< Mithali 21 >

1 Moyo wa mfalme uko katika mkono wa Bwana; huuongoza kama mkondo wa maji, popote apendapo.
Le cœur du Roi est en la main de l'Eternel [comme] des ruisseaux d'eaux, il l'incline à tout ce qu'il veut.
2 Njia zote za mwanadamu huonekana sawa kwake, bali Bwana huupima moyo.
Chaque voie de l'homme lui semble droite; mais l'Eternel pèse les cœurs.
3 Kufanya yaliyo sawa na haki inakubalika zaidi kwa Bwana kuliko dhabihu.
Faire ce qui est juste et droit, est une chose que l'Eternel aime mieux que des sacrifices.
4 Macho ya kudharau na moyo wa kiburi, ambavyo ni taa ya waovu, vyote ni dhambi!
Les yeux élevés, et le cœur enflé, est le labourage des méchants, qui n'est que péché.
5 Mipango ya mwenye bidii huelekeza kwenye faida, kama vile kwa hakika pupa huelekeza kwenye umaskini.
Les pensées d'un homme diligent le conduisent à l'abondance, mais tout étourdi tombe dans l'indigence.
6 Mali iliyopatikana kwa ulimi wa uongo ni mvuke upitao upesi na mtego wa kufisha.
Travailler à avoir des trésors par une langue trompeuse, c'est une vanité poussée au loin par ceux qui cherchent la mort.
7 Jeuri ya waovu itawaburuta mbali, kwa kuwa wanakataa kufanya yaliyo sawa.
Le fourragement des méchants les abattra, parce qu'ils auront refusé de faire ce qui est droit.
8 Njia ya mwenye hatia ni ya upotovu, bali tabia ya mtu asiye na hatia ni nyofu.
Quand un homme marche de travers, il s'égare; mais l'œuvre de celui qui est pur, est droite.
9 Ni afadhali kuishi pembeni mwa paa la nyumba, kuliko kuishi nyumba moja na mke mgomvi.
Il vaut mieux habiter au coin d'un toit, que dans une maison spacieuse avec une femme querelleuse.
10 Mtu mwovu hutamani sana ubaya, jirani yake hapati huruma kutoka kwake.
L'âme du méchant souhaite le mal, et son prochain ne trouve point de grâce devant lui.
11 Wakati mwenye mzaha ameadhibiwa, mjinga hupata hekima; wakati mtu mwenye hekima afundishwapo, hupata maarifa.
Quand on punit le moqueur, le niais devient sage; et quand on instruit le sage, il reçoit la science.
12 Mwenye Haki huyajua yanayotendeka katika nyumba za waovu, naye atawaangamiza waovu.
Le juste considère prudemment la maison du méchant, quand les méchants sont renversés dans la misère.
13 Mtu akiziba masikio asisikie kilio cha maskini, yeye pia atalia, wala hatajibiwa.
Celui qui bouche son oreille pour n'ouïr point le cri du chétif, criera aussi lui-même, et on ne lui répondra point.
14 Zawadi itolewayo kwa siri hutuliza hasira na rushwa iliyofichwa kwenye nguo hutuliza ghadhabu kali.
Le don fait en secret apaise la colère, et le présent mis au sein apaise une véhémente fureur.
15 Wakati haki imetendeka, huleta furaha kwa wenye haki, bali kitisho kwa watenda mabaya.
C'est une joie au juste de faire ce qui est droit; mais c'est une frayeur aux ouvriers d'iniquité.
16 Mtu anayepotea kutoka mapito ya ufahamu, hupumzika katika kundi la waliokufa.
L'homme qui se détourne du chemin de la prudence aura sa demeure dans l'assemblée des trépassés.
17 Mtu apendaye anasa atakuwa maskini, yeyote apendaye mvinyo na mafuta kamwe hatakuwa tajiri.
L'homme qui aime à rire, sera indigent; et celui qui aime le vin et la graisse, ne s'enrichira point.
18 Waovu huwa fidia kwa ajili ya wenye haki, nao wasio waaminifu kwa ajili ya wanyofu.
Le méchant sera l'échange du juste; et le perfide, au lieu des hommes intègres.
19 Ni afadhali kuishi jangwani kuliko kuishi na mke mgomvi na mkorofi.
Il vaut mieux habiter dans une terre déserte, qu'avec une femme querelleuse et qui se dépite.
20 Katika nyumba ya mwenye hekima kuna akiba ya vyakula vizuri na mafuta, lakini mtu mpumbavu hutafuna vyote alivyo navyo.
La provision désirable, et l'huile, est dans la demeure du sage; mais l'homme fou l'engloutit.
21 Yeye afuatiaye haki na upendo hupata uzima, mafanikio na heshima.
Celui qui s'adonne soigneusement à la justice, et à la miséricorde, trouvera la vie, la justice, et la gloire.
22 Mtu mwenye hekima huushambulia mji wa wenye nguvu, na kuangusha ngome wanazozitegemea.
Le sage entre dans la ville des forts, et rabaisse la force de sa confiance.
23 Yeye alindaye kinywa chake na ulimi wake hujilinda na maafa.
Celui qui garde sa bouche et sa langue, garde son âme de détresse.
24 Mtu mwenye kiburi na majivuno, “Mdhihaki” ndilo jina lake; hutenda mambo kwa kiburi kilichozidi.
Un superbe arrogant s'appelle un moqueur, qui fait tout avec colère et fierté.
25 Kutamani sana kwa mvivu kutakuwa kifo chake, kwa sababu mikono yake haitaki kufanya kazi.
Le souhait du paresseux le tue; car ses mains ont refusé de travailler.
26 Mchana kutwa hutamani zaidi, lakini mnyofu hutoa pasipo kuzuia.
Il y a tel qui tout le jour ne fait que souhaiter; mais le juste donne, et n'épargne rien.
27 Dhabihu ya mtu mwovu ni chukizo, si zaidi sana itolewapo kwa nia mbaya!
Le sacrifice des méchants est une abomination; combien plus s'ils l'apportent avec une méchante intention?
28 Shahidi wa uongo ataangamia, bali maneno ya mwenye kusikia yatadumu.
Le témoin menteur périra; mais l'homme qui écoute, parlera avec gain de cause.
29 Mtu mwovu ana uso wa ushupavu, bali mtu mnyofu huzifikiria njia zake.
L'homme méchant a un air impudent; mais l'homme juste dresse ses voies.
30 Hakuna hekima, wala akili, wala mpango unaoweza kufaulu dhidi ya Bwana.
Il n'y a ni sagesse, ni intelligence, ni conseil contre l'Eternel.
31 Farasi huandaliwa kwa ajili ya siku ya vita, bali ushindi huwa kwa Bwana.
Le cheval est équipé pour le jour de la bataille, mais la délivrance vient de l'Eternel.

< Mithali 21 >