< Mithali 23 >

1 Uketipo kula chakula na mtawala, angalia vyema kile kilicho mbele yako,
治める人と共に座して食事するとき、あなたの前にあるものを、よくわきまえ、
2 na utie kisu kooni mwako kama ukiwa mlafi.
あなたがもし食をたしなむ者であるならば、あなたののどに刀をあてよ。
3 Usitamani vyakula vyake vitamu kwa kuwa chakula hicho ni cha hila.
そのごちそうをむさぼり食べてはならない、これは人を欺く食物だからである。
4 Usijitaabishe ili kuupata utajiri, uwe na hekima kuonyesha kujizuia.
富を得ようと苦労してはならない、かしこく思いとどまるがよい。
5 Kufumba na kufumbua utajiri hutoweka, huwa kama umepata mabawa ghafula, ukaruka na kutoweka angani kama tai.
あなたの目をそれにとめると、それはない、富はたちまち自ら翼を生じて、わしのように天に飛び去るからだ。
6 Usile chakula cha mtu mchoyo, usitamani vyakula vyake vitamu,
物惜しみする人のパンを食べてはならない、そのごちそうをむさぼり願ってはならない。
7 kwa maana yeye ni aina ya mtu ambaye kila mara anafikiri juu ya gharama. Anakuambia, “Kula na kunywa,” lakini moyo wake hauko pamoja nawe.
彼は心のうちで勘定する人のように、「食え、飲め」とあなたに言うけれども、その心はあなたに真実ではない。
8 Utatapika kile kidogo ulichokula, nawe utakuwa umepoteza bure maneno yako ya kumsifu.
あなたはついにその食べた物を吐き出すようになり、あなたのねんごろな言葉もむだになる。
9 Usizungumze na mpumbavu, kwa maana atadhihaki hekima ya maneno yako.
愚かな者の耳に語ってはならない、彼はあなたの言葉が示す知恵をいやしめるからだ。
10 Usisogeze jiwe la mpaka wa zamani wala kunyemelea kwenye mashamba ya yatima,
古い地境を移してはならない、みなしごの畑を侵してはならない。
11 kwa kuwa Mtetezi wao ni mwenye nguvu, atalichukua shauri lao dhidi yako.
彼らのあがない主は強くいらせられ、あなたに逆らって彼らの訴えを弁護されるからだ。
12 Elekeza moyo wako kwenye mafundisho na masikio yako kwenye maneno ya maarifa.
あなたの心を教訓に用い、あなたの耳を知識の言葉に傾けよ。
13 Usimnyime mtoto adhabu, ukimwadhibu kwa fimbo, hatakufa.
子を懲らすことを、さし控えてはならない、むちで彼を打っても死ぬことはない。
14 Mwadhibu kwa fimbo na kuiokoa nafsi yake kutoka mautini. (Sheol h7585)
もし、むちで彼を打つならば、その命を陰府から救うことができる。 (Sheol h7585)
15 Mwanangu, kama moyo wako una hekima, basi moyo wangu utafurahi,
わが子よ、もしあなたの心が賢くあれば、わたしの心もまた喜び、
16 utu wangu wa ndani utafurahi, wakati midomo yako itakapozungumza lililo sawa.
もしあなたのくちびるが正しい事を言うならば、わたしの心も喜ぶ。
17 Usiuruhusu moyo wako kuwaonea wivu wenye dhambi, bali kila mara uwe na bidii katika kumcha Bwana.
心に罪びとをうらやんではならない、ただ、ひねもす主を恐れよ。
18 Hakika kuna tumaini la baadaye kwa ajili yako, nalo tarajio lako halitakatiliwa mbali.
かならず後のよい報いがあって、あなたの望みは、すたらない。
19 Sikiliza, mwanangu na uwe na hekima, weka moyo wako kwenye njia iliyo sawa.
わが子よ、よく聞いて、知恵を得よ、かつ、あなたの心を道に向けよ。
20 Usiwe miongoni mwa wanywao mvinyo, au wale walao nyama kwa pupa,
酒にふけり、肉をたしなむ者と交わってはならない。
21 kwa maana walevi na walafi huwa maskini, nako kusinzia huwavika matambara.
酒にふける者と、肉をたしなむ者とは貧しくなり、眠りをむさぼる者は、ぼろを身にまとうようになる。
22 Msikilize baba yako, aliyekuzaa, wala usimdharau mama yako atakapokuwa mzee.
あなたを生んだ父のいうことを聞き、年老いた母を軽んじてはならない。
23 Nunua kweli wala usiiuze, pata hekima, adabu na ufahamu.
真理を買え、これを売ってはならない、知恵と教訓と悟りをも買え。
24 Baba wa mwenye haki ana furaha kubwa, naye aliye na mwana mwenye hekima humfurahia.
正しい人の父は大いによろこび、知恵ある子を生む者は子のために楽しむ。
25 Baba yako na mama yako na wafurahi, mama aliyekuzaa na ashangilie!
あなたの父母を楽しませ、あなたを産んだ母を喜ばせよ。
26 Mwanangu, nipe moyo wako, macho yako na yafuate njia zangu,
わが子よ、あなたの心をわたしに与え、あなたの目をわたしの道に注げ。
27 kwa maana kahaba ni shimo refu na mwanamke mpotovu ni kisima chembamba.
遊女は深い穴のごとく、みだらな女は狭い井戸のようだ。
28 Kama mnyangʼanyi, hungojea akivizia, naye huzidisha wasio waaminifu miongoni mwa wanaume.
彼女は盗びとのように人をうかがい、かつ世の人のうちに、不信実な者を多くする。
29 Ni nani mwenye ole? Ni nani mwenye huzuni? Ni nani mwenye ugomvi? Ni nani mwenye malalamiko? Ni nani aliye na majeraha yasiyo na sababu? Ni nani mwenye macho mekundu?
災ある者はだれか、憂いある者はだれか、争いをする者はだれか、煩いある者はだれか、ゆえなく傷をうける者はだれか、赤い目をしている者はだれか。
30 Ni hao wakaao sana kwenye mvinyo, hao waendao kuonja mabakuli ya mvinyo uliochanganywa.
酒に夜をふかす者、行って、混ぜ合わせた酒を味わう者である。
31 Usiukodolee macho mvinyo wakati ukiwa mwekundu, wakati unapometameta kwenye bilauri, wakati ushukapo taratibu!
酒はあかく、杯の中にあわだち、なめらかにくだる、あなたはこれを見てはならない。
32 Mwishowe huuma kama nyoka na kutia sumu yake kama nyoka mwenye sumu.
これはついに、へびのようにかみ、まむしのように刺す。
33 Macho yako yataona mambo mageni na moyo wako kuwazia mambo yaliyopotoka.
あなたの目は怪しいものを見、あなたの心は偽りを言う。
34 Utakuwa kama alalaye katikati ya bahari, alalaye juu ya kamba ya merikebu.
あなたは海の中に寝ている人のように、帆柱の上に寝ている人のようになる。
35 Utasema, “Wamenipiga lakini sikuumia! Wamenichapa, lakini sisikii! Nitaamka lini ili nikanywe tena?”
あなたは言う、「人がわたしを撃ったが、わたしは痛くはなかった。わたしを、たたいたが、わたしは何も覚えはない。いつわたしはさめるのか、また酒を求めよう」と。

< Mithali 23 >