< Mithali 24 >
1 Usiwaonee wivu watu waovu, usitamani ushirika nao;
ne aemuleris viros malos nec desideres esse cum eis
2 kwa maana mioyo yao hupanga mambo ya jeuri, nayo midomo yao husema juu ya kuleta madhara.
quia rapinas meditatur mens eorum et fraudes labia eorum loquuntur
3 Kwa hekima nyumba hujengwa, nayo kwa njia ya ufahamu huimarishwa
sapientia aedificabitur domus et prudentia roborabitur
4 kwa njia ya maarifa vyumba vyake hujazwa vitu vya thamani na vya kupendeza.
in doctrina replebuntur cellaria universa substantia pretiosa et pulcherrima
5 Mtu mwenye hekima ana uwezo mkubwa, naye mtu mwenye maarifa huongeza nguvu,
vir sapiens et fortis est et vir doctus robustus et validus
6 kwa kufanya vita unahitaji uongozi na kwa ushindi washauri wengi.
quia cum dispositione initur bellum et erit salus ubi multa consilia sunt
7 Hekima i juu mno kwa mpumbavu, katika kusanyiko langoni hana lolote la kusema.
excelsa stulto sapientia in porta non aperiet os suum
8 Yeye apangaye mabaya atajulikana kama mtu wa hila.
qui cogitat malefacere stultus vocabitur
9 Mipango ya upumbavu ni dhambi, watu huchukizwa na mwenye dhihaka.
cogitatio stulti peccatum est et abominatio hominum detractor
10 Ukikata tamaa wakati wa taabu, jinsi gani nguvu zako ni kidogo!
si desperaveris lassus in die angustiae inminuetur fortitudo tua
11 Okoa wale wanaoongozwa kwenye kifo; wazuie wote wanaojikokota kuelekea machinjoni.
erue eos qui ducuntur ad mortem et qui trahuntur ad interitum liberare ne cesses
12 Kama mkisema, “Lakini hatukujua lolote kuhusu hili,” je, yule apimaye mioyo halitambui hili? Je, yule awalindaye maisha yenu halijui hili? Je, hatamlipa kila mtu kulingana na aliyotenda?
si dixeris vires non suppetunt qui inspector est cordis ipse intellegit et servatorem animae tuae nihil fallit reddetque homini iuxta opera sua
13 Ule asali mwanangu, kwa kuwa ni nzuri; asali kutoka kwenye sega ni tamu kwa kuonja.
comede fili mi mel quia bonum est et favum dulcissimum gutturi tuo
14 Ujue pia kwamba hekima ni tamu kwa nafsi yako, kama ukiipata, kuna matumaini kwako ya siku zijazo, nalo tumaini lako halitakatiliwa mbali.
sic et doctrina sapientiae animae tuae quam cum inveneris habebis in novissimis et spes tua non peribit
15 Usivizie kama haramia afanyavyo ili kuyashambulia makao ya mwenye haki, wala usiyavamie makazi yake,
ne insidieris et quaeras impietatem in domo iusti neque vastes requiem eius
16 Kwa maana ingawa mtu mwenye haki huanguka mara saba, huinuka tena, lakini waovu huangushwa chini na maafa.
septies enim cadet iustus et resurget impii autem corruent in malum
17 Usitazame kwa kufurahia adui yako aangukapo; wakati ajikwaapo, usiruhusu moyo wako ushangilie.
cum ceciderit inimicus tuus ne gaudeas et in ruina eius ne exultet cor tuum
18 Bwana asije akaona na kuchukia akaiondoa ghadhabu yake mbali naye.
ne forte videat Dominus et displiceat ei et auferat ab eo iram suam
19 Usikasirike kwa sababu ya watu wabaya wala usiwaonee wivu waovu,
ne contendas cum pessimis nec aemuleris impios
20 kwa maana mtu mbaya hana tumaini la siku zijazo, nayo taa ya waovu itazimwa.
quoniam non habent futurorum spem mali et lucerna impiorum extinguetur
21 Mwanangu, mche Bwana na mfalme, wala usijiunge na waasi,
time Dominum fili mi et regem et cum detractoribus non commiscearis
22 kwa maana hao wawili watatuma maangamizi ya ghafula juu yao, naye ni nani ajuaye maafa wawezayo kuleta?
quoniam repente consurget perditio eorum et ruinam utriusque quis novit
23 Hii pia ni misemo ya wenye hekima: Kuonyesha upendeleo katika hukumu si vyema:
haec quoque sapientibus cognoscere personam in iudicio non est bonum
24 Yeyote amwambiaye mwenye hatia, “Wewe huna hatia,” Kabila zitamlaani na mataifa yatamkana.
qui dicit impio iustus es maledicent ei populi et detestabuntur eum tribus
25 Bali itakuwa vyema kwa wale watakaowatia hatiani wenye hatia, nazo baraka tele zitawajilia juu yao.
qui arguunt laudabuntur et super ipsos veniet benedictio
26 Jawabu la uaminifu ni kama busu la midomoni.
labia deosculabitur qui recta verba respondet
27 Maliza kazi zako za nje, nawe uweke mashamba yako tayari, baada ya hayo, jenga nyumba yako.
praepara foris opus tuum et diligenter exerce agrum tuum ut postea aedifices domum tuam
28 Usishuhudie dhidi ya jirani yako bila sababu, au kutumia midomo yako kudanganya.
ne sis testis frustra contra proximum tuum nec lactes quemquam labiis tuis
29 Usiseme, “Nitamtenda kama alivyonitenda mimi; nitamlipiza mtu yule kwa kile alichonitendea.”
ne dicas quomodo fecit mihi sic faciam ei reddam unicuique secundum opus suum
30 Nilipita karibu na shamba la mvivu, karibu na shamba la mizabibu la mtu asiye na akili,
per agrum hominis pigri transivi et per vineam viri stulti
31 miiba ilikuwa imeota kila mahali, ardhi ilikuwa imefunikwa na magugu, na ukuta wa mawe ulikuwa umebomoka.
et ecce totum repleverant urticae operuerant superficiem eius spinae et maceria lapidum destructa erat
32 Nikatafakari moyoni mwangu lile nililoliona, nami nikajifunza somo kutokana na niliyoyaona:
quod cum vidissem posui in corde meo et exemplo didici disciplinam
33 Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, bado kukunja mikono kidogo upate kupumzika:
parum inquam dormies modicum dormitabis pauxillum manus conseres ut quiescas
34 hivyo umaskini utakuja juu yako kama mnyangʼanyi, na kupungukiwa kutakujia kama mtu mwenye silaha.
et veniet quasi cursor egestas tua et mendicitas quasi vir armatus