< Mithali 24 >

1 Usiwaonee wivu watu waovu, usitamani ushirika nao;
Ne porte pas envie aux hommes méchants, et ne désire pas d’être avec eux.
2 kwa maana mioyo yao hupanga mambo ya jeuri, nayo midomo yao husema juu ya kuleta madhara.
Car leur cœur médite la violence, et leurs lèvres ne profèrent que le malheur. Avantages pratiques de la sagesse.
3 Kwa hekima nyumba hujengwa, nayo kwa njia ya ufahamu huimarishwa
C’est par la sagesse qu’une maison s’élève, et par l’intelligence qu’elle s’affermit.
4 kwa njia ya maarifa vyumba vyake hujazwa vitu vya thamani na vya kupendeza.
C’est par la science que l’intérieur se remplit, de tous les biens précieux et agréables.
5 Mtu mwenye hekima ana uwezo mkubwa, naye mtu mwenye maarifa huongeza nguvu,
Un homme sage est plein de force, et celui qui a de la science montre une grande puissance.
6 kwa kufanya vita unahitaji uongozi na kwa ushindi washauri wengi.
Car avec la prudence tu conduiras la guerre, et le salut est dans le grand nombre des conseillers.
7 Hekima i juu mno kwa mpumbavu, katika kusanyiko langoni hana lolote la kusema.
La sagesse est trop haute pour l’insensé; il n’ouvre pas la bouche à la porte de la ville. L’intrigant.
8 Yeye apangaye mabaya atajulikana kama mtu wa hila.
Celui qui pense à faire le mal s’appelle un artisan d’intrigues. L’insensé.
9 Mipango ya upumbavu ni dhambi, watu huchukizwa na mwenye dhihaka.
Le dessein de l’insensé, c’est le péché, et le railleur est en abomination parmi les hommes. L’indolent.
10 Ukikata tamaa wakati wa taabu, jinsi gani nguvu zako ni kidogo!
Si tu te montres faible au jour de la détresse, ta force n’est que faiblesse. Porter secours aux malheureux opprimés.
11 Okoa wale wanaoongozwa kwenye kifo; wazuie wote wanaojikokota kuelekea machinjoni.
Délivre ceux qu’on traîne à la mort; ceux qui vont en chancelant au massacre, sauve-les!
12 Kama mkisema, “Lakini hatukujua lolote kuhusu hili,” je, yule apimaye mioyo halitambui hili? Je, yule awalindaye maisha yenu halijui hili? Je, hatamlipa kila mtu kulingana na aliyotenda?
Si tu dis: « Mais! Nous ne le savions pas! » Celui qui pèse les cœurs ne le voit-il pas? Celui qui veille sur ton âme ne le connaît-il pas, et ne rendra-t-il pas à chacun selon ses œuvres?
13 Ule asali mwanangu, kwa kuwa ni nzuri; asali kutoka kwenye sega ni tamu kwa kuonja.
Mon fils, mange du miel, car il est bon; un rayon de miel est doux à ton palais.
14 Ujue pia kwamba hekima ni tamu kwa nafsi yako, kama ukiipata, kuna matumaini kwako ya siku zijazo, nalo tumaini lako halitakatiliwa mbali.
Sache que la sagesse est la même chose pour ton âme; si tu l’acquiers, il est un avenir, et ton espérance ne sera pas frustrée.
15 Usivizie kama haramia afanyavyo ili kuyashambulia makao ya mwenye haki, wala usiyavamie makazi yake,
Ne tends pas, ô méchant, des embûches à la demeure du juste, et ne dévaste pas le lieu où il repose;
16 Kwa maana ingawa mtu mwenye haki huanguka mara saba, huinuka tena, lakini waovu huangushwa chini na maafa.
car sept fois le juste tombe, et il se relève, mais les méchants sont précipités dans le malheur.
