< Mithali 24 >
1 Usiwaonee wivu watu waovu, usitamani ushirika nao;
Älä kadehdi pahoja ihmisiä äläkä halua heidän seuraansa.
2 kwa maana mioyo yao hupanga mambo ya jeuri, nayo midomo yao husema juu ya kuleta madhara.
Sillä heidän mielensä miettii väkivaltaa, ja turmiota haastavat heidän huulensa.
3 Kwa hekima nyumba hujengwa, nayo kwa njia ya ufahamu huimarishwa
Viisaudella talo rakennetaan ja ymmärryksellä vahvaksi varustetaan.
4 kwa njia ya maarifa vyumba vyake hujazwa vitu vya thamani na vya kupendeza.
Taidolla täytetään kammiot, kaikkea kallista ja ihanaa tavaraa täyteen.
5 Mtu mwenye hekima ana uwezo mkubwa, naye mtu mwenye maarifa huongeza nguvu,
Viisas mies on väkevä, ja taidon mies on voipa voimaltansa.
6 kwa kufanya vita unahitaji uongozi na kwa ushindi washauri wengi.
Neuvokkuudella näet on sinun käytävä sotaa, ja neuvonantajain runsaus tuo menestyksen.
7 Hekima i juu mno kwa mpumbavu, katika kusanyiko langoni hana lolote la kusema.
Kovin on korkea hullulle viisaus, ei hän suutansa avaa portissa.
8 Yeye apangaye mabaya atajulikana kama mtu wa hila.
Jolla on pahanteko mielessä, sitä juonittelijaksi sanotaan.
9 Mipango ya upumbavu ni dhambi, watu huchukizwa na mwenye dhihaka.
Synti on hulluuden työ, ja pilkkaaja on ihmisille kauhistus.
10 Ukikata tamaa wakati wa taabu, jinsi gani nguvu zako ni kidogo!
Jos olet ollut veltto, joutuu ahtaana aikana voimasi ahtaalle.
11 Okoa wale wanaoongozwa kwenye kifo; wazuie wote wanaojikokota kuelekea machinjoni.
Pelasta ne, joita kuolemaan viedään, pysäytä ne, jotka surmapaikalle hoippuvat.
12 Kama mkisema, “Lakini hatukujua lolote kuhusu hili,” je, yule apimaye mioyo halitambui hili? Je, yule awalindaye maisha yenu halijui hili? Je, hatamlipa kila mtu kulingana na aliyotenda?
Jos sanot: "Katso, emme tienneet siitä", niin ymmärtäähän asian sydänten tutkija; sinun sielusi vartioitsija sen tietää, ja hän kostaa ihmiselle hänen tekojensa mukaan.
13 Ule asali mwanangu, kwa kuwa ni nzuri; asali kutoka kwenye sega ni tamu kwa kuonja.
Syö hunajaa, poikani, sillä se on hyvää, ja mesi on makeaa suussasi.
14 Ujue pia kwamba hekima ni tamu kwa nafsi yako, kama ukiipata, kuna matumaini kwako ya siku zijazo, nalo tumaini lako halitakatiliwa mbali.
Samankaltaiseksi tunne viisaus sielullesi; jos sen löydät, on sinulla tulevaisuus, ja toivosi ei mene turhaan.
15 Usivizie kama haramia afanyavyo ili kuyashambulia makao ya mwenye haki, wala usiyavamie makazi yake,
Älä väijy, jumalaton, vanhurskaan majaa, älä hävitä hänen leposijaansa.
16 Kwa maana ingawa mtu mwenye haki huanguka mara saba, huinuka tena, lakini waovu huangushwa chini na maafa.
Sillä seitsemästi vanhurskas lankeaa ja nousee jälleen, mutta jumalattomat suistuvat onnettomuuteen.
