< Mithali 24 >
1 Usiwaonee wivu watu waovu, usitamani ushirika nao;
Ne porte pas envie aux hommes méchants, et ne désire pas d’être avec eux;
2 kwa maana mioyo yao hupanga mambo ya jeuri, nayo midomo yao husema juu ya kuleta madhara.
Parce que leur âme médite des rapines, et que leurs lèvres parlent fraudes.
3 Kwa hekima nyumba hujengwa, nayo kwa njia ya ufahamu huimarishwa
C’est par la sagesse que se bâtira une maison, et par la prudence qu’elle s’affermira.
4 kwa njia ya maarifa vyumba vyake hujazwa vitu vya thamani na vya kupendeza.
Par la science, les celliers se rempliront de toute sorte de biens précieux et très beaux.
5 Mtu mwenye hekima ana uwezo mkubwa, naye mtu mwenye maarifa huongeza nguvu,
L’homme sage est puissant, et l’homme instruit est robuste et vigoureux.
6 kwa kufanya vita unahitaji uongozi na kwa ushindi washauri wengi.
Parce que c’est avec réflexion que s’entreprend une guerre; et que le salut sera où il y a beaucoup de conseils.
7 Hekima i juu mno kwa mpumbavu, katika kusanyiko langoni hana lolote la kusema.
Bien élevée est pour l’insensé la sagesse à la porte de la ville, il n’ouvrira pas la bouche.
8 Yeye apangaye mabaya atajulikana kama mtu wa hila.
Celui qui pense à faire le mal sera appelé insensé.
9 Mipango ya upumbavu ni dhambi, watu huchukizwa na mwenye dhihaka.
La pensée de l’insensé est péché; et c’est l’abomination des hommes, que le médisant.
10 Ukikata tamaa wakati wa taabu, jinsi gani nguvu zako ni kidogo!
Si, fatigué au jour de l’angoisse, tu désespères, ta force sera diminuée.
11 Okoa wale wanaoongozwa kwenye kifo; wazuie wote wanaojikokota kuelekea machinjoni.
Arrache au péril ceux qui sont conduits à la mort, et, ceux que l’on traîne à la destruction, ne cesse pas de les délivrer.
12 Kama mkisema, “Lakini hatukujua lolote kuhusu hili,” je, yule apimaye mioyo halitambui hili? Je, yule awalindaye maisha yenu halijui hili? Je, hatamlipa kila mtu kulingana na aliyotenda?
Si tu dis: Les forces me manquent; celui qui observe le cœur le discerne lui-même, rien ne trompe le conservateur de ton âme; et il rendra à l’homme selon ses œuvres.
13 Ule asali mwanangu, kwa kuwa ni nzuri; asali kutoka kwenye sega ni tamu kwa kuonja.
Mange, mon fils, le miel, parce qu’il est bon, et le rayon doux à ton gosier.
14 Ujue pia kwamba hekima ni tamu kwa nafsi yako, kama ukiipata, kuna matumaini kwako ya siku zijazo, nalo tumaini lako halitakatiliwa mbali.
Telle est la doctrine de la sagesse à ton âme: quand tu l’auras trouvée, tu auras à tes derniers moments l’espérance et ton espérance ne périra pas.
15 Usivizie kama haramia afanyavyo ili kuyashambulia makao ya mwenye haki, wala usiyavamie makazi yake,
Ne dresse pas d’embûches, et ne cherche pas l’impiété dans la maison du juste, et ne détruis pas son repos.
16 Kwa maana ingawa mtu mwenye haki huanguka mara saba, huinuka tena, lakini waovu huangushwa chini na maafa.
Car le juste tombera sept fois et se relèvera; mais les impies seront abattus dans le malheur.
17 Usitazame kwa kufurahia adui yako aangukapo; wakati ajikwaapo, usiruhusu moyo wako ushangilie.
Lorsque ton ennemi sera tombé, ne Le réjouis pas: et qu’à sa ruine ton cœur n’exulte pas;
18 Bwana asije akaona na kuchukia akaiondoa ghadhabu yake mbali naye.
De peur que le Seigneur ne le voie, et que cela ne lui déplaise; et qu’il ne retire de lui sa colère.
19 Usikasirike kwa sababu ya watu wabaya wala usiwaonee wivu waovu,
Ne dispute pas avec les hommes très méchants; et ne porte pas envie aux impies;
20 kwa maana mtu mbaya hana tumaini la siku zijazo, nayo taa ya waovu itazimwa.
Parce qu’ils n’ont pas l’espérance des choses futures, les méchants, et que la lampe des impies s’éteindra.
21 Mwanangu, mche Bwana na mfalme, wala usijiunge na waasi,
Crains, mon fils, le Seigneur et le roi, et ne te lie pas avec les médisants;
22 kwa maana hao wawili watatuma maangamizi ya ghafula juu yao, naye ni nani ajuaye maafa wawezayo kuleta?
Parce que tout à coup s’élèvera leur perte, et la ruine de l’un et de l’autre, qui la connaît?
23 Hii pia ni misemo ya wenye hekima: Kuonyesha upendeleo katika hukumu si vyema:
Voici aussi pour les sages: Faire acception de la personne dans le jugement n’est pas bon.
24 Yeyote amwambiaye mwenye hatia, “Wewe huna hatia,” Kabila zitamlaani na mataifa yatamkana.
Quant à ceux qui disent à l’impie: Tu es juste; les peuples les maudiront et les tribus les détesteront.
25 Bali itakuwa vyema kwa wale watakaowatia hatiani wenye hatia, nazo baraka tele zitawajilia juu yao.
Ceux qui le reprennent seront loués; et sur eux viendra la bénédiction.
26 Jawabu la uaminifu ni kama busu la midomoni.
Il baisera les lèvres, celui qui répond des paroles droites.
27 Maliza kazi zako za nje, nawe uweke mashamba yako tayari, baada ya hayo, jenga nyumba yako.
Prépare au dehors ton œuvre, et avec soin cultive ton champ; afin qu’ensuite tu bâtisses ta maison.
28 Usishuhudie dhidi ya jirani yako bila sababu, au kutumia midomo yako kudanganya.
Ne sois pas témoin sans raison contre ton prochain; et ne séduis personne par tes lèvres.
29 Usiseme, “Nitamtenda kama alivyonitenda mimi; nitamlipiza mtu yule kwa kile alichonitendea.”
Ne dis pas: Comme il m’a fait, ainsi je lui ferai: je rendrai à chacun selon son œuvre.
30 Nilipita karibu na shamba la mvivu, karibu na shamba la mizabibu la mtu asiye na akili,
J’ai passé dans le champ du paresseux, et par la vigne de l’insensé:
31 miiba ilikuwa imeota kila mahali, ardhi ilikuwa imefunikwa na magugu, na ukuta wa mawe ulikuwa umebomoka.
Et voilà que tout était rempli d’orties; et que les épines en avaient couvert la surface, et que la muraille de pierres était détruite.
32 Nikatafakari moyoni mwangu lile nililoliona, nami nikajifunza somo kutokana na niliyoyaona:
Ce qu’ayant vu, je l’ai mis dans mon cœur, et par cet exemple je me suis instruit.
33 Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, bado kukunja mikono kidogo upate kupumzika:
Tu dormiras un peu, dis-je, tu sommeilleras modérément, tu mettras faiblement les mains l’une dans l’autre, afin que tu reposes:
34 hivyo umaskini utakuja juu yako kama mnyangʼanyi, na kupungukiwa kutakujia kama mtu mwenye silaha.
Et viendra à toi, comme un coureur, la détresse; et la mendicité, comme un homme armé.