< Mithali 24 >
1 Usiwaonee wivu watu waovu, usitamani ushirika nao;
Mon fils, ne rivalise point avec les méchants, et ne désire pas être avec eux.
2 kwa maana mioyo yao hupanga mambo ya jeuri, nayo midomo yao husema juu ya kuleta madhara.
Car leur cœur médite des fraudes, et leurs lèvres disent des paroles affligeantes.
3 Kwa hekima nyumba hujengwa, nayo kwa njia ya ufahamu huimarishwa
La sagesse bâtit sa maison; l'intelligence la dirige;
4 kwa njia ya maarifa vyumba vyake hujazwa vitu vya thamani na vya kupendeza.
avec la doctrine on remplit les celliers de tout ce qu'il y a de riche, de précieux et de bon.
5 Mtu mwenye hekima ana uwezo mkubwa, naye mtu mwenye maarifa huongeza nguvu,
Mieux vaut le sage que le fort, et un homme de bon sens que de vastes domaines.
6 kwa kufanya vita unahitaji uongozi na kwa ushindi washauri wengi.
Avec l'art de gouverner, on conduit la guerre; avec un cœur résolu, on trouve le salut.
7 Hekima i juu mno kwa mpumbavu, katika kusanyiko langoni hana lolote la kusema.
La sagesse et les bonnes pensées sont à la porte des sages; les sages ne se détournent pas de la parole du Seigneur.
8 Yeye apangaye mabaya atajulikana kama mtu wa hila.
Mais ils sont appréciés dans les conseils. la mort surprend les imprudents.
9 Mipango ya upumbavu ni dhambi, watu huchukizwa na mwenye dhihaka.
L'insensé meurt dans son péché. L'impureté est dans l'homme de pestilence;
10 Ukikata tamaa wakati wa taabu, jinsi gani nguvu zako ni kidogo!
il sera déshonoré au jour fatal, au jour de la tribulation, jusqu'à ce qu'il soit renversé.
11 Okoa wale wanaoongozwa kwenye kifo; wazuie wote wanaojikokota kuelekea machinjoni.
Délivre ceux que l'on conduit à la mort; rachète ceux qu'on va faire mourir, et n'y épargne pas tes soins.
12 Kama mkisema, “Lakini hatukujua lolote kuhusu hili,” je, yule apimaye mioyo halitambui hili? Je, yule awalindaye maisha yenu halijui hili? Je, hatamlipa kila mtu kulingana na aliyotenda?
Si tu dis: Je ne connais pas cet homme; sache que Dieu connaît tous les cœurs; Celui qui a donné le souffle à tous, sait toutes choses, et Il rétribue chacun selon ses œuvres.
13 Ule asali mwanangu, kwa kuwa ni nzuri; asali kutoka kwenye sega ni tamu kwa kuonja.
Mon fils, mange du miel; car le rayon de miel est bon; que ton gosier en goûte la douceur.
14 Ujue pia kwamba hekima ni tamu kwa nafsi yako, kama ukiipata, kuna matumaini kwako ya siku zijazo, nalo tumaini lako halitakatiliwa mbali.
C'est ainsi que tu feras comprendre la sagesse à ton âme; car si tu l'acquiers, ta fin sera bonne, et l'espérance ne t'abandonnera point.
15 Usivizie kama haramia afanyavyo ili kuyashambulia makao ya mwenye haki, wala usiyavamie makazi yake,
Ne conduis pas l'impie dans les pâturages des justes; ne te laisse pas séduire par l'appât de la gourmandise.
16 Kwa maana ingawa mtu mwenye haki huanguka mara saba, huinuka tena, lakini waovu huangushwa chini na maafa.
Car le juste tombera sept fois, et il se relèvera; mais les impies seront sans force dans le malheur.
17 Usitazame kwa kufurahia adui yako aangukapo; wakati ajikwaapo, usiruhusu moyo wako ushangilie.
Si ton ennemi tombe, ne te moque pas de lui, et ne t'enorgueillis pas de sa ruine.
