< Mithali 21 >

1 Moyo wa mfalme uko katika mkono wa Bwana; huuongoza kama mkondo wa maji, popote apendapo.
Le cœur d’un roi, dans la main de l’Éternel, est des ruisseaux d’eau; il l’incline à tout ce qui lui plaît.
2 Njia zote za mwanadamu huonekana sawa kwake, bali Bwana huupima moyo.
Toute voie de l’homme est droite à ses yeux; mais l’Éternel pèse les cœurs.
3 Kufanya yaliyo sawa na haki inakubalika zaidi kwa Bwana kuliko dhabihu.
Pratiquer ce qui est juste et droit, est une chose plus agréable à l’Éternel qu’un sacrifice.
4 Macho ya kudharau na moyo wa kiburi, ambavyo ni taa ya waovu, vyote ni dhambi!
L’élévation des yeux et un cœur qui s’enfle, la lampe des méchants, c’est péché.
5 Mipango ya mwenye bidii huelekeza kwenye faida, kama vile kwa hakika pupa huelekeza kwenye umaskini.
Les pensées d’un homme diligent [ne mènent] qu’à l’abondance; mais tout étourdi [ne court] qu’à la disette.
6 Mali iliyopatikana kwa ulimi wa uongo ni mvuke upitao upesi na mtego wa kufisha.
Acquérir des trésors par une langue fausse, c’est une vanité fugitive de ceux qui cherchent la mort.
7 Jeuri ya waovu itawaburuta mbali, kwa kuwa wanakataa kufanya yaliyo sawa.
La dévastation des méchants les emporte, car ils refusent de pratiquer ce qui est droit.
8 Njia ya mwenye hatia ni ya upotovu, bali tabia ya mtu asiye na hatia ni nyofu.
La voie d’un homme coupable est détournée; mais l’œuvre de celui qui est pur est droite.
9 Ni afadhali kuishi pembeni mwa paa la nyumba, kuliko kuishi nyumba moja na mke mgomvi.
Mieux vaut habiter sur le coin d’un toit, que [d’avoir] une femme querelleuse et une maison en commun.
10 Mtu mwovu hutamani sana ubaya, jirani yake hapati huruma kutoka kwake.
L’âme du méchant désire le mal; son prochain ne trouve pas grâce à ses yeux.
11 Wakati mwenye mzaha ameadhibiwa, mjinga hupata hekima; wakati mtu mwenye hekima afundishwapo, hupata maarifa.
Quand on punit le moqueur, le simple devient sage; et quand on instruit le sage, il reçoit de la connaissance.
12 Mwenye Haki huyajua yanayotendeka katika nyumba za waovu, naye atawaangamiza waovu.
Il y a un juste qui considère attentivement la maison du méchant, il renverse les méchants dans le malheur.
13 Mtu akiziba masikio asisikie kilio cha maskini, yeye pia atalia, wala hatajibiwa.
Celui qui ferme son oreille au cri du pauvre, criera lui aussi, et on ne lui répondra pas.
14 Zawadi itolewayo kwa siri hutuliza hasira na rushwa iliyofichwa kwenye nguo hutuliza ghadhabu kali.
Un don [fait] en secret apaise la colère, et un présent [mis] dans le sein [calme] une violente fureur.
15 Wakati haki imetendeka, huleta furaha kwa wenye haki, bali kitisho kwa watenda mabaya.
C’est une joie pour le juste de pratiquer ce qui est droit, mais c’est la ruine pour les ouvriers d’iniquité.
16 Mtu anayepotea kutoka mapito ya ufahamu, hupumzika katika kundi la waliokufa.
L’homme qui s’égare du chemin de la sagesse demeurera dans l’assemblée des trépassés.
17 Mtu apendaye anasa atakuwa maskini, yeyote apendaye mvinyo na mafuta kamwe hatakuwa tajiri.
Celui qui aime la joie sera dans l’indigence; celui qui aime le vin et l’huile ne s’enrichira pas.
18 Waovu huwa fidia kwa ajili ya wenye haki, nao wasio waaminifu kwa ajili ya wanyofu.
Le méchant est une rançon pour le juste, et le perfide est à la place des hommes intègres.
19 Ni afadhali kuishi jangwani kuliko kuishi na mke mgomvi na mkorofi.
Mieux vaut habiter dans une terre déserte, qu’avec une femme querelleuse et irritable.
20 Katika nyumba ya mwenye hekima kuna akiba ya vyakula vizuri na mafuta, lakini mtu mpumbavu hutafuna vyote alivyo navyo.
Il y a un trésor désirable et de l’huile dans la demeure du sage; mais l’homme insensé les engloutit.
21 Yeye afuatiaye haki na upendo hupata uzima, mafanikio na heshima.
Qui poursuit la justice et la bonté trouvera la vie, la justice, et la gloire.
22 Mtu mwenye hekima huushambulia mji wa wenye nguvu, na kuangusha ngome wanazozitegemea.
Le sage monte dans la ville des hommes forts, et abat la force de ce qui en faisait la sécurité.
23 Yeye alindaye kinywa chake na ulimi wake hujilinda na maafa.
Qui garde sa bouche et sa langue, garde son âme de détresses.
24 Mtu mwenye kiburi na majivuno, “Mdhihaki” ndilo jina lake; hutenda mambo kwa kiburi kilichozidi.
Orgueilleux, arrogant, moqueur, est le nom de celui qui agit avec colère et orgueil.
25 Kutamani sana kwa mvivu kutakuwa kifo chake, kwa sababu mikono yake haitaki kufanya kazi.
Le désir du paresseux le tue, car ses mains refusent de travailler.
26 Mchana kutwa hutamani zaidi, lakini mnyofu hutoa pasipo kuzuia.
Tout le jour il désire avidement; mais le juste donne et ne retient pas.
27 Dhabihu ya mtu mwovu ni chukizo, si zaidi sana itolewapo kwa nia mbaya!
Le sacrifice des méchants est une abomination; combien plus s’ils l’apportent avec une pensée mauvaise.
28 Shahidi wa uongo ataangamia, bali maneno ya mwenye kusikia yatadumu.
Le témoin menteur périra; mais l’homme qui écoute parlera à toujours.
29 Mtu mwovu ana uso wa ushupavu, bali mtu mnyofu huzifikiria njia zake.
L’homme méchant enhardit son visage, mais celui qui est droit règle sa voie.
30 Hakuna hekima, wala akili, wala mpango unaoweza kufaulu dhidi ya Bwana.
Il n’y a point de sagesse, et il n’y a point d’intelligence, et il n’y a point de conseil, en présence de l’Éternel.
31 Farasi huandaliwa kwa ajili ya siku ya vita, bali ushindi huwa kwa Bwana.
Le cheval est préparé pour le jour de la bataille, mais la délivrance est à l’Éternel.

< Mithali 21 >