< Mithali 24 >
1 Usiwaonee wivu watu waovu, usitamani ushirika nao;
No envidies a los perversos, Ni desees estar con ellos.
2 kwa maana mioyo yao hupanga mambo ya jeuri, nayo midomo yao husema juu ya kuleta madhara.
Porque su corazón trama violencia, Y sus labios hablan gran injusticia.
3 Kwa hekima nyumba hujengwa, nayo kwa njia ya ufahamu huimarishwa
Con la sabiduría se edifica una casa, Con la prudencia se afirma,
4 kwa njia ya maarifa vyumba vyake hujazwa vitu vya thamani na vya kupendeza.
Con el conocimiento se llenan sus cuartos De todo bien preciado y agradable.
5 Mtu mwenye hekima ana uwezo mkubwa, naye mtu mwenye maarifa huongeza nguvu,
Mejor es el varón sabio que el fuerte. El hombre de conocimiento aumenta su poder.
6 kwa kufanya vita unahitaji uongozi na kwa ushindi washauri wengi.
Porque con estrategia harás tu guerra, Y en la multitud de consejeros está la victoria.
7 Hekima i juu mno kwa mpumbavu, katika kusanyiko langoni hana lolote la kusema.
La sabiduría está demasiado alta para el necio. En la puerta no abrirá su boca.
8 Yeye apangaye mabaya atajulikana kama mtu wa hila.
Al que trama el mal Lo llamarán hombre de malas intenciones.
9 Mipango ya upumbavu ni dhambi, watu huchukizwa na mwenye dhihaka.
La intención del insensato es pecado, El burlador es detestado por los hombres.
10 Ukikata tamaa wakati wa taabu, jinsi gani nguvu zako ni kidogo!
Si flaqueas en el día de la adversidad, También tu fuerza se reducirá.
11 Okoa wale wanaoongozwa kwenye kifo; wazuie wote wanaojikokota kuelekea machinjoni.
¡Libra a los que son llevados a la muerte! ¡Rescata a los que se tambalean hacia a la matanza!
12 Kama mkisema, “Lakini hatukujua lolote kuhusu hili,” je, yule apimaye mioyo halitambui hili? Je, yule awalindaye maisha yenu halijui hili? Je, hatamlipa kila mtu kulingana na aliyotenda?
Si dices: En verdad, no lo supimos. El que pesa los corazones, ¿no lo sabrá? ¿No lo sabrá el que vigila tu vida, Y paga al hombre según sus obras?
13 Ule asali mwanangu, kwa kuwa ni nzuri; asali kutoka kwenye sega ni tamu kwa kuonja.
Come miel, hijo mío, pues es buena. Sí, el panal es dulce a tu paladar.
14 Ujue pia kwamba hekima ni tamu kwa nafsi yako, kama ukiipata, kuna matumaini kwako ya siku zijazo, nalo tumaini lako halitakatiliwa mbali.
Así aprópiate de la sabiduría para tu vida. Si la hallas, habrá un porvenir, Y tu esperanza no será frustrada.
15 Usivizie kama haramia afanyavyo ili kuyashambulia makao ya mwenye haki, wala usiyavamie makazi yake,
Oh impío, no aceches la tienda del justo Ni saquees su lugar de reposo,
16 Kwa maana ingawa mtu mwenye haki huanguka mara saba, huinuka tena, lakini waovu huangushwa chini na maafa.
Porque siete veces cae el justo y se vuelve a levantar, Pero los impíos tropiezan en la calamidad.
17 Usitazame kwa kufurahia adui yako aangukapo; wakati ajikwaapo, usiruhusu moyo wako ushangilie.
Si tu enemigo cae, no te alegres, Y si tropieza, no se regocije tu corazón,
18 Bwana asije akaona na kuchukia akaiondoa ghadhabu yake mbali naye.
No sea que Yavé lo vea y le desagrade, Y aparte de sobre él su enojo.
19 Usikasirike kwa sababu ya watu wabaya wala usiwaonee wivu waovu,
No te impacientes a causa de los malhechores, Ni tengas envidia de los pecadores,
20 kwa maana mtu mbaya hana tumaini la siku zijazo, nayo taa ya waovu itazimwa.
Porque para el perverso no habrá buen fin, Y la lámpara de los impíos será apagada.
21 Mwanangu, mche Bwana na mfalme, wala usijiunge na waasi,
Hijo mío: Teme a Yavé y también al rey. No te asocies con los sediciosos,
22 kwa maana hao wawili watatuma maangamizi ya ghafula juu yao, naye ni nani ajuaye maafa wawezayo kuleta?
Porque su calamidad viene de repente, Y la ruina que viene de ambos, ¿quién la conocerá?
23 Hii pia ni misemo ya wenye hekima: Kuonyesha upendeleo katika hukumu si vyema:
También estos son dichos de los sabios: No es bueno hacer acepción de personas en el juicio.
24 Yeyote amwambiaye mwenye hatia, “Wewe huna hatia,” Kabila zitamlaani na mataifa yatamkana.
El que dice al impío: Eres justo, Lo maldecirán los pueblos, Y lo detestarán las naciones.
25 Bali itakuwa vyema kwa wale watakaowatia hatiani wenye hatia, nazo baraka tele zitawajilia juu yao.
Pero los que lo reprenden serán apreciados, Y una gran bendición vendrá sobre ellos.
26 Jawabu la uaminifu ni kama busu la midomoni.
Besados serán los labios Del que responde palabras rectas.
27 Maliza kazi zako za nje, nawe uweke mashamba yako tayari, baada ya hayo, jenga nyumba yako.
Prepara tus labores de afuera, Y disponlas en tus campos, Y después edifica tu casa.
28 Usishuhudie dhidi ya jirani yako bila sababu, au kutumia midomo yako kudanganya.
No testifiques sin causa contra tu prójimo, Ni engañes con tus labios.
29 Usiseme, “Nitamtenda kama alivyonitenda mimi; nitamlipiza mtu yule kwa kile alichonitendea.”
No digas: Le haré como él me hizo, Le retribuiré conforme a su obra.
30 Nilipita karibu na shamba la mvivu, karibu na shamba la mizabibu la mtu asiye na akili,
Pasé junto al campo de un hombre perezoso, Por la viña de un hombre falto de entendimiento,
31 miiba ilikuwa imeota kila mahali, ardhi ilikuwa imefunikwa na magugu, na ukuta wa mawe ulikuwa umebomoka.
Y ahí todo estaba cubierto de espinas. Su superficie estaba cubierta de ortigas, Y su muro de piedra, derribado.
32 Nikatafakari moyoni mwangu lile nililoliona, nami nikajifunza somo kutokana na niliyoyaona:
Observé esto y reflexioné. Lo vi y aprendí la lección:
33 Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, bado kukunja mikono kidogo upate kupumzika:
Un poco de sueño, un poco de dormitar, Un poco de cruzar las manos para descansar,
34 hivyo umaskini utakuja juu yako kama mnyangʼanyi, na kupungukiwa kutakujia kama mtu mwenye silaha.
Así vendrá tu miseria como un vagabundo, Y tu escasez como un hombre armado.