< Mithali 24 >
1 Usiwaonee wivu watu waovu, usitamani ushirika nao;
Be not you envious against evil men, neither desire to be with them.
2 kwa maana mioyo yao hupanga mambo ya jeuri, nayo midomo yao husema juu ya kuleta madhara.
For their heart studies destruction, and their lips talk of mischief.
3 Kwa hekima nyumba hujengwa, nayo kwa njia ya ufahamu huimarishwa
Through wisdom is an house built; and by understanding it is established:
4 kwa njia ya maarifa vyumba vyake hujazwa vitu vya thamani na vya kupendeza.
And by knowledge shall the chambers be filled with all precious and pleasant riches.
5 Mtu mwenye hekima ana uwezo mkubwa, naye mtu mwenye maarifa huongeza nguvu,
A wise man is strong; yea, a man of knowledge increases strength.
6 kwa kufanya vita unahitaji uongozi na kwa ushindi washauri wengi.
For by wise counsel you shall make your war: and in multitude of counsellors there is safety.
7 Hekima i juu mno kwa mpumbavu, katika kusanyiko langoni hana lolote la kusema.
Wisdom is too high for a fool: he opens not his mouth in the gate.
8 Yeye apangaye mabaya atajulikana kama mtu wa hila.
He that devises to do evil shall be called a mischievous person.
9 Mipango ya upumbavu ni dhambi, watu huchukizwa na mwenye dhihaka.
The thought of foolishness is sin: and the scorner is an abomination to men.
10 Ukikata tamaa wakati wa taabu, jinsi gani nguvu zako ni kidogo!
If you faint in the day of adversity, your strength is small.
11 Okoa wale wanaoongozwa kwenye kifo; wazuie wote wanaojikokota kuelekea machinjoni.
If you forbear to deliver them that are drawn unto death, and those that are ready to be slain;
12 Kama mkisema, “Lakini hatukujua lolote kuhusu hili,” je, yule apimaye mioyo halitambui hili? Je, yule awalindaye maisha yenu halijui hili? Je, hatamlipa kila mtu kulingana na aliyotenda?
If you say, Behold, we knew it not; does not he that ponders the heart consider it? and he that keeps your soul, does not he know it? and shall not he render to every man according to his works?
13 Ule asali mwanangu, kwa kuwa ni nzuri; asali kutoka kwenye sega ni tamu kwa kuonja.
My son, eat you honey, because it is good; and the honeycomb, which is sweet to your taste:
14 Ujue pia kwamba hekima ni tamu kwa nafsi yako, kama ukiipata, kuna matumaini kwako ya siku zijazo, nalo tumaini lako halitakatiliwa mbali.
So shall the knowledge of wisdom be unto your soul: when you have found it, then there shall be a reward, and your expectation shall not be cut off.
15 Usivizie kama haramia afanyavyo ili kuyashambulia makao ya mwenye haki, wala usiyavamie makazi yake,
Lay not wait, O wicked man, against the dwelling of the righteous; spoil not his resting place:
16 Kwa maana ingawa mtu mwenye haki huanguka mara saba, huinuka tena, lakini waovu huangushwa chini na maafa.
For a just man falls seven times, and rises up again: but the wicked shall fall into mischief.
17 Usitazame kwa kufurahia adui yako aangukapo; wakati ajikwaapo, usiruhusu moyo wako ushangilie.
Rejoice not when your enemy falls, and let not your heart be glad when he stumbles:
18 Bwana asije akaona na kuchukia akaiondoa ghadhabu yake mbali naye.
Lest the LORD see it, and it displease him, and he turn away his wrath from him.
19 Usikasirike kwa sababu ya watu wabaya wala usiwaonee wivu waovu,
Fret not yourself because of evil men, neither be you envious at the wicked:
20 kwa maana mtu mbaya hana tumaini la siku zijazo, nayo taa ya waovu itazimwa.
For there shall be no reward to the evil man; the candle of the wicked shall be put out.
21 Mwanangu, mche Bwana na mfalme, wala usijiunge na waasi,
My son, fear you the LORD and the king: and meddle not with them that are given to change:
22 kwa maana hao wawili watatuma maangamizi ya ghafula juu yao, naye ni nani ajuaye maafa wawezayo kuleta?
For their calamity shall rise suddenly; and who knows the ruin of them both?
23 Hii pia ni misemo ya wenye hekima: Kuonyesha upendeleo katika hukumu si vyema:
These things also belong to the wise. It is not good to have respect of persons in judgment.
24 Yeyote amwambiaye mwenye hatia, “Wewe huna hatia,” Kabila zitamlaani na mataifa yatamkana.
He that says unto the wicked, You are righteous; him shall the people curse, nations shall detest him:
25 Bali itakuwa vyema kwa wale watakaowatia hatiani wenye hatia, nazo baraka tele zitawajilia juu yao.
But to them that rebuke him shall be delight, and a good blessing shall come upon them.
26 Jawabu la uaminifu ni kama busu la midomoni.
Every man shall kiss his lips that gives a right answer.
27 Maliza kazi zako za nje, nawe uweke mashamba yako tayari, baada ya hayo, jenga nyumba yako.
Prepare your work without, and make it fit for yourself in the field; and afterwards build your house.
28 Usishuhudie dhidi ya jirani yako bila sababu, au kutumia midomo yako kudanganya.
Be not a witness against your neighbour without cause; and deceive not with your lips.
29 Usiseme, “Nitamtenda kama alivyonitenda mimi; nitamlipiza mtu yule kwa kile alichonitendea.”
Say not, I will do so to him as he has done to me: I will render to the man according to his work.
30 Nilipita karibu na shamba la mvivu, karibu na shamba la mizabibu la mtu asiye na akili,
I went by the field of the slothful, and by the vineyard of the man void of understanding;
31 miiba ilikuwa imeota kila mahali, ardhi ilikuwa imefunikwa na magugu, na ukuta wa mawe ulikuwa umebomoka.
And, lo, it was all grown over with thorns, and nettles had covered the face thereof, and the stone wall thereof was broken down.
32 Nikatafakari moyoni mwangu lile nililoliona, nami nikajifunza somo kutokana na niliyoyaona:
Then I saw, and considered it well: I looked upon it, and received instruction.
33 Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, bado kukunja mikono kidogo upate kupumzika:
Yet a little sleep, a little slumber, a little folding of the hands to sleep:
34 hivyo umaskini utakuja juu yako kama mnyangʼanyi, na kupungukiwa kutakujia kama mtu mwenye silaha.
So shall your poverty come as one that travels; and your lack as an armed man.