< Mithali 22 >
1 Heri kuchagua jina jema kuliko utajiri mwingi, kuheshimiwa ni bora kuliko fedha au dhahabu.
Laba slava der vairāk, nekā liela bagātība; mīlestība pie ļaudīm labāka, nekā sudrabs un zelts.
2 Tajiri na maskini wanafanana kwa hili: Bwana ni Muumba wao wote.
Bagāts sastopas ar nabagu; Tas Kungs viņus visus radījis.
3 Mtu mwenye busara huona hatari na kujificha, bali mjinga huendelea mbele kama kipofu nayo ikamtesa.
Gudrais paredz nelaimi un paglābjas; bet neprāta ļaudis skrien vien un dabū ciest.
4 Unyenyekevu na kumcha Bwana huleta utajiri, heshima na uzima.
Pazemības, proti Dieva bijības alga ir bagātība un gods un dzīvība.
5 Katika mapito ya waovu kuna miiba na mitego, bali yeye ailindaye nafsi yake hukaa mbali nayo.
Ērkšķi un valgi ir netiklam ceļā; kas savu dvēseli sargā, paliks tālu no tiem.
6 Mfundishe mtoto njia impasayo kuiendea, naye hataiacha hata akiwa mzee.
Māci bērnam viņa ceļu, tad viņš, arī vecs palicis, no tā neatkāpsies.
7 Matajiri huwatawala maskini naye akopaye ni mtumwa wa akopeshaye.
Bagātais valda pār nabagiem, un kas aizņēmās, ir aizdevēja kalps.
8 Yeye aupandaye uovu huvuna taabu, nayo fimbo ya ghadhabu yake itaangamizwa.
Kas netaisnību sēj, tas bēdas pļaus un ies bojā caur savas blēdības rīksti.
9 Mtu mkarimu yeye mwenyewe atabarikiwa kwa kuwa hushiriki chakula chake na maskini.
Žēlīga acs taps svētīta; jo viņa no savas maizes dod nabagam.
10 Mfukuze mwenye dhihaka, na mvutano utatoweka; ugomvi na matukano vitakoma.
Izdzen garzobi, tad aizies ķilda, un riešana mitēsies un kauns.
11 Yeye apendaye moyo safi na yeye ambaye maneno yake ni ya neema, mfalme atakuwa rafiki yake.
Kam šķīsta sirds un mute mīlīga, tam ķēniņš ir par draugu.
12 Macho ya Bwana hulinda maarifa, bali huyapinga maneno ya asiye mwaminifu.
Tā Kunga acis pasargā, kam atzīšana; bet nelieša vārdus viņš izdeldē.
13 Mvivu husema, “Yuko simba nje!” au, “Nitauawa katika mitaa!”
Slinkais saka: „Lauva ir ārā; ielas vidū mani saplosīs!“
14 Kinywa cha mwanamke kahaba ni shimo refu; yeye aliye chini ya ghadhabu ya Bwana atatumbukia ndani yake.
Maukas mute ir dziļa bedre; ko Tas Kungs ienīst, tas krīt tur iekšā.
15 Upumbavu umefungwa ndani ya moyo wa mtoto, bali fimbo ya adhabu itaufukuzia mbali naye.
Blēņas līp bērna sirdī; bet pārmācības rīkste tās izdzen tālu.
16 Yeye amwoneaye maskini ili kujiongezea mali, naye ampaye tajiri zawadi, wote huwa maskini.
Kas no nabaga plēš, savu mantu vairot, tas to atkal dos bagātam līdz pat trūcībai.
17 Tega sikio na usikie misemo ya wenye hekima, elekeza moyo wako kwenye yale nifundishayo,
Griez savu ausi un klausies gudro vārdu un loki savu sirdi pie manas atzīšanas.
18 kwa maana inapendeza unapoyahifadhi moyoni mwako na kuwa nayo yote tayari midomoni mwako.
Jo tas būs jaukums, ja tu tos sirdī pasargāsi un tos visnotaļ stādīsi uz savām lūpām.
19 Ili tumaini lako liwe katika Bwana, hata wewe, ninakufundisha leo.
Lai tava cerība stāv uz To Kungu. Šodien es tevi mācu, tiešām tevi!
20 Je, sijakuandikia misemo thelathini, misemo ya mashauri na maarifa,
Vai tev jau sen to neesmu rakstījis ar padomiem un mācībām,
21 kukufundisha maneno ya kweli na ya kuaminika, ili uweze kutoa majibu sahihi kwake yeye aliyekutuma?
Ka tev rādītu taisnus un patiesīgus vārdus, atbildēt patiesības vārdus tiem, kas tevi sūta.
22 Usiwadhulumu maskini kwa sababu ni maskini, wala kumdhulumu mhitaji mahakamani,
Neaplaupi nabagu, tādēļ ka tas nabags, un nenospaidi sērdieni tiesas priekšā;
23 kwa sababu Bwana atalichukua shauri lao naye atawateka wao waliowateka.
Jo Tas Kungs iztiesās viņu tiesu un laupīs dvēseli tiem, kas tos laupa.
24 Usifanye urafiki na mtu mwenye hasira ya haraka, usishirikiane na yule aliye mwepesi kukasirika,
Netinies ar bargu, un nesameties ar to, kam ātras dusmas,
25 la sivyo utajifunza njia zake na kujiingiza mwenyewe kwenye mtego.
Ka tu nemācies viņa tekas un nesavaldzini savu dvēseli.
26 Usiwe mwenye kupana mikono katika rehani, au kuweka dhamana kwa ajili ya madeni.
Neturies pie tiem, kas ar roku apsolās un par parādu galvo;
27 Kama ukikosa njia ya kulipa, kitanda chako kitachukuliwa ukiwa umekilalia.
Kad tev nebūs ko maksāt, tad noņems tavu gultu apakš tevis.
28 Usisogeze jiwe la mpaka wa zamani lililowekwa na baba zako.
Neatcel vecās robežas, ko tavi tēvi likuši.
29 Je, unamwona mtu stadi katika kazi yake? Atahudumu mbele ya wafalme; hatahudumu mbele ya watu duni.
Ja tu vīru redzi, kas tikuši(prasmīgi) savu darbu dara, tas stāvēs ķēniņu priekšā, un nestāvēs šādu tādu ļaužu priekšā.