< Mithali 22 >

1 Heri kuchagua jina jema kuliko utajiri mwingi, kuheshimiwa ni bora kuliko fedha au dhahabu.
De más estima es la buena fama que las muchas riquezas; y la buena gracia, que la plata y que el oro.
2 Tajiri na maskini wanafanana kwa hili: Bwana ni Muumba wao wote.
El rico y el pobre se encontraron: a todos ellos hizo Jehová.
3 Mtu mwenye busara huona hatari na kujificha, bali mjinga huendelea mbele kama kipofu nayo ikamtesa.
El avisado ve el mal, y escóndese: mas los simples pasan, y reciben el daño.
4 Unyenyekevu na kumcha Bwana huleta utajiri, heshima na uzima.
El salario de la humildad y del temor de Jehová, son riquezas, y honra, y vida.
5 Katika mapito ya waovu kuna miiba na mitego, bali yeye ailindaye nafsi yake hukaa mbali nayo.
Espinas y lazos hay en el camino del perverso: el que guarda su alma se alejará de ellos.
6 Mfundishe mtoto njia impasayo kuiendea, naye hataiacha hata akiwa mzee.
Instruye al niño en su carrera: aun cuando fuere viejo no se apartará de ella.
7 Matajiri huwatawala maskini naye akopaye ni mtumwa wa akopeshaye.
El rico se enseñoreará de los pobres; y el que toma emprestado es siervo del que empresta.
8 Yeye aupandaye uovu huvuna taabu, nayo fimbo ya ghadhabu yake itaangamizwa.
El que sembrare iniquidad, iniquidad segará; y la vara de su ira se acabará.
9 Mtu mkarimu yeye mwenyewe atabarikiwa kwa kuwa hushiriki chakula chake na maskini.
El ojo misericordioso será bendito; porque dio de su pan al menesteroso.
10 Mfukuze mwenye dhihaka, na mvutano utatoweka; ugomvi na matukano vitakoma.
Echa al burlador, y saldrá la contienda; y cesará el pleito, y la vergüenza.
11 Yeye apendaye moyo safi na yeye ambaye maneno yake ni ya neema, mfalme atakuwa rafiki yake.
El que ama la limpieza de corazón, y la gracia de sus labios, su compañero será el rey.
12 Macho ya Bwana hulinda maarifa, bali huyapinga maneno ya asiye mwaminifu.
Los ojos de Jehová miran por la ciencia; y las cosas del prevaricador pervierte.
13 Mvivu husema, “Yuko simba nje!” au, “Nitauawa katika mitaa!”
Dice el perezoso: El león está fuera: en mitad de las calles seré muerto.
14 Kinywa cha mwanamke kahaba ni shimo refu; yeye aliye chini ya ghadhabu ya Bwana atatumbukia ndani yake.
Sima profunda es la boca de las mujeres extrañas: aquel contra el cual Jehová tuviere ira, caerá en ella.
15 Upumbavu umefungwa ndani ya moyo wa mtoto, bali fimbo ya adhabu itaufukuzia mbali naye.
La insensatez está ligada en el corazón del muchacho: mas la vara de la corrección la hará alejar de él.
16 Yeye amwoneaye maskini ili kujiongezea mali, naye ampaye tajiri zawadi, wote huwa maskini.
El que oprime al pobre para aumentarse él, y el que da al rico, ciertamente será pobre.
17 Tega sikio na usikie misemo ya wenye hekima, elekeza moyo wako kwenye yale nifundishayo,
Inclina tu oído, y oye las palabras de los sabios, y pon tu corazón a mi sabiduría:
18 kwa maana inapendeza unapoyahifadhi moyoni mwako na kuwa nayo yote tayari midomoni mwako.
Porque es cosa deleitable, si las guardares en tus entrañas; y que juntamente sean ordenadas en tus labios.
19 Ili tumaini lako liwe katika Bwana, hata wewe, ninakufundisha leo.
Para que tu confianza esté en Jehová, te las he hecho saber hoy a ti también.
20 Je, sijakuandikia misemo thelathini, misemo ya mashauri na maarifa,
¿No te he escrito tres veces en consejos y ciencia;
21 kukufundisha maneno ya kweli na ya kuaminika, ili uweze kutoa majibu sahihi kwake yeye aliyekutuma?
Para hacerte saber la certidumbre de las razones verdaderas; para que respondas razones de verdad a los que enviaren a ti?
22 Usiwadhulumu maskini kwa sababu ni maskini, wala kumdhulumu mhitaji mahakamani,
No robes al pobre, porque es pobre: ni quebrantes en la puerta al afligido:
23 kwa sababu Bwana atalichukua shauri lao naye atawateka wao waliowateka.
Porque Jehová juzgará la causa de ellos; y robará su alma a los que los robaren.
24 Usifanye urafiki na mtu mwenye hasira ya haraka, usishirikiane na yule aliye mwepesi kukasirika,
No te entremetas con el iracundo: ni te acompañes con el hombre enojoso.
25 la sivyo utajifunza njia zake na kujiingiza mwenyewe kwenye mtego.
Porque no aprendas sus veredas, y tomes lazo para tu alma.
26 Usiwe mwenye kupana mikono katika rehani, au kuweka dhamana kwa ajili ya madeni.
No estés entre los que tocan la mano: entre los que fian por deudas.
27 Kama ukikosa njia ya kulipa, kitanda chako kitachukuliwa ukiwa umekilalia.
Si no tuvieres para pagar: ¿por qué quitarán tu cama de debajo de ti?
28 Usisogeze jiwe la mpaka wa zamani lililowekwa na baba zako.
No traspases el término antiguo que hicieron tus padres.
29 Je, unamwona mtu stadi katika kazi yake? Atahudumu mbele ya wafalme; hatahudumu mbele ya watu duni.
¿Has visto hombre solícito en su obra? delante de los reyes estará: no estará delante de los de baja suerte.

< Mithali 22 >