< Mithali 24 >
1 Usiwaonee wivu watu waovu, usitamani ushirika nao;
No tengas envidia de los malvados, ni desees su compañía,
2 kwa maana mioyo yao hupanga mambo ya jeuri, nayo midomo yao husema juu ya kuleta madhara.
porque ellos conspiran planes crueles y discuten entre ellos para causar tribulación.
3 Kwa hekima nyumba hujengwa, nayo kwa njia ya ufahamu huimarishwa
Una casa se construye con sabiduría. Su fundamento seguro es la inteligencia.
4 kwa njia ya maarifa vyumba vyake hujazwa vitu vya thamani na vya kupendeza.
Sus habitaciones están llenas de conocimiento, con todo tipo de hermosos y valiosos objetos.
5 Mtu mwenye hekima ana uwezo mkubwa, naye mtu mwenye maarifa huongeza nguvu,
Si tienes sabiduría, serás fuerte. Si tienes inteligencia, tu poder aumentará.
6 kwa kufanya vita unahitaji uongozi na kwa ushindi washauri wengi.
Porque con la guía correcta, podrás ir a la guerra, y serás victorioso si tienes muchos buenos consejeros.
7 Hekima i juu mno kwa mpumbavu, katika kusanyiko langoni hana lolote la kusema.
La sabiduría examina las mentes de los tontos. Ellos no tienen nada que aportar en las discusiones sobre los asuntos importantes.
8 Yeye apangaye mabaya atajulikana kama mtu wa hila.
Todo aquel que hace planes para hacer el mal, será considerado un problemático.
9 Mipango ya upumbavu ni dhambi, watu huchukizwa na mwenye dhihaka.
Los planes que hacen los tontos son de pecado. Todos aborrecen a los que se burlan de otros.
10 Ukikata tamaa wakati wa taabu, jinsi gani nguvu zako ni kidogo!
Si te rindes en el momento de la prueba, mostraras cuan débil eres.
11 Okoa wale wanaoongozwa kwenye kifo; wazuie wote wanaojikokota kuelekea machinjoni.
Rescata a los que son expulsados para ser ejecutados. Salva a los que desfallecen de camino a su muerte.
12 Kama mkisema, “Lakini hatukujua lolote kuhusu hili,” je, yule apimaye mioyo halitambui hili? Je, yule awalindaye maisha yenu halijui hili? Je, hatamlipa kila mtu kulingana na aliyotenda?
Si dices: “No sabíamos nada sobre esto”, ¿no crees que el Dios que juzga las motivaciones no se dará cuenta de lo que ocurre realmente? El que te mira desde arriba lo sabe todo, y le pagará a todos según sus actos.
13 Ule asali mwanangu, kwa kuwa ni nzuri; asali kutoka kwenye sega ni tamu kwa kuonja.
Hijo mío, comer miel te conviene; el panal de miel tiene un dulce sabor.
14 Ujue pia kwamba hekima ni tamu kwa nafsi yako, kama ukiipata, kuna matumaini kwako ya siku zijazo, nalo tumaini lako halitakatiliwa mbali.
Del mismo modo, debes saber que te conviene la sabiduría; y que sin la encuentras habrá un futuro para ti que no será frustrado.
15 Usivizie kama haramia afanyavyo ili kuyashambulia makao ya mwenye haki, wala usiyavamie makazi yake,
No seas como el criminal que espera para entrar por sorpresa en las casas de las buenas personas. No ataques el lugar donde viven.
16 Kwa maana ingawa mtu mwenye haki huanguka mara saba, huinuka tena, lakini waovu huangushwa chini na maafa.
Los que hacen el bien podrán caer siete veces, y aun así se levantaran; pero el desastre vendrá para derribar a los malvados.
17 Usitazame kwa kufurahia adui yako aangukapo; wakati ajikwaapo, usiruhusu moyo wako ushangilie.
No celebres cuando tu enemigo caiga. No te alegues cuando se tropiece,
18 Bwana asije akaona na kuchukia akaiondoa ghadhabu yake mbali naye.
porque puede que cuando el Señor lo note, se desagrade de ti y no lo castigue como lo había pensado.
19 Usikasirike kwa sababu ya watu wabaya wala usiwaonee wivu waovu,
No te enojes por causa de los malvados, ni sientas celos por los que hacen el mal,
20 kwa maana mtu mbaya hana tumaini la siku zijazo, nayo taa ya waovu itazimwa.
porque los malvados no tienen futuro. La lámpara de los malvados se apagará.
21 Mwanangu, mche Bwana na mfalme, wala usijiunge na waasi,
Hijo mío, honra al Señor y al rey, y no te juntes con los rebeldes,
22 kwa maana hao wawili watatuma maangamizi ya ghafula juu yao, naye ni nani ajuaye maafa wawezayo kuleta?
porque el desastre vendrá sobre ellos repentinamente. ¿Quién podrá saber cómo los castigarán el Señor y el rey?
23 Hii pia ni misemo ya wenye hekima: Kuonyesha upendeleo katika hukumu si vyema:
Estos son más dichos del sabio: Mostrar preferencias cuando emites un juicio no es bueno.
24 Yeyote amwambiaye mwenye hatia, “Wewe huna hatia,” Kabila zitamlaani na mataifa yatamkana.
Los que le dicen al culpable: “Eres inocente”, serán malditos por el pueblo y odiados por la nación,
25 Bali itakuwa vyema kwa wale watakaowatia hatiani wenye hatia, nazo baraka tele zitawajilia juu yao.
pero los que condenan al culpable serán estimados, y recibirán rica bendición.
26 Jawabu la uaminifu ni kama busu la midomoni.
Una respuesta honesta es como un beso en los labios.
27 Maliza kazi zako za nje, nawe uweke mashamba yako tayari, baada ya hayo, jenga nyumba yako.
Haz primero el trabajo que necesitas hacer afuera y prepárate para sembrar tus campos. Solo después de eso, comienza a construir tu casa.
28 Usishuhudie dhidi ya jirani yako bila sababu, au kutumia midomo yako kudanganya.
No seas testigo contra tu prójimo sin tener una buena razón, ni digas mentiras.
29 Usiseme, “Nitamtenda kama alivyonitenda mimi; nitamlipiza mtu yule kwa kile alichonitendea.”
No digas en tu pensamiento: “Voy a hacerle lo mismo que me hizo! ¡Haré que me pague por lo que ha hecho!”
30 Nilipita karibu na shamba la mvivu, karibu na shamba la mizabibu la mtu asiye na akili,
Mientras caminaba, pasé por el campo del hombre perezoso, y por el viñedo de un insensato.
31 miiba ilikuwa imeota kila mahali, ardhi ilikuwa imefunikwa na magugu, na ukuta wa mawe ulikuwa umebomoka.
Y estaba lleno de monte y espinas, el suelo estaba cubierto de hierba y la piedra angular se había caído.
32 Nikatafakari moyoni mwangu lile nililoliona, nami nikajifunza somo kutokana na niliyoyaona:
Y mientras veía, pensé y aprendí una lección:
33 Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, bado kukunja mikono kidogo upate kupumzika:
Puedes decir: “Solo dormiré un poco más, me recostaré apenas un rato, y cruzaré mis brazos para descansar un poco más”,
34 hivyo umaskini utakuja juu yako kama mnyangʼanyi, na kupungukiwa kutakujia kama mtu mwenye silaha.
pero la pobreza te atacará como un ladrón, y la miseria como un guerrero armado.