< Mithali 23 >

1 Uketipo kula chakula na mtawala, angalia vyema kile kilicho mbele yako,
幾時你與首長坐席,應記著,在你面前的是誰。
2 na utie kisu kooni mwako kama ukiwa mlafi.
你若過於貪食,應在咽喉上,放上一把刀。
3 Usitamani vyakula vyake vitamu kwa kuwa chakula hicho ni cha hila.
休要羨慕他的珍饈,因那是騙人的食品。
4 Usijitaabishe ili kuupata utajiri, uwe na hekima kuonyesha kujizuia.
不要辛苦企求致富,反應放棄這種企圖。
5 Kufumba na kufumbua utajiri hutoweka, huwa kama umepata mabawa ghafula, ukaruka na kutoweka angani kama tai.
你向之一注目,即不再存在了:它會生出翅膀,如鷹向天飛去。
6 Usile chakula cha mtu mchoyo, usitamani vyakula vyake vitamu,
不要與虎視眈眈的人進食,也不要羨慕他的山珍海味,
7 kwa maana yeye ni aina ya mtu ambaye kila mara anafikiri juu ya gharama. Anakuambia, “Kula na kunywa,” lakini moyo wake hauko pamoja nawe.
因為他原是只顧自己的人,他口頭雖對你說「請吃請喝! 」但他的心中並不與你友善;
8 Utatapika kile kidogo ulichokula, nawe utakuwa umepoteza bure maneno yako ya kumsifu.
你吃下的那口食物,還得吐出;你婉轉悅耳的言辭,盡屬枉費。
9 Usizungumze na mpumbavu, kwa maana atadhihaki hekima ya maneno yako.
不要與愚人交耳接談,因他必輕視你的高見。
10 Usisogeze jiwe la mpaka wa zamani wala kunyemelea kwenye mashamba ya yatima,
不要移動孀婦的地界,不要侵佔孤兒的田地;
11 kwa kuwa Mtetezi wao ni mwenye nguvu, atalichukua shauri lao dhidi yako.
因為他們的辯護者是大能的,他必為他們的案件與你爭辯。
12 Elekeza moyo wako kwenye mafundisho na masikio yako kwenye maneno ya maarifa.
你應專心接受教訓,傾耳細聽益智之言。
13 Usimnyime mtoto adhabu, ukimwadhibu kwa fimbo, hatakufa.
對孩童不可忽略懲戒;用棍打他,他不致死去。
14 Mwadhibu kwa fimbo na kuiokoa nafsi yake kutoka mautini. (Sheol h7585)
你用棍杖打他,是救他的靈魂免下陰府。 (Sheol h7585)
15 Mwanangu, kama moyo wako una hekima, basi moyo wangu utafurahi,
我兒,你若心懷智慧,我也誠心喜樂;
16 utu wangu wa ndani utafurahi, wakati midomo yako itakapozungumza lililo sawa.
你的唇舌若談吐正義的事,我的五衷也必會踴躍歡欣。
17 Usiuruhusu moyo wako kuwaonea wivu wenye dhambi, bali kila mara uwe na bidii katika kumcha Bwana.
心裏不要羨慕罪人,卻要日日敬畏上主;
18 Hakika kuna tumaini la baadaye kwa ajili yako, nalo tarajio lako halitakatiliwa mbali.
這樣你的將來必然順利,你的希望絕不落空。
19 Sikiliza, mwanangu na uwe na hekima, weka moyo wako kwenye njia iliyo sawa.
我兒,你要聽話,作個明智人;且要引領你的心走上正道。
20 Usiwe miongoni mwa wanywao mvinyo, au wale walao nyama kwa pupa,
貪嗜酒肉的人,不可與之來往;
21 kwa maana walevi na walafi huwa maskini, nako kusinzia huwavika matambara.
因為嗜酒貪食的人,必陷於窮困;貪懶好睡的人,必衣著襤褸。
22 Msikilize baba yako, aliyekuzaa, wala usimdharau mama yako atakapokuwa mzee.
對生養你的父親,應當聽從;對你年邁的母親,不可輕視。
23 Nunua kweli wala usiiuze, pata hekima, adabu na ufahamu.
應獲取真理,不可出賣,還有智慧、訓誨和見識。
24 Baba wa mwenye haki ana furaha kubwa, naye aliye na mwana mwenye hekima humfurahia.
義人的父親,必欣然喜樂;生育慧子的,必為此歡騰。
25 Baba yako na mama yako na wafurahi, mama aliyekuzaa na ashangilie!
應使你的父親因你而喜悅,應使你的生母因你而快樂。
26 Mwanangu, nipe moyo wako, macho yako na yafuate njia zangu,
我兒,將你的心交給我,注目於我的道路:
27 kwa maana kahaba ni shimo refu na mwanamke mpotovu ni kisima chembamba.
妓女是一個深坑,淫婦是一個陷阱;
28 Kama mnyangʼanyi, hungojea akivizia, naye huzidisha wasio waaminifu miongoni mwa wanaume.
她潛伏著,實如強盜,使人世間,增添奸夫。
29 Ni nani mwenye ole? Ni nani mwenye huzuni? Ni nani mwenye ugomvi? Ni nani mwenye malalamiko? Ni nani aliye na majeraha yasiyo na sababu? Ni nani mwenye macho mekundu?
是誰將哀鳴,是誰將悲嘆﹖是誰將爭吵,是誰將抱怨﹖是誰將無故受傷,是誰將雙目赤紅﹖
30 Ni hao wakaao sana kwenye mvinyo, hao waendao kuonja mabakuli ya mvinyo uliochanganywa.
是那流連於醉鄉,去搜求醇酒的人。
31 Usiukodolee macho mvinyo wakati ukiwa mwekundu, wakati unapometameta kwenye bilauri, wakati ushukapo taratibu!
你不要注視酒色怎樣紅,在杯中怎樣閃耀,飲下去怎樣痛快!
32 Mwishowe huuma kama nyoka na kutia sumu yake kama nyoka mwenye sumu.
終究它要咬人如蛇,刺人如虺。
33 Macho yako yataona mambo mageni na moyo wako kuwazia mambo yaliyopotoka.
那時,你的眼要見到奇景,你的心要吐出狂語。
34 Utakuwa kama alalaye katikati ya bahari, alalaye juu ya kamba ya merikebu.
你宛如躺在海中心,睡在桅杆頂。「
35 Utasema, “Wamenipiga lakini sikuumia! Wamenichapa, lakini sisikii! Nitaamka lini ili nikanywe tena?”
人打我,我不痛,人捶我,我不覺;我何時甦醒,好再去尋醉! 」

< Mithali 23 >