< Mithali 21 >
1 Moyo wa mfalme uko katika mkono wa Bwana; huuongoza kama mkondo wa maji, popote apendapo.
El corazón del rey está en la mano de Yahvé como las corrientes de agua. Lo convierte en lo que desea.
2 Njia zote za mwanadamu huonekana sawa kwake, bali Bwana huupima moyo.
Todo camino del hombre es correcto a sus propios ojos, pero Yahvé pesa los corazones.
3 Kufanya yaliyo sawa na haki inakubalika zaidi kwa Bwana kuliko dhabihu.
Hacer rectitud y justicia es más aceptable para Yahvé que el sacrificio.
4 Macho ya kudharau na moyo wa kiburi, ambavyo ni taa ya waovu, vyote ni dhambi!
Una mirada elevada y un corazón orgulloso, la lámpara de los malvados, es el pecado.
5 Mipango ya mwenye bidii huelekeza kwenye faida, kama vile kwa hakika pupa huelekeza kwenye umaskini.
Los planes de los diligentes seguramente conducen a la ganancia; y todo el que se precipita seguramente se precipita a la pobreza.
6 Mali iliyopatikana kwa ulimi wa uongo ni mvuke upitao upesi na mtego wa kufisha.
Conseguir tesoros por una lengua mentirosa es un vapor fugaz para los que buscan la muerte.
7 Jeuri ya waovu itawaburuta mbali, kwa kuwa wanakataa kufanya yaliyo sawa.
La violencia de los malvados los ahuyentará, porque se niegan a hacer lo que es correcto.
8 Njia ya mwenye hatia ni ya upotovu, bali tabia ya mtu asiye na hatia ni nyofu.
El camino del culpable es tortuoso, pero la conducta del inocente es recta.
9 Ni afadhali kuishi pembeni mwa paa la nyumba, kuliko kuishi nyumba moja na mke mgomvi.
Es mejor habitar en el rincón de la azotea que compartir una casa con una mujer contenciosa.
10 Mtu mwovu hutamani sana ubaya, jirani yake hapati huruma kutoka kwake.
El alma del malvado desea el mal; su prójimo no encuentra misericordia en sus ojos.
11 Wakati mwenye mzaha ameadhibiwa, mjinga hupata hekima; wakati mtu mwenye hekima afundishwapo, hupata maarifa.
Cuando el burlador es castigado, el simple adquiere sabiduría. Cuando el sabio se instruye, recibe conocimiento.
12 Mwenye Haki huyajua yanayotendeka katika nyumba za waovu, naye atawaangamiza waovu.
El Justo considera la casa de los malvados, y lleva a los malvados a la ruina.
13 Mtu akiziba masikio asisikie kilio cha maskini, yeye pia atalia, wala hatajibiwa.
El que detenga sus oídos ante el clamor de los pobres, también gritará, pero no será escuchado.
14 Zawadi itolewayo kwa siri hutuliza hasira na rushwa iliyofichwa kwenye nguo hutuliza ghadhabu kali.
Un regalo en secreto apacigua la ira, y un soborno en el manto, una fuerte ira.
15 Wakati haki imetendeka, huleta furaha kwa wenye haki, bali kitisho kwa watenda mabaya.
El justo se alegra de hacer justicia; sino que es una destrucción para los obreros de la iniquidad.
16 Mtu anayepotea kutoka mapito ya ufahamu, hupumzika katika kundi la waliokufa.
El hombre que se aleja del camino del entendimiento descansará en la asamblea de los espíritus difuntos.
17 Mtu apendaye anasa atakuwa maskini, yeyote apendaye mvinyo na mafuta kamwe hatakuwa tajiri.
El que ama el placer será un hombre pobre. El que ama el vino y el aceite no será rico.
18 Waovu huwa fidia kwa ajili ya wenye haki, nao wasio waaminifu kwa ajili ya wanyofu.
El impío es un rescate para el justo, los traidores por los rectos.
19 Ni afadhali kuishi jangwani kuliko kuishi na mke mgomvi na mkorofi.
Es mejor habitar en una tierra desierta, que con una mujer contenciosa e inquieta.
20 Katika nyumba ya mwenye hekima kuna akiba ya vyakula vizuri na mafuta, lakini mtu mpumbavu hutafuna vyote alivyo navyo.
Hay un tesoro precioso y aceite en la morada de los sabios, pero el necio se lo traga.
21 Yeye afuatiaye haki na upendo hupata uzima, mafanikio na heshima.
El que sigue la justicia y la bondad encuentra la vida, la justicia y el honor.
22 Mtu mwenye hekima huushambulia mji wa wenye nguvu, na kuangusha ngome wanazozitegemea.
Un hombre sabio escala la ciudad de los poderosos, y hace bajar la fuerza de su confianza.
23 Yeye alindaye kinywa chake na ulimi wake hujilinda na maafa.
El que cuida su boca y su lengua guarda su alma de los problemas.
24 Mtu mwenye kiburi na majivuno, “Mdhihaki” ndilo jina lake; hutenda mambo kwa kiburi kilichozidi.
El hombre orgulloso y arrogante — “burlador” es su nombre — trabaja en la arrogancia del orgullo.
25 Kutamani sana kwa mvivu kutakuwa kifo chake, kwa sababu mikono yake haitaki kufanya kazi.
El deseo del perezoso lo mata, porque sus manos se niegan a trabajar.
26 Mchana kutwa hutamani zaidi, lakini mnyofu hutoa pasipo kuzuia.
Hay quienes codician con avidez todo el día; pero los justos dan y no retienen.
27 Dhabihu ya mtu mwovu ni chukizo, si zaidi sana itolewapo kwa nia mbaya!
El sacrificio de los malvados es una abominación — ¡cuánto más, cuando lo trae con una mente perversa!
28 Shahidi wa uongo ataangamia, bali maneno ya mwenye kusikia yatadumu.
El testigo falso perecerá. Un hombre que escucha habla con la eternidad.
29 Mtu mwovu ana uso wa ushupavu, bali mtu mnyofu huzifikiria njia zake.
El malvado endurece su rostro; pero en cuanto a los rectos, él establece sus caminos.
30 Hakuna hekima, wala akili, wala mpango unaoweza kufaulu dhidi ya Bwana.
No hay sabiduría ni entendimiento ni consejo contra Yahvé.
31 Farasi huandaliwa kwa ajili ya siku ya vita, bali ushindi huwa kwa Bwana.
El caballo está preparado para el día de la batalla; pero la victoria es de Yahvé.