18 Bwana asije akaona na kuchukia akaiondoa ghadhabu yake mbali naye.
Car le Seigneur te verrait, et Il ne t'aurait point pour agréable, et Il détournerait Sa colère de ton ennemi.
19 Usikasirike kwa sababu ya watu wabaya wala usiwaonee wivu waovu,
Ne prends point part aux joies des méchants; ne porte point envie aux pécheurs.
20 kwa maana mtu mbaya hana tumaini la siku zijazo, nayo taa ya waovu itazimwa.
Car les pervers n'auront point de postérité, et la langue des impies s'éteindra.
21 Mwanangu, mche Bwana na mfalme, wala usijiunge na waasi,
Crains Dieu et le roi, mon fils, et ne leur désobéis jamais.
22 kwa maana hao wawili watatuma maangamizi ya ghafula juu yao, naye ni nani ajuaye maafa wawezayo kuleta?
Car ils punissent inopinément les impies; et qui peut prévoir quelle sera leur vengeance?
23 Hii pia ni misemo ya wenye hekima: Kuonyesha upendeleo katika hukumu si vyema:
Qu'aucun mensonge se soit dit par la langue du roi; que nulle fausseté ne sorte de sa langue. Voici ce que je dis, à vous sages, pour que vous le sachiez: Il n'est pas bien, en justice, d'avoir égard au rang.
24 Yeyote amwambiaye mwenye hatia, “Wewe huna hatia,” Kabila zitamlaani na mataifa yatamkana.
La langue du roi n'est point de chair, c'est un glaive; et celui qui lui sera livré, sera brisé; Ceux qui disent de l'impie: C'est un juste, seront maudits du peuple et odieux aux nations.
25 Bali itakuwa vyema kwa wale watakaowatia hatiani wenye hatia, nazo baraka tele zitawajilia juu yao.
car si sa colère est excitée, elle détruit les hommes avec leurs nerfs; Mais ceux qui le réprimandent paraîtront meilleurs, et la bénédiction viendra sur eux.
26 Jawabu la uaminifu ni kama busu la midomoni.
elle dévore leurs os, elles les consume comme la flamme, au point que les aiglons n'y trouveraient pas de quoi se repaître. On baisera les livres qui diront de bonnes paroles.
27 Maliza kazi zako za nje, nawe uweke mashamba yako tayari, baada ya hayo, jenga nyumba yako.
Prépare ton ouvrage au dehors; arrive à ton champ, tout préparé; marche sur mes traces, et tu réédifieras ta maison.
28 Usishuhudie dhidi ya jirani yako bila sababu, au kutumia midomo yako kudanganya.
Ne porte pas contre un concitoyen de faux témoignage, et n'ouvre pas les lèvres contre lui.
29 Usiseme, “Nitamtenda kama alivyonitenda mimi; nitamlipiza mtu yule kwa kile alichonitendea.”
Ne dis pas: Comme il m'a traité, je le traiterai; je me vengerai du tort qu'il m'a fait.
30 Nilipita karibu na shamba la mvivu, karibu na shamba la mizabibu la mtu asiye na akili,
L'insensé est comme un champ; l'homme qui manque d'esprit est comme un vignoble.
31 miiba ilikuwa imeota kila mahali, ardhi ilikuwa imefunikwa na magugu, na ukuta wa mawe ulikuwa umebomoka.
Si tu le délaisses, il sera stérile et tout couvert de mauvaises herbes; il dépérit, et sa clôture de pierres s'écroule.
32 Nikatafakari moyoni mwangu lile nililoliona, nami nikajifunza somo kutokana na niliyoyaona:
À la fin, j'ai réfléchi et j'ai songé à chercher la vraie doctrine.
33 Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, bado kukunja mikono kidogo upate kupumzika:
Je sommeille un moment; un moment je m'endors, et je me tiens un moment les bras croisés.
34 hivyo umaskini utakuja juu yako kama mnyangʼanyi, na kupungukiwa kutakujia kama mtu mwenye silaha.
Si tu fais cela, l'indigence t'arrivera à grands pas, et le besoin fondra sur toi comme un agile coursier.