< Mithali 24 >

1 Usiwaonee wivu watu waovu, usitamani ushirika nao;
Ne soyez pas envieux des hommes mauvais, ni le désir d'être avec eux;
2 kwa maana mioyo yao hupanga mambo ya jeuri, nayo midomo yao husema juu ya kuleta madhara.
pour la violence du complot de leurs cœurs et leurs lèvres parlent de méchanceté.
3 Kwa hekima nyumba hujengwa, nayo kwa njia ya ufahamu huimarishwa
C'est par la sagesse que l'on construit une maison; par l'entendement, il est établi;
4 kwa njia ya maarifa vyumba vyake hujazwa vitu vya thamani na vya kupendeza.
par connaissance les chambres sont remplies avec tous les trésors rares et magnifiques.
5 Mtu mwenye hekima ana uwezo mkubwa, naye mtu mwenye maarifa huongeza nguvu,
Un homme sage a un grand pouvoir. Un homme bien informé accroît sa force,
6 kwa kufanya vita unahitaji uongozi na kwa ushindi washauri wengi.
car c'est par des conseils avisés que tu fais la guerre, et la victoire est dans de nombreux conseillers.
7 Hekima i juu mno kwa mpumbavu, katika kusanyiko langoni hana lolote la kusema.
La sagesse est trop élevée pour un fou. Il n'ouvre pas sa bouche dans la porte.
8 Yeye apangaye mabaya atajulikana kama mtu wa hila.
Celui qui complote pour faire le mal sera appelé un magouilleur.
9 Mipango ya upumbavu ni dhambi, watu huchukizwa na mwenye dhihaka.
Les projets de la folie sont des péchés. Le moqueur est détesté par les hommes.
10 Ukikata tamaa wakati wa taabu, jinsi gani nguvu zako ni kidogo!
Si vous chancelez au moment de la détresse, votre force est faible.
11 Okoa wale wanaoongozwa kwenye kifo; wazuie wote wanaojikokota kuelekea machinjoni.
Sauvez ceux qui sont conduits à la mort! En effet, retenez ceux qui titubent vers le massacre!
12 Kama mkisema, “Lakini hatukujua lolote kuhusu hili,” je, yule apimaye mioyo halitambui hili? Je, yule awalindaye maisha yenu halijui hili? Je, hatamlipa kila mtu kulingana na aliyotenda?
Si vous dites: « Voici, nous ne savions pas cela, » Celui qui pèse les cœurs ne le considère-t-il pas? Celui qui garde ton âme, ne le sait-il pas? Ne doit-il pas rendre à chacun selon son travail?
13 Ule asali mwanangu, kwa kuwa ni nzuri; asali kutoka kwenye sega ni tamu kwa kuonja.
Mon fils, mange du miel, car il est bon, les excréments du rayon de miel, qui sont doux à votre goût;
14 Ujue pia kwamba hekima ni tamu kwa nafsi yako, kama ukiipata, kuna matumaini kwako ya siku zijazo, nalo tumaini lako halitakatiliwa mbali.
Ainsi tu connaîtras la sagesse pour ton âme. Si vous l'avez trouvé, il y aura une récompense: Votre espoir ne sera pas coupé.
15 Usivizie kama haramia afanyavyo ili kuyashambulia makao ya mwenye haki, wala usiyavamie makazi yake,
Ne fais pas d'embuscades, méchant, contre la demeure des justes. Ne détruisez pas son lieu de repos;
16 Kwa maana ingawa mtu mwenye haki huanguka mara saba, huinuka tena, lakini waovu huangushwa chini na maafa.
car le juste tombe sept fois et se relève, mais les méchants sont renversés par la calamité.
17 Usitazame kwa kufurahia adui yako aangukapo; wakati ajikwaapo, usiruhusu moyo wako ushangilie.
Ne te réjouis pas quand ton ennemi tombe. Ne laissez pas votre cœur se réjouir quand il sera renversé,
18 Bwana asije akaona na kuchukia akaiondoa ghadhabu yake mbali naye.
de peur que Yahvé ne le voie et que cela ne lui déplaise, et il détourne de lui sa colère.
19 Usikasirike kwa sababu ya watu wabaya wala usiwaonee wivu waovu,
Ne vous inquiétez pas à cause des méchants, ne soyez pas envieux des méchants;
20 kwa maana mtu mbaya hana tumaini la siku zijazo, nayo taa ya waovu itazimwa.
car il n'y aura pas de récompense pour l'homme mauvais. La lampe des méchants sera éteinte.
21 Mwanangu, mche Bwana na mfalme, wala usijiunge na waasi,
Mon fils, crains Yahvé et le roi. Ne vous joignez pas à ceux qui sont rebelles,
22 kwa maana hao wawili watatuma maangamizi ya ghafula juu yao, naye ni nani ajuaye maafa wawezayo kuleta?
car leur calamité se lève soudainement. Qui sait quelle destruction peut venir de ces deux-là?
23 Hii pia ni misemo ya wenye hekima: Kuonyesha upendeleo katika hukumu si vyema:
Ce sont là des paroles de sages: Faire preuve de partialité dans le jugement n'est pas bon.
24 Yeyote amwambiaye mwenye hatia, “Wewe huna hatia,” Kabila zitamlaani na mataifa yatamkana.
Celui qui dit au méchant: « Tu es juste, » les peuples le maudiront, et les nations l'abhorreront -
25 Bali itakuwa vyema kwa wale watakaowatia hatiani wenye hatia, nazo baraka tele zitawajilia juu yao.
mais il ira bien avec ceux qui condamnent les coupables, et une riche bénédiction viendra sur eux.
26 Jawabu la uaminifu ni kama busu la midomoni.
Une réponse honnête est comme un baiser sur les lèvres.
27 Maliza kazi zako za nje, nawe uweke mashamba yako tayari, baada ya hayo, jenga nyumba yako.
Préparez votre travail à l'extérieur, et préparez vos champs. Ensuite, construisez votre maison.
28 Usishuhudie dhidi ya jirani yako bila sababu, au kutumia midomo yako kudanganya.
Ne sois pas un témoin contre ton prochain sans raison. Ne trompez pas avec vos lèvres.
29 Usiseme, “Nitamtenda kama alivyonitenda mimi; nitamlipiza mtu yule kwa kile alichonitendea.”
Ne dites pas: « Je lui ferai ce qu'il m'a fait »; Je rendrai à l'homme ce qu'il a fait. »
30 Nilipita karibu na shamba la mvivu, karibu na shamba la mizabibu la mtu asiye na akili,
Je suis passé par le champ du paresseux, par la vigne de l'homme dépourvu d'intelligence.
31 miiba ilikuwa imeota kila mahali, ardhi ilikuwa imefunikwa na magugu, na ukuta wa mawe ulikuwa umebomoka.
Voici, elle était couverte d'épines. Sa surface était couverte d'orties, et son mur de pierre a été démoli.
32 Nikatafakari moyoni mwangu lile nililoliona, nami nikajifunza somo kutokana na niliyoyaona:
Alors j'ai vu, et j'ai bien réfléchi. J'ai vu, et reçu des instructions:
33 Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, bado kukunja mikono kidogo upate kupumzika:
un peu de sommeil, un peu d'assoupissement, un petit pliage des mains pour dormir,
34 hivyo umaskini utakuja juu yako kama mnyangʼanyi, na kupungukiwa kutakujia kama mtu mwenye silaha.
alors ta pauvreté viendra comme un voleur et votre volonté en tant qu'homme armé.

< Mithali 24 >