17 Usitazame kwa kufurahia adui yako aangukapo; wakati ajikwaapo, usiruhusu moyo wako ushangilie.
Si ton ennemi tombe, ne te réjouis pas, et que ton cœur ne se réjouisse pas de sa ruine,
18 Bwana asije akaona na kuchukia akaiondoa ghadhabu yake mbali naye.
de peur que Yahweh ne le voie, que cela soit mauvais à ses yeux, et qu’il ne détourne de lui sa colère.
19 Usikasirike kwa sababu ya watu wabaya wala usiwaonee wivu waovu,
Ne t’irrite pas à cause des méchants, ne porte pas envie aux pervers,
20 kwa maana mtu mbaya hana tumaini la siku zijazo, nayo taa ya waovu itazimwa.
car il n’y a point d’avenir pour celui qui fait le mal, et la lampe des méchants s’éteindra.
21 Mwanangu, mche Bwana na mfalme, wala usijiunge na waasi,
Mon fils, crains Yahweh et le roi; ne te mêle pas avec les hommes remuants;
22 kwa maana hao wawili watatuma maangamizi ya ghafula juu yao, naye ni nani ajuaye maafa wawezayo kuleta?
car soudain surgira leur malheur, et qui connaît la ruine des uns et des autres?
23 Hii pia ni misemo ya wenye hekima: Kuonyesha upendeleo katika hukumu si vyema:
Ce qui suit vient encore des sages: Il n’est pas bon, dans les jugements, d’avoir égard aux personnes.
24 Yeyote amwambiaye mwenye hatia, “Wewe huna hatia,” Kabila zitamlaani na mataifa yatamkana.
Celui qui dit aux méchants: « Tu es juste », les peuples le maudissent, les nations l’exècrent.
25 Bali itakuwa vyema kwa wale watakaowatia hatiani wenye hatia, nazo baraka tele zitawajilia juu yao.
Mais ceux qui le corrigent sont applaudis, sur eux viennent la bénédiction et le bonheur.
26 Jawabu la uaminifu ni kama busu la midomoni.
Il baise sur les lèvres celui qui répond des paroles justes.
27 Maliza kazi zako za nje, nawe uweke mashamba yako tayari, baada ya hayo, jenga nyumba yako.
Règle ton travail au dehors, applique-le à ton champ, puis tu bâtiras ta maison.
28 Usishuhudie dhidi ya jirani yako bila sababu, au kutumia midomo yako kudanganya.
Ne témoigne pas à la légère contre ton prochain: voudrais-tu tromper par tes lèvres?
29 Usiseme, “Nitamtenda kama alivyonitenda mimi; nitamlipiza mtu yule kwa kile alichonitendea.”
Ne dis pas: « Comme il m’a fait, je lui ferai; je rendrai à cet homme selon ses œuvres. »
30 Nilipita karibu na shamba la mvivu, karibu na shamba la mizabibu la mtu asiye na akili,
J’ai passé près du champ d’un paresseux, et près de la vigne d’un insensé.
31 miiba ilikuwa imeota kila mahali, ardhi ilikuwa imefunikwa na magugu, na ukuta wa mawe ulikuwa umebomoka.
Et voici, … les épines y croissaient partout, les ronces en couvraient la surface, et le mur de pierres était écroulé.
32 Nikatafakari moyoni mwangu lile nililoliona, nami nikajifunza somo kutokana na niliyoyaona:
J’ai regardé, et j’ai appliqué mon cœur, j’ai considéré et j’ai tiré cette leçon:
33 Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, bado kukunja mikono kidogo upate kupumzika:
« Un peu de sommeil, un peu d’assoupissement, un peu croiser les mains pour dormir,
34 hivyo umaskini utakuja juu yako kama mnyangʼanyi, na kupungukiwa kutakujia kama mtu mwenye silaha.
et ta pauvreté viendra comme un rôdeur, et ton indigence comme un homme armé. »

< Mithali 24 >