< Mithali 24 >

1 Usiwaonee wivu watu waovu, usitamani ushirika nao;
Ne porte pas envie aux hommes méchants, et ne désire pas leur société!
2 kwa maana mioyo yao hupanga mambo ya jeuri, nayo midomo yao husema juu ya kuleta madhara.
Car leur cœur médite la ruine, et leurs lèvres ont un langage funeste.
3 Kwa hekima nyumba hujengwa, nayo kwa njia ya ufahamu huimarishwa
Par la sagesse une maison s'élève, et par l'intelligence elle se consolide;
4 kwa njia ya maarifa vyumba vyake hujazwa vitu vya thamani na vya kupendeza.
et par la science les chambres se remplissent de tous les biens de prix et d'agrément.
5 Mtu mwenye hekima ana uwezo mkubwa, naye mtu mwenye maarifa huongeza nguvu,
L'homme sage a de la force, et l'homme qui sait, gagne en vigueur.
6 kwa kufanya vita unahitaji uongozi na kwa ushindi washauri wengi.
Car tu feras la guerre ayant pris tes mesures, et c'est le nombre des conseillers qui donne la victoire.
7 Hekima i juu mno kwa mpumbavu, katika kusanyiko langoni hana lolote la kusema.
Pour l'insensé la sagesse est chose trop haute; aux Portes il n'ouvre pas la bouche.
8 Yeye apangaye mabaya atajulikana kama mtu wa hila.
Celui qui médite de faire du mal, reçoit le nom d'homme d'intrigue.
9 Mipango ya upumbavu ni dhambi, watu huchukizwa na mwenye dhihaka.
La pensée de la folie, c'est le péché; et le moqueur est l'abomination des hommes.
10 Ukikata tamaa wakati wa taabu, jinsi gani nguvu zako ni kidogo!
Si tu faiblis au jour de la détresse, tes forces s'affaibliront.
11 Okoa wale wanaoongozwa kwenye kifo; wazuie wote wanaojikokota kuelekea machinjoni.
Sauve ceux qu'on traîne à la mort; retiens ceux qui vont tomber sous les coups meurtriers!
12 Kama mkisema, “Lakini hatukujua lolote kuhusu hili,” je, yule apimaye mioyo halitambui hili? Je, yule awalindaye maisha yenu halijui hili? Je, hatamlipa kila mtu kulingana na aliyotenda?
Si tu dis: « Nous ne le connaissons point! » Celui qui pèse les cœurs, ne l'entendra-t-Il pas? et le Gardien de ton âme ne le saura-t-il pas? et ne rend-Il pas à chacun selon ses œuvres?
13 Ule asali mwanangu, kwa kuwa ni nzuri; asali kutoka kwenye sega ni tamu kwa kuonja.
Mon fils, mange le miel, car il est bon, et le rayon de miel, qui est doux à ton palais!
14 Ujue pia kwamba hekima ni tamu kwa nafsi yako, kama ukiipata, kuna matumaini kwako ya siku zijazo, nalo tumaini lako halitakatiliwa mbali.
Sache que telle sera la sagesse à ton âme. Si tu la trouves, il est un avenir; et ton espoir ne sera pas mis à néant.
15 Usivizie kama haramia afanyavyo ili kuyashambulia makao ya mwenye haki, wala usiyavamie makazi yake,
Impie, ne dresse point d'embûches à la demeure du juste, et ne dévaste point son gîte.
16 Kwa maana ingawa mtu mwenye haki huanguka mara saba, huinuka tena, lakini waovu huangushwa chini na maafa.
Car sept fois le juste tombe, et il se relève; mais les impies périssent dans le malheur.
17 Usitazame kwa kufurahia adui yako aangukapo; wakati ajikwaapo, usiruhusu moyo wako ushangilie.
Ne te réjouis pas de la chute de ton ennemi, et que ton cœur ne se délecte pas de sa ruine,
18 Bwana asije akaona na kuchukia akaiondoa ghadhabu yake mbali naye.
de peur que l'Éternel ne le voie, et n'en ait déplaisir, et qu'il ne détourne sa colère de lui.
19 Usikasirike kwa sababu ya watu wabaya wala usiwaonee wivu waovu,
Ne t'irrite point à la vue des méchants, et ne sois point jaloux des impies,
20 kwa maana mtu mbaya hana tumaini la siku zijazo, nayo taa ya waovu itazimwa.
car le méchant n'a point d'avenir, le flambeau des impies s'éteint.
21 Mwanangu, mche Bwana na mfalme, wala usijiunge na waasi,
Crains l'Éternel, mon fils, et le roi, et ne t'associe point aux novateurs!
22 kwa maana hao wawili watatuma maangamizi ya ghafula juu yao, naye ni nani ajuaye maafa wawezayo kuleta?
car leur ruine surgit tout-à-coup, et le temps du châtiment des uns et des autres, qui le sait?
23 Hii pia ni misemo ya wenye hekima: Kuonyesha upendeleo katika hukumu si vyema:
Encore paroles de sages. Etre partial, quand on juge, n'est pas bien.
24 Yeyote amwambiaye mwenye hatia, “Wewe huna hatia,” Kabila zitamlaani na mataifa yatamkana.
Quiconque dit au coupable: Tu es innocent! encourt la malédiction des peuples, et le courroux des nations.
25 Bali itakuwa vyema kwa wale watakaowatia hatiani wenye hatia, nazo baraka tele zitawajilia juu yao.
Mais ceux qui osent punir, s'en trouvent bien, et obtiennent le bonheur comme bénédiction.
26 Jawabu la uaminifu ni kama busu la midomoni.
Il donne un baiser sur les lèvres, celui qui répond pertinemment.
27 Maliza kazi zako za nje, nawe uweke mashamba yako tayari, baada ya hayo, jenga nyumba yako.
Soigne au dehors tes affaires, et mets en bon état ton champ; alors tu peux bâtir ta maison.
28 Usishuhudie dhidi ya jirani yako bila sababu, au kutumia midomo yako kudanganya.
Ne témoigne pas à la légère contre ton prochain; et de tes lèvres voudrais-tu tromper?
29 Usiseme, “Nitamtenda kama alivyonitenda mimi; nitamlipiza mtu yule kwa kile alichonitendea.”
Ne dis pas: Ce qu'il m'a fait, je le lui ferai, je rendrai à chacun selon ses œuvres.
30 Nilipita karibu na shamba la mvivu, karibu na shamba la mizabibu la mtu asiye na akili,
Près du champ du paresseux je passais, et près de la vigne de l'homme privé de sens;
31 miiba ilikuwa imeota kila mahali, ardhi ilikuwa imefunikwa na magugu, na ukuta wa mawe ulikuwa umebomoka.
et voici, le chardon y poussait partout, et des orties en couvraient le sol, et son mur de pierres s'était écroulé.
32 Nikatafakari moyoni mwangu lile nililoliona, nami nikajifunza somo kutokana na niliyoyaona:
Et je regardai, et fis attention; je vis, et en tirai une leçon:
33 Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, bado kukunja mikono kidogo upate kupumzika:
« Un peu dormir, un peu sommeiller, un peu croiser les bras en étant couché! »
34 hivyo umaskini utakuja juu yako kama mnyangʼanyi, na kupungukiwa kutakujia kama mtu mwenye silaha.
Ainsi, la pauvreté fondra sur toi, comme un larron, et l'indigence, comme un homme portant le bouclier.

< Mithali 24 >