.
16 Ukipata asali, kula kiasi tu cha kukutosha, ukila zaidi, utatapika.
Nalezneš-li med, jez, pokudž by dosti bylo tobě, abys snad nasycen jsa jím, nevyvrátil ho.
17 Ingiza mguu wako nyumbani kwa jirani yako mara chache, ukizidisha, atakukinai na atakuchukia.
Zdržuj nohu svou od domu bližního svého, aby syt jsa tebe, neměl tě v nenávisti.
18 Kama vile rungu au upanga au mshale mkali ndivyo alivyo mtu atoaye ushuhuda wa uongo dhidi ya jirani yake.
Kladivo a meč a střela ostrá jest každý, kdož mluví falešné svědectví proti bližnímu svému.
19 Kama vile jino bovu au mguu uliolemaa, ndivyo ilivyo kumtegemea mtu asiye mwaminifu wakati wa shida.
Zub vylomený a noha vytknutá jest doufání v převráceném v den úzkosti.
20 Kama vile avuaye mavazi siku ya baridi, au kama siki iliyomwagwa juu ya magadi, ndivyo alivyo yeye amuimbiaye nyimbo mtu mwenye moyo mzito.
Jako ten, kdož svláčí oděv v čas zimy, a ocet lije k sanitru, tak kdož zpívá písničky srdci smutnému.
21 Kama adui yako ana njaa, mpe chakula ale; kama ana kiu, mpe maji anywe.
Jestliže by lačněl ten, jenž tě nenávidí, nakrm jej chlebem, a žíznil-li by, napoj jej vodou.
22 Kwa kufanya hivyo, unaweka makaa ya moto yanayowaka kichwani pake, naye Bwana atakupa thawabu.
Nebo uhlí řeřavé shromáždíš na hlavu jeho, a Hospodin odplatí tobě.
23 Kama vile upepo wa kaskazini uletavyo mvua, ndivyo ulimi usingiziao uletavyo uso wa hasira.
Vítr půlnoční zplozuje déšť, a tvář hněvivá jazyk tajně utrhající.
24 Ni afadhali kuishi pembeni mwa paa la nyumba, kuliko kuishi nyumba moja na mke mgomvi.
Lépe jest bydliti v koutě na střeše, nežli s ženou svárlivou v domě společném.
25 Kama vile maji baridi kwa nafsi iliyochoka ndivyo zilivyo habari njema kutoka nchi ya mbali.
Voda studená duši ustalé jest novina dobrá z země daleké.
26 Kama vile chemchemi iliyotibuliwa matope au kisima kilichotiwa taka ndivyo alivyo mtu mwenye haki akishiriki na waovu.
Studnice nohami zakalená a pramen zkažený jest spravedlivý z místa svého před bezbožným vystrčený.
27 Si vyema kula asali nyingi sana, wala si heshima kujitafutia heshima yako mwenyewe.
Jísti mnoho medu není dobře; tak zpytování slávy jejich není slavné.
28 Kama vile mji ambao kuta zake zimebomoka ndivyo alivyo mtu ambaye hawezi kujitawala mwenyewe.
Město rozbořené beze zdi jest muž, kterýž nemá moci nad duchem svým.

< Mithali 25 >