< Mithali 21 >
1 Moyo wa mfalme uko katika mkono wa Bwana; huuongoza kama mkondo wa maji, popote apendapo.
Como los repartimientos de las aguas, Así el corazón del rey está en la mano de Yavé. A todo lo que quiere lo inclina.
2 Njia zote za mwanadamu huonekana sawa kwake, bali Bwana huupima moyo.
Todo camino del hombre es recto en su propia opinión, Pero Yavé pesa los corazones.
3 Kufanya yaliyo sawa na haki inakubalika zaidi kwa Bwana kuliko dhabihu.
Yavé prefiere el derecho y la justicia en vez de los sacrificios.
4 Macho ya kudharau na moyo wa kiburi, ambavyo ni taa ya waovu, vyote ni dhambi!
Ojos altivos, corazón arrogante, Y la lámpara de los perversos son pecado.
5 Mipango ya mwenye bidii huelekeza kwenye faida, kama vile kwa hakika pupa huelekeza kwenye umaskini.
Los planes del diligente solo traen ganancia, Los del precipitado, solo indigencia.
6 Mali iliyopatikana kwa ulimi wa uongo ni mvuke upitao upesi na mtego wa kufisha.
Acumular tesoros con boca mentirosa Es vanidad ilusoria y trampa de muerte.
7 Jeuri ya waovu itawaburuta mbali, kwa kuwa wanakataa kufanya yaliyo sawa.
La violencia de los impíos los arrastrará, Por cuanto se niegan a obrar con justicia.
8 Njia ya mwenye hatia ni ya upotovu, bali tabia ya mtu asiye na hatia ni nyofu.
La senda del vicioso es torcida y extraña, Las acciones del puro son rectas.
9 Ni afadhali kuishi pembeni mwa paa la nyumba, kuliko kuishi nyumba moja na mke mgomvi.
Más vale vivir en rincón de azotea, Que en casa espaciosa con mujer rencillosa.
10 Mtu mwovu hutamani sana ubaya, jirani yake hapati huruma kutoka kwake.
Afán del perverso es desear el mal, Su prójimo nunca halla favor ante sus ojos.
11 Wakati mwenye mzaha ameadhibiwa, mjinga hupata hekima; wakati mtu mwenye hekima afundishwapo, hupata maarifa.
Cuando el burlador es castigado, el simple se hace prudente, Y cuando el sabio es instruido, adquiere conocimiento.
12 Mwenye Haki huyajua yanayotendeka katika nyumba za waovu, naye atawaangamiza waovu.
El justo considera la casa del impío, Y precipita al impío a la ruina.
13 Mtu akiziba masikio asisikie kilio cha maskini, yeye pia atalia, wala hatajibiwa.
El que cierra sus oídos al clamor del pobre No será escuchado cuando grite.
14 Zawadi itolewayo kwa siri hutuliza hasira na rushwa iliyofichwa kwenye nguo hutuliza ghadhabu kali.
Un regalo en secreto aplaca la ira, Y un soborno bajo el manto, el gran furor.
15 Wakati haki imetendeka, huleta furaha kwa wenye haki, bali kitisho kwa watenda mabaya.
Alegría para el justo es que se haga justicia, Pero terror para los que practican iniquidad.
16 Mtu anayepotea kutoka mapito ya ufahamu, hupumzika katika kundi la waliokufa.
Hombre que se extravía del camino de la sabiduría Va a parar a la asamblea de los difuntos.
17 Mtu apendaye anasa atakuwa maskini, yeyote apendaye mvinyo na mafuta kamwe hatakuwa tajiri.
El que ama el deleite será un hombre pobre, Quien ama el vino y los ungüentos no enriquecerá.
18 Waovu huwa fidia kwa ajili ya wenye haki, nao wasio waaminifu kwa ajili ya wanyofu.
El impío está en lugar del justo y El que pervierte ocupa el puesto de los rectos.
19 Ni afadhali kuishi jangwani kuliko kuishi na mke mgomvi na mkorofi.
Más vale habitar en tierra desierta, Que con mujer rencillosa e iracunda.
20 Katika nyumba ya mwenye hekima kuna akiba ya vyakula vizuri na mafuta, lakini mtu mpumbavu hutafuna vyote alivyo navyo.
Preciosos tesoros y aceite hay en la casa del sabio, Pero el hombre insensato los dilapida.
21 Yeye afuatiaye haki na upendo hupata uzima, mafanikio na heshima.
El que va tras la justicia y la misericordia Halla vida, prosperidad y honra.
22 Mtu mwenye hekima huushambulia mji wa wenye nguvu, na kuangusha ngome wanazozitegemea.
El sabio conquista la ciudad de los poderosos, Y humilla la fortaleza en la que ella confía.
23 Yeye alindaye kinywa chake na ulimi wake hujilinda na maafa.
El que guarda su boca y su lengua Guarda su alma de penurias.
24 Mtu mwenye kiburi na majivuno, “Mdhihaki” ndilo jina lake; hutenda mambo kwa kiburi kilichozidi.
El soberbio presuntuoso tiene por nombre insolente, Y obra con saña y furor.
25 Kutamani sana kwa mvivu kutakuwa kifo chake, kwa sababu mikono yake haitaki kufanya kazi.
Los deseos del perezoso lo matan, Pues sus manos no quieren trabajar.
26 Mchana kutwa hutamani zaidi, lakini mnyofu hutoa pasipo kuzuia.
Todo el día desea y desea más, Pero el justo da y no escatima.
27 Dhabihu ya mtu mwovu ni chukizo, si zaidi sana itolewapo kwa nia mbaya!
Los sacrificios del perverso son repugnancia, ¡Cuánto más cuando los ofrece con malicia!
28 Shahidi wa uongo ataangamia, bali maneno ya mwenye kusikia yatadumu.
El testigo falso perecerá, Pero el que atiende, habla perpetuamente.
29 Mtu mwovu ana uso wa ushupavu, bali mtu mnyofu huzifikiria njia zake.
El perverso se presenta desafiante, Pero el recto examina su camino.
30 Hakuna hekima, wala akili, wala mpango unaoweza kufaulu dhidi ya Bwana.
No hay habilidad, ni inteligencia, Ni consejo frente a Yavé.
31 Farasi huandaliwa kwa ajili ya siku ya vita, bali ushindi huwa kwa Bwana.
El caballo es preparado para el día de la batalla, Pero la victoria es de Yavé.