< Mithali 24 >

1 Usiwaonee wivu watu waovu, usitamani ushirika nao;
Sue thou not yuele men, desire thou not to be with hem.
2 kwa maana mioyo yao hupanga mambo ya jeuri, nayo midomo yao husema juu ya kuleta madhara.
For the soule of hem bithenkith raueyns, and her lippis speken fraudis.
3 Kwa hekima nyumba hujengwa, nayo kwa njia ya ufahamu huimarishwa
An hous schal be bildid bi wisdom, and schal be maad strong bi prudence.
4 kwa njia ya maarifa vyumba vyake hujazwa vitu vya thamani na vya kupendeza.
Celeris schulen be fillid in teching, al riches preciouse and ful fair.
5 Mtu mwenye hekima ana uwezo mkubwa, naye mtu mwenye maarifa huongeza nguvu,
A wijs man is strong, and a lerned man is stalworth and miyti.
6 kwa kufanya vita unahitaji uongozi na kwa ushindi washauri wengi.
For whi batel is bigunnun with ordenaunce, and helthe schal be, where many counsels ben.
7 Hekima i juu mno kwa mpumbavu, katika kusanyiko langoni hana lolote la kusema.
Wisdom is hiy to a fool; in the yate he schal not opene his mouth.
8 Yeye apangaye mabaya atajulikana kama mtu wa hila.
He that thenkith to do yuels, schal be clepid a fool.
9 Mipango ya upumbavu ni dhambi, watu huchukizwa na mwenye dhihaka.
The thouyte of a fool is synne; and a bacbitere is abhomynacioun of men.
10 Ukikata tamaa wakati wa taabu, jinsi gani nguvu zako ni kidogo!
If thou that hast slide, dispeirist in the dai of angwisch, thi strengthe schal be maad lesse.
11 Okoa wale wanaoongozwa kwenye kifo; wazuie wote wanaojikokota kuelekea machinjoni.
Delyuere thou hem, that ben led to deth; and ceesse thou not to delyuere hem, that ben drawun to deth.
12 Kama mkisema, “Lakini hatukujua lolote kuhusu hili,” je, yule apimaye mioyo halitambui hili? Je, yule awalindaye maisha yenu halijui hili? Je, hatamlipa kila mtu kulingana na aliyotenda?
If thou seist, Strengthis suffisen not; he that is biholdere of the herte, vndirstondith, and no thing disseyueth the kepere of thi soule, and he schal yelde to a man bi hise werkis.
13 Ule asali mwanangu, kwa kuwa ni nzuri; asali kutoka kwenye sega ni tamu kwa kuonja.
Mi sone, ete thou hony, for it is good; and an honycomb ful swete to thi throte.
14 Ujue pia kwamba hekima ni tamu kwa nafsi yako, kama ukiipata, kuna matumaini kwako ya siku zijazo, nalo tumaini lako halitakatiliwa mbali.
`So and the techyng of wisdom is good to thi soule; and whanne thou hast founde it, thou schalt haue hope in the laste thingis, and thin hope schal not perische.
15 Usivizie kama haramia afanyavyo ili kuyashambulia makao ya mwenye haki, wala usiyavamie makazi yake,
Aspie thou not, and seke not wickidnesse in the hous of a iust man, nether waste thou his reste.
16 Kwa maana ingawa mtu mwenye haki huanguka mara saba, huinuka tena, lakini waovu huangushwa chini na maafa.
For a iust man schal falle seuene sithis in the dai, and schal rise ayen; but wickid men schulen falle in to yuele.
17 Usitazame kwa kufurahia adui yako aangukapo; wakati ajikwaapo, usiruhusu moyo wako ushangilie.
Whanne thin enemye fallith, haue thou not ioye; and thin herte haue not ful out ioiyng in his fal;
18 Bwana asije akaona na kuchukia akaiondoa ghadhabu yake mbali naye.
lest perauenture the Lord se, and it displese hym, and he take awei his ire fro hym.
19 Usikasirike kwa sababu ya watu wabaya wala usiwaonee wivu waovu,
Stryue thou not with `the worste men, nether sue thou wickid men.
20 kwa maana mtu mbaya hana tumaini la siku zijazo, nayo taa ya waovu itazimwa.
For whi yuele men han not hope of thingis to comynge, and the lanterne of wickid men schal be quenchid.
21 Mwanangu, mche Bwana na mfalme, wala usijiunge na waasi,
My sone, drede thou God, and the kyng; and be thou not medlid with bacbiteris.
22 kwa maana hao wawili watatuma maangamizi ya ghafula juu yao, naye ni nani ajuaye maafa wawezayo kuleta?
For her perdicioun schal rise togidere sudenli, and who knowith the fal of euer either?
23 Hii pia ni misemo ya wenye hekima: Kuonyesha upendeleo katika hukumu si vyema:
Also these thingis that suen ben to wise men. It is not good to knowe a persoone in doom.
24 Yeyote amwambiaye mwenye hatia, “Wewe huna hatia,” Kabila zitamlaani na mataifa yatamkana.
Puplis schulen curse hem, that seien to a wickid man, Thou art iust; and lynagis schulen holde hem abhomynable.
25 Bali itakuwa vyema kwa wale watakaowatia hatiani wenye hatia, nazo baraka tele zitawajilia juu yao.
Thei that repreuen iustli synners, schulen be preisid; and blessing schal come on hem.
26 Jawabu la uaminifu ni kama busu la midomoni.
He that answerith riytful wordis, schal kisse lippis.
27 Maliza kazi zako za nje, nawe uweke mashamba yako tayari, baada ya hayo, jenga nyumba yako.
Make redi thi werk with outforth, and worche thi feelde dilygentli, that thou bilde thin hous aftirward.
28 Usishuhudie dhidi ya jirani yako bila sababu, au kutumia midomo yako kudanganya.
Be thou not a witnesse with out resonable cause ayens thi neiybore; nether flatere thou ony man with thi lippis.
29 Usiseme, “Nitamtenda kama alivyonitenda mimi; nitamlipiza mtu yule kwa kile alichonitendea.”
Seie thou not, As he dide to me, so Y schal do to him, and Y schal yelde to ech man aftir his werk.
30 Nilipita karibu na shamba la mvivu, karibu na shamba la mizabibu la mtu asiye na akili,
I passide bi the feeld of a slow man, and bi the vyner of a fonned man; and, lo!
31 miiba ilikuwa imeota kila mahali, ardhi ilikuwa imefunikwa na magugu, na ukuta wa mawe ulikuwa umebomoka.
nettlis hadden fillid al, thornes hadden hilid the hiyere part therof, and the wal of stoonys with out morter was distried.
32 Nikatafakari moyoni mwangu lile nililoliona, nami nikajifunza somo kutokana na niliyoyaona:
And whanne Y hadde seyn this thing, Y settide in myn herte, and bi ensaumple Y lernyde techyng.
33 Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, bado kukunja mikono kidogo upate kupumzika:
Hou longe slepist thou, slow man? whanne schalt thou ryse fro sleep? Sotheli thou schalt slepe a litil, thou schalt nappe a litil, thou schalt ioyne togidere the hondis a litil, to take reste;
34 hivyo umaskini utakuja juu yako kama mnyangʼanyi, na kupungukiwa kutakujia kama mtu mwenye silaha.
and thi nedynesse as a currour schal come to thee, and thi beggerie as an armed man.

< Mithali 24 >