17 Usitazame kwa kufurahia adui yako aangukapo; wakati ajikwaapo, usiruhusu moyo wako ushangilie.
Älä iloitse vihamiehesi langetessa, älköön sydämesi riemuitko hänen suistuessaan kumoon,
18 Bwana asije akaona na kuchukia akaiondoa ghadhabu yake mbali naye.
ettei Herra, kun sen näkee, sitä pahana pitäisi, ja kääntäisi vihaansa pois hänestä.
19 Usikasirike kwa sababu ya watu wabaya wala usiwaonee wivu waovu,
Älä vihastu pahantekijäin tähden, älä kadehdi jumalattomia.
20 kwa maana mtu mbaya hana tumaini la siku zijazo, nayo taa ya waovu itazimwa.
Sillä ei ole pahalla tulevaisuutta; jumalattomien lamppu sammuu.
21 Mwanangu, mche Bwana na mfalme, wala usijiunge na waasi,
Pelkää, poikani, Herraa ja kuningasta, älä sekaannu kapinallisten seuraan.
22 kwa maana hao wawili watatuma maangamizi ya ghafula juu yao, naye ni nani ajuaye maafa wawezayo kuleta?
Sillä yhtäkkiä tulee heille onnettomuus, tuomio-kuka tietää milloin-toisille niinkuin toisillekin.
23 Hii pia ni misemo ya wenye hekima: Kuonyesha upendeleo katika hukumu si vyema:
Nämäkin ovat viisaitten sanoja. Ei ole hyvä tuomitessa henkilöön katsoa.
24 Yeyote amwambiaye mwenye hatia, “Wewe huna hatia,” Kabila zitamlaani na mataifa yatamkana.
Joka sanoo syylliselle: "Sinä olet syytön", sitä kansat kiroavat, kansakunnat sadattelevat.
25 Bali itakuwa vyema kwa wale watakaowatia hatiani wenye hatia, nazo baraka tele zitawajilia juu yao.
Mutta jotka oikein tuomitsevat, niiden käy hyvin, ja heille tulee onnen siunaus.
26 Jawabu la uaminifu ni kama busu la midomoni.
Se huulille suutelee, joka oikean vastauksen antaa.
27 Maliza kazi zako za nje, nawe uweke mashamba yako tayari, baada ya hayo, jenga nyumba yako.
Toimita tehtäväsi ulkona ja tee valmista pellollasi; sitten perusta itsellesi perhe.
28 Usishuhudie dhidi ya jirani yako bila sababu, au kutumia midomo yako kudanganya.
Älä ole syyttä todistajana lähimmäistäsi vastaan, vai petätkö sinä huulillasi?
29 Usiseme, “Nitamtenda kama alivyonitenda mimi; nitamlipiza mtu yule kwa kile alichonitendea.”
Älä sano: "Niinkuin hän teki minulle, niin teen minä hänelle, minä kostan miehelle hänen tekojensa mukaan".
30 Nilipita karibu na shamba la mvivu, karibu na shamba la mizabibu la mtu asiye na akili,
Minä kuljin laiskurin pellon ohitse, mielettömän miehen viinitarhan vieritse.
31 miiba ilikuwa imeota kila mahali, ardhi ilikuwa imefunikwa na magugu, na ukuta wa mawe ulikuwa umebomoka.
Ja katso: se kasvoi yltänsä polttiaisia; sen pinta oli nokkosten peitossa ja sen kiviaita luhistunut.
32 Nikatafakari moyoni mwangu lile nililoliona, nami nikajifunza somo kutokana na niliyoyaona:
Minä katselin ja painoin mieleeni, havaitsin ja otin opikseni:
33 Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, bado kukunja mikono kidogo upate kupumzika:
Nuku vielä vähän, torku vähän, makaa vähän ristissä käsin,
34 hivyo umaskini utakuja juu yako kama mnyangʼanyi, na kupungukiwa kutakujia kama mtu mwenye silaha.
niin köyhyys käy päällesi niinkuin rosvo ja puute niinkuin asestettu mies.