< Mithali 21 >

1 Moyo wa mfalme uko katika mkono wa Bwana; huuongoza kama mkondo wa maji, popote apendapo.
COMO los repartimientos de las aguas, así está el corazón del rey en la mano de Jehová: á todo lo que quiere lo inclina.
2 Njia zote za mwanadamu huonekana sawa kwake, bali Bwana huupima moyo.
Todo camino del hombre es recto en su opinión: mas Jehová pesa los corazones.
3 Kufanya yaliyo sawa na haki inakubalika zaidi kwa Bwana kuliko dhabihu.
Hacer justicia y juicio es á Jehová más agradable que sacrificio.
4 Macho ya kudharau na moyo wa kiburi, ambavyo ni taa ya waovu, vyote ni dhambi!
Altivez de ojos, y orgullo de corazón, y el brillo de los impíos, son pecado.
5 Mipango ya mwenye bidii huelekeza kwenye faida, kama vile kwa hakika pupa huelekeza kwenye umaskini.
Los pensamientos del solícito ciertamente [van] á abundancia; mas todo presuroso, indefectiblemente á pobreza.
6 Mali iliyopatikana kwa ulimi wa uongo ni mvuke upitao upesi na mtego wa kufisha.
Allegar tesoros con lengua de mentira, es vanidad desatentada de aquellos que buscan la muerte.
7 Jeuri ya waovu itawaburuta mbali, kwa kuwa wanakataa kufanya yaliyo sawa.
La rapiña de los impíos los destruirá; por cuanto no quisieron hacer juicio.
8 Njia ya mwenye hatia ni ya upotovu, bali tabia ya mtu asiye na hatia ni nyofu.
El camino del hombre perverso es torcido y extraño: mas la obra del limpio es recta.
9 Ni afadhali kuishi pembeni mwa paa la nyumba, kuliko kuishi nyumba moja na mke mgomvi.
Mejor es vivir en un rincón de zaquizamí, que con la mujer rencillosa en espaciosa casa.
10 Mtu mwovu hutamani sana ubaya, jirani yake hapati huruma kutoka kwake.
El alma del impío desea mal: su prójimo no le parece bien.
11 Wakati mwenye mzaha ameadhibiwa, mjinga hupata hekima; wakati mtu mwenye hekima afundishwapo, hupata maarifa.
Cuando el escarnecedor es castigado, el simple se hace sabio; y cuando se amonestare al sabio, aprenderá ciencia.
12 Mwenye Haki huyajua yanayotendeka katika nyumba za waovu, naye atawaangamiza waovu.
Considera el justo la casa del impío: [cómo] los impíos son trastornados por el mal.
13 Mtu akiziba masikio asisikie kilio cha maskini, yeye pia atalia, wala hatajibiwa.
El que cierra su oído al clamor del pobre, también él clamará, y no será oído.
14 Zawadi itolewayo kwa siri hutuliza hasira na rushwa iliyofichwa kwenye nguo hutuliza ghadhabu kali.
El presente en secreto amansa el furor, y el don en el seno, la fuerte ira.
15 Wakati haki imetendeka, huleta furaha kwa wenye haki, bali kitisho kwa watenda mabaya.
Alegría es al justo hacer juicio; mas quebrantamiento á los que hacen iniquidad.
16 Mtu anayepotea kutoka mapito ya ufahamu, hupumzika katika kundi la waliokufa.
El hombre que se extravía del camino de la sabiduría, vendrá á parar en la compañía de los muertos.
17 Mtu apendaye anasa atakuwa maskini, yeyote apendaye mvinyo na mafuta kamwe hatakuwa tajiri.
Hombre necesitado será el que ama el deleite: y el que ama el vino y ungüentos no enriquecerá.
18 Waovu huwa fidia kwa ajili ya wenye haki, nao wasio waaminifu kwa ajili ya wanyofu.
El rescate del justo es el impío, y por los rectos el prevaricador.
19 Ni afadhali kuishi jangwani kuliko kuishi na mke mgomvi na mkorofi.
Mejor es morar en tierra del desierto, que con la mujer rencillosa é iracunda.
20 Katika nyumba ya mwenye hekima kuna akiba ya vyakula vizuri na mafuta, lakini mtu mpumbavu hutafuna vyote alivyo navyo.
Tesoro codiciable y pingüe hay en la casa del sabio; mas el hombre insensato lo disipará.
21 Yeye afuatiaye haki na upendo hupata uzima, mafanikio na heshima.
El que sigue la justicia y la misericordia, hallará la vida, la justicia, y la honra.
22 Mtu mwenye hekima huushambulia mji wa wenye nguvu, na kuangusha ngome wanazozitegemea.
La ciudad de los fuertes tomó el sabio, y derribó la fuerza en que ella confiaba.
23 Yeye alindaye kinywa chake na ulimi wake hujilinda na maafa.
El que guarda su boca y su lengua, su alma guarda de angustias.
24 Mtu mwenye kiburi na majivuno, “Mdhihaki” ndilo jina lake; hutenda mambo kwa kiburi kilichozidi.
Soberbio y presuntuoso escarnecedor es el nombre del que obra con orgullosa saña.
25 Kutamani sana kwa mvivu kutakuwa kifo chake, kwa sababu mikono yake haitaki kufanya kazi.
El deseo del perezoso le mata, porque sus manos no quieren trabajar.
26 Mchana kutwa hutamani zaidi, lakini mnyofu hutoa pasipo kuzuia.
Hay quien todo el día codicia: mas el justo da, y no desperdicia.
27 Dhabihu ya mtu mwovu ni chukizo, si zaidi sana itolewapo kwa nia mbaya!
El sacrificio de los impíos es abominación: ¡cuánto más ofreciéndolo con maldad!
28 Shahidi wa uongo ataangamia, bali maneno ya mwenye kusikia yatadumu.
El testigo mentiroso perecerá: mas el hombre que oye, permanecerá en su dicho.
29 Mtu mwovu ana uso wa ushupavu, bali mtu mnyofu huzifikiria njia zake.
El hombre impío afirma su rostro: mas el recto ordena sus caminos.
30 Hakuna hekima, wala akili, wala mpango unaoweza kufaulu dhidi ya Bwana.
No hay sabiduría, ni inteligencia, ni consejo, contra Jehová.
31 Farasi huandaliwa kwa ajili ya siku ya vita, bali ushindi huwa kwa Bwana.
El caballo se apareja para el día de la batalla: mas de Jehová es el salvar.

< Mithali 21 >