< Mithali 21 >

1 Moyo wa mfalme uko katika mkono wa Bwana; huuongoza kama mkondo wa maji, popote apendapo.
[Como] ribeiros de águas é o coração do rei na mão do SENHOR, ele o conduz para onde quer.
2 Njia zote za mwanadamu huonekana sawa kwake, bali Bwana huupima moyo.
Todo caminho do homem é correto aos seus [próprios] olhos; mas o SENHOR pesa os corações.
3 Kufanya yaliyo sawa na haki inakubalika zaidi kwa Bwana kuliko dhabihu.
Praticar justiça e juízo é mais aceitável ao SENHOR do que sacrifício.
4 Macho ya kudharau na moyo wa kiburi, ambavyo ni taa ya waovu, vyote ni dhambi!
Olhos orgulhosos e coração arrogante: a lavoura dos perversos é pecado.
5 Mipango ya mwenye bidii huelekeza kwenye faida, kama vile kwa hakika pupa huelekeza kwenye umaskini.
Os planos de quem trabalha com empenho somente [levam] à abundância; mas [os de] todo apressado somente à pobreza.
6 Mali iliyopatikana kwa ulimi wa uongo ni mvuke upitao upesi na mtego wa kufisha.
Trabalhar [para obter] tesouros com língua mentirosa é algo inútil [e] fácil de se perder; os que [assim fazem] buscam a morte.
7 Jeuri ya waovu itawaburuta mbali, kwa kuwa wanakataa kufanya yaliyo sawa.
A violência [praticada] pelos perversos os destruirá, porque se negam a fazer o que é justo.
8 Njia ya mwenye hatia ni ya upotovu, bali tabia ya mtu asiye na hatia ni nyofu.
O caminho do homem transgressor [é] problemático; porém a obra do puro é correta.
9 Ni afadhali kuishi pembeni mwa paa la nyumba, kuliko kuishi nyumba moja na mke mgomvi.
É melhor morar num canto do terraço do que numa casa espaçosa com uma mulher briguenta.
10 Mtu mwovu hutamani sana ubaya, jirani yake hapati huruma kutoka kwake.
A alma do perverso deseja o mal; seu próximo não lhe agrada em seus olhos.
11 Wakati mwenye mzaha ameadhibiwa, mjinga hupata hekima; wakati mtu mwenye hekima afundishwapo, hupata maarifa.
Castigando ao zombador, o ingênuo se torna sábio; e ensinando ao sábio, ele ganha conhecimento.
12 Mwenye Haki huyajua yanayotendeka katika nyumba za waovu, naye atawaangamiza waovu.
O justo considera prudentemente a casa do perverso; ele transtorna os perversos para a ruína.
13 Mtu akiziba masikio asisikie kilio cha maskini, yeye pia atalia, wala hatajibiwa.
Quem tapa seu ouvido ao clamor do pobre, ele também clamará, mas não será ouvido.
14 Zawadi itolewayo kwa siri hutuliza hasira na rushwa iliyofichwa kwenye nguo hutuliza ghadhabu kali.
O presente em segredo extingue a ira; e a dádiva no colo [acalma] o forte furor.
15 Wakati haki imetendeka, huleta furaha kwa wenye haki, bali kitisho kwa watenda mabaya.
Alegria para o justo é fazer justiça; mas [isso é] pavor para os que praticam maldade.
16 Mtu anayepotea kutoka mapito ya ufahamu, hupumzika katika kundi la waliokufa.
O homem que se afasta do caminho do entendimento repousará no ajuntamento dos mortos.
17 Mtu apendaye anasa atakuwa maskini, yeyote apendaye mvinyo na mafuta kamwe hatakuwa tajiri.
Quem ama o prazer sofrerá necessidade; aquele que ama o vinho e o azeite nunca enriquecerá.
18 Waovu huwa fidia kwa ajili ya wenye haki, nao wasio waaminifu kwa ajili ya wanyofu.
O resgate [em troca] do justo é o perverso; e no lugar do reto [fica] o transgressor.
19 Ni afadhali kuishi jangwani kuliko kuishi na mke mgomvi na mkorofi.
É melhor morar em terra deserta do que com uma mulher briguenta e que se irrita facilmente.
20 Katika nyumba ya mwenye hekima kuna akiba ya vyakula vizuri na mafuta, lakini mtu mpumbavu hutafuna vyote alivyo navyo.
[Há] tesouro desejável e azeite na casa do sábio; mas o homem tolo é devorador.
21 Yeye afuatiaye haki na upendo hupata uzima, mafanikio na heshima.
Quem segue a justiça e a bondade achará vida, justiça e honra.
22 Mtu mwenye hekima huushambulia mji wa wenye nguvu, na kuangusha ngome wanazozitegemea.
O sábio passa por cima da cidade dos fortes e derruba a fortaleza em que confiam.
23 Yeye alindaye kinywa chake na ulimi wake hujilinda na maafa.
Quem guarda sua boca e sua língua guarda sua alma de angústias.
24 Mtu mwenye kiburi na majivuno, “Mdhihaki” ndilo jina lake; hutenda mambo kwa kiburi kilichozidi.
“Zombador” é o nome do arrogante e orgulhoso; ele trata [os outros] com uma arrogância irritante.
25 Kutamani sana kwa mvivu kutakuwa kifo chake, kwa sababu mikono yake haitaki kufanya kazi.
O desejo do preguiçoso o matará, porque suas mãos se recusam a trabalhar;
26 Mchana kutwa hutamani zaidi, lakini mnyofu hutoa pasipo kuzuia.
Ele fica desejando suas cobiças o dia todo; mas o justo dá, e não deixa de dar.
27 Dhabihu ya mtu mwovu ni chukizo, si zaidi sana itolewapo kwa nia mbaya!
O sacrifício dos perversos é abominável; quanto mais quando a oferta é feita com má intenção.
28 Shahidi wa uongo ataangamia, bali maneno ya mwenye kusikia yatadumu.
A testemunha mentirosa perecerá; porém o homem que ouve [a verdade] falará com sucesso.
29 Mtu mwovu ana uso wa ushupavu, bali mtu mnyofu huzifikiria njia zake.
O homem perverso endurece seu rosto, mas o correto confirma o seu caminho.
30 Hakuna hekima, wala akili, wala mpango unaoweza kufaulu dhidi ya Bwana.
Não há sabedoria, nem entendimento, nem conselho contra o SENHOR.
31 Farasi huandaliwa kwa ajili ya siku ya vita, bali ushindi huwa kwa Bwana.
O cavalo é preparado para o dia da batalha, mas a vitória [vem] do SENHOR.

< Mithali 21 >