< Mithali 24 >

1 Usiwaonee wivu watu waovu, usitamani ushirika nao;
Misund ej onde Folk, hav ikke lyst til at være med dem;
2 kwa maana mioyo yao hupanga mambo ya jeuri, nayo midomo yao husema juu ya kuleta madhara.
thi deres Hjerte pønser paa Vold, deres Læbers Ord volder Men.
3 Kwa hekima nyumba hujengwa, nayo kwa njia ya ufahamu huimarishwa
Ved Visdom bygges et Hus, ved Indsigt holdes det oppe,
4 kwa njia ya maarifa vyumba vyake hujazwa vitu vya thamani na vya kupendeza.
ved Kundskab fyldes Kamrene med alskens kosteligt, herligt Gods.
5 Mtu mwenye hekima ana uwezo mkubwa, naye mtu mwenye maarifa huongeza nguvu,
Vismand er større end Kæmpe, kyndig Mand mer end Kraftkarl.
6 kwa kufanya vita unahitaji uongozi na kwa ushindi washauri wengi.
Thi Krig skal du føre efter modent Overlæg, vel staar det til, hvor mange giver Raad.
7 Hekima i juu mno kwa mpumbavu, katika kusanyiko langoni hana lolote la kusema.
Visdom er Daaren for høj, han aabner ej Munden i Porten.
8 Yeye apangaye mabaya atajulikana kama mtu wa hila.
Den, der har ondt i Sinde, kaldes en rænkefuld Mand.
9 Mipango ya upumbavu ni dhambi, watu huchukizwa na mwenye dhihaka.
Hvad en Daare har for, er Synd, en Spotter er Folk en Gru.
10 Ukikata tamaa wakati wa taabu, jinsi gani nguvu zako ni kidogo!
Taber du Modet paa Trængslens Dag, da er din Kraft kun ringe.
11 Okoa wale wanaoongozwa kwenye kifo; wazuie wote wanaojikokota kuelekea machinjoni.
Frels dem, der slæbes til Døden, red dem, der vakler hen for at dræbes.
12 Kama mkisema, “Lakini hatukujua lolote kuhusu hili,” je, yule apimaye mioyo halitambui hili? Je, yule awalindaye maisha yenu halijui hili? Je, hatamlipa kila mtu kulingana na aliyotenda?
Siger du: »Se, jeg vidste det ikke« — mon ej han, der vejer Hjerter, kan skønne? Han, der tager Vare paa din Sjæl, han ved det, han gengælder Mennesker, hvad de har gjort.
13 Ule asali mwanangu, kwa kuwa ni nzuri; asali kutoka kwenye sega ni tamu kwa kuonja.
Spis Honning, min Søn, det er godt, og Kubens Saft er sød for din Gane;
14 Ujue pia kwamba hekima ni tamu kwa nafsi yako, kama ukiipata, kuna matumaini kwako ya siku zijazo, nalo tumaini lako halitakatiliwa mbali.
vid, at saa er og Visdom for Sjælen! Naar du finder den, har du en Fremtid, dit Haab bliver ikke til intet.
15 Usivizie kama haramia afanyavyo ili kuyashambulia makao ya mwenye haki, wala usiyavamie makazi yake,
Lur ej paa den retfærdiges Bolig, du gudløse, ødelæg ikke hans Hjem;
16 Kwa maana ingawa mtu mwenye haki huanguka mara saba, huinuka tena, lakini waovu huangushwa chini na maafa.
thi syv Gange falder en retfærdig og staar op, men gudløse styrter i Fordærv.
17 Usitazame kwa kufurahia adui yako aangukapo; wakati ajikwaapo, usiruhusu moyo wako ushangilie.
Falder din Fjende, saa glæd dig ikke, snubler han, juble dit Hjerte ikke,
18 Bwana asije akaona na kuchukia akaiondoa ghadhabu yake mbali naye.
at ikke HERREN skal se det med Mishag og vende sin Vrede fra ham.
19 Usikasirike kwa sababu ya watu wabaya wala usiwaonee wivu waovu,
Græm dig ej over Ugerningsmænd, misund ikke de gudløse;
20 kwa maana mtu mbaya hana tumaini la siku zijazo, nayo taa ya waovu itazimwa.
thi den onde har ingen Fremtid, gudløses Lampe gaar ud.
21 Mwanangu, mche Bwana na mfalme, wala usijiunge na waasi,
Frygt HERREN og Kongen, min Søn, indlad dig ikke med Folk, som gør Oprør;
22 kwa maana hao wawili watatuma maangamizi ya ghafula juu yao, naye ni nani ajuaye maafa wawezayo kuleta?
thi brat kommer Ulykke fra dem, uventet Fordærv fra begge.
23 Hii pia ni misemo ya wenye hekima: Kuonyesha upendeleo katika hukumu si vyema:
Ogsaa følgende Ordsprog er af vise Mænd. Partiskhed i Retten er ilde.
24 Yeyote amwambiaye mwenye hatia, “Wewe huna hatia,” Kabila zitamlaani na mataifa yatamkana.
Mod den, som kender en skyldig fri, er Folkeslags Banden, Folkefærds Vrede;
25 Bali itakuwa vyema kwa wale watakaowatia hatiani wenye hatia, nazo baraka tele zitawajilia juu yao.
men dem, der dømmer med Ret, gaar det vel, dem kommer Lykkens Velsignelse over.
26 Jawabu la uaminifu ni kama busu la midomoni.
Et Kys paa Læberne giver den, som kommer med ærligt Svar.
27 Maliza kazi zako za nje, nawe uweke mashamba yako tayari, baada ya hayo, jenga nyumba yako.
Fuldfør din Gerning udendørs, gør dig færdig ude paa Marken og byg dig siden et Hus!
28 Usishuhudie dhidi ya jirani yako bila sababu, au kutumia midomo yako kudanganya.
Vidn ikke falsk mod din Næste, vær ikke letsindig med dine Læber;
29 Usiseme, “Nitamtenda kama alivyonitenda mimi; nitamlipiza mtu yule kwa kile alichonitendea.”
sig ikke: »Jeg gør mod ham, som han gjorde mod mig, jeg gengælder hver hans Gerning.«
30 Nilipita karibu na shamba la mvivu, karibu na shamba la mizabibu la mtu asiye na akili,
Jeg kom forbi en lad Mands Mark og et uforstandigt Menneskes Vingaard;
31 miiba ilikuwa imeota kila mahali, ardhi ilikuwa imefunikwa na magugu, na ukuta wa mawe ulikuwa umebomoka.
se, den var overgroet af Tidsler, ganske skjult af Nælder; Stendiget om den laa nedbrudt.
32 Nikatafakari moyoni mwangu lile nililoliona, nami nikajifunza somo kutokana na niliyoyaona:
Jeg skued og skrev mig det bag Øre, jeg saa og tog Lære deraf:
33 Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, bado kukunja mikono kidogo upate kupumzika:
Lidt Søvn endnu, lidt Blund, lidt Hvile med samlagte Hænder:
34 hivyo umaskini utakuja juu yako kama mnyangʼanyi, na kupungukiwa kutakujia kama mtu mwenye silaha.
Som en Stimand kommer da Fattigdom over dig, Trang som en skjoldvæbnet Mand.

< Mithali 24 >