< Mithali 21 >

1 Moyo wa mfalme uko katika mkono wa Bwana; huuongoza kama mkondo wa maji, popote apendapo.
The Kings heart is in the hand of the Lord, as the riuers of waters: he turneth it whithersoeuer it pleaseth him.
2 Njia zote za mwanadamu huonekana sawa kwake, bali Bwana huupima moyo.
Euery way of a man is right in his owne eyes: but the Lord pondereth the hearts.
3 Kufanya yaliyo sawa na haki inakubalika zaidi kwa Bwana kuliko dhabihu.
To doe iustice and iudgement is more acceptable to the Lord then sacrifice.
4 Macho ya kudharau na moyo wa kiburi, ambavyo ni taa ya waovu, vyote ni dhambi!
A hautie looke, and a proude heart, which is the light of the wicked, is sinne.
5 Mipango ya mwenye bidii huelekeza kwenye faida, kama vile kwa hakika pupa huelekeza kwenye umaskini.
The thoughtes of the diligent doe surely bring abundance: but whosoeuer is hastie, commeth surely to pouertie.
6 Mali iliyopatikana kwa ulimi wa uongo ni mvuke upitao upesi na mtego wa kufisha.
The gathering of treasures by a deceitfull tongue is vanitie tossed to and from of them that seeke death.
7 Jeuri ya waovu itawaburuta mbali, kwa kuwa wanakataa kufanya yaliyo sawa.
The robberie of the wicked shall destroy them: for they haue refused to execute iudgement.
8 Njia ya mwenye hatia ni ya upotovu, bali tabia ya mtu asiye na hatia ni nyofu.
The way of some is peruerted and strange: but of the pure man, his worke is right.
9 Ni afadhali kuishi pembeni mwa paa la nyumba, kuliko kuishi nyumba moja na mke mgomvi.
It is better to dwell in a corner of the house top, then with a contentious woman in a wide house.
10 Mtu mwovu hutamani sana ubaya, jirani yake hapati huruma kutoka kwake.
The soule of the wicked wisheth euill: and his neighbour hath no fauour in his eyes.
11 Wakati mwenye mzaha ameadhibiwa, mjinga hupata hekima; wakati mtu mwenye hekima afundishwapo, hupata maarifa.
When the scorner is punished, the foolish is wise: and when one instructeth the wise, he wil receiue knowledge.
12 Mwenye Haki huyajua yanayotendeka katika nyumba za waovu, naye atawaangamiza waovu.
The righteous teacheth the house of the wicked: but God ouerthroweth the wicked for their euill.
13 Mtu akiziba masikio asisikie kilio cha maskini, yeye pia atalia, wala hatajibiwa.
He that stoppeth his eare at the crying of the poore, he shall also cry and not be heard.
14 Zawadi itolewayo kwa siri hutuliza hasira na rushwa iliyofichwa kwenye nguo hutuliza ghadhabu kali.
A gift in secret pacifieth anger, and a gift in the bosome great wrath.
15 Wakati haki imetendeka, huleta furaha kwa wenye haki, bali kitisho kwa watenda mabaya.
It is ioye to the iust to doe iudgement: but destruction shalbe to the workers of iniquitie.
16 Mtu anayepotea kutoka mapito ya ufahamu, hupumzika katika kundi la waliokufa.
A man that wandreth out of the way of wisdome, shall remaine in the congregation of the dead.
17 Mtu apendaye anasa atakuwa maskini, yeyote apendaye mvinyo na mafuta kamwe hatakuwa tajiri.
Hee that loueth pastime, shalbe a poore man: and he that loueth wine and oyle, shall not be riche.
18 Waovu huwa fidia kwa ajili ya wenye haki, nao wasio waaminifu kwa ajili ya wanyofu.
The wicked shalbe a ransome for the iust, and the transgressour for the righteous.
19 Ni afadhali kuishi jangwani kuliko kuishi na mke mgomvi na mkorofi.
It is better to dwell in the wildernesse, then with a contentious and angry woman.
20 Katika nyumba ya mwenye hekima kuna akiba ya vyakula vizuri na mafuta, lakini mtu mpumbavu hutafuna vyote alivyo navyo.
In the house of the wise is a pleasant treasure and oyle: but a foolish man deuoureth it.
21 Yeye afuatiaye haki na upendo hupata uzima, mafanikio na heshima.
He that followeth after righteousnes and mercy, shall finde life, righteousnes, and glory.
22 Mtu mwenye hekima huushambulia mji wa wenye nguvu, na kuangusha ngome wanazozitegemea.
A wise man goeth vp into the citie of the mightie, and casteth downe the strength of the confidence thereof.
23 Yeye alindaye kinywa chake na ulimi wake hujilinda na maafa.
He that keepeth his mouth and his tongue, keepeth his soule from afflictions.
24 Mtu mwenye kiburi na majivuno, “Mdhihaki” ndilo jina lake; hutenda mambo kwa kiburi kilichozidi.
Proude, hautie and scornefull is his name that worketh in his arrogancie wrath.
25 Kutamani sana kwa mvivu kutakuwa kifo chake, kwa sababu mikono yake haitaki kufanya kazi.
The desire of the slouthfull slayeth him: for his hands refuse to worke.
26 Mchana kutwa hutamani zaidi, lakini mnyofu hutoa pasipo kuzuia.
He coueteth euermore greedily, but the righteous giueth and spareth not.
27 Dhabihu ya mtu mwovu ni chukizo, si zaidi sana itolewapo kwa nia mbaya!
The sacrifice of the wicked is an abomination: how much more when he bringeth it with a wicked minde?
28 Shahidi wa uongo ataangamia, bali maneno ya mwenye kusikia yatadumu.
A false witnes shall perish: but hee that heareth, speaketh continually.
29 Mtu mwovu ana uso wa ushupavu, bali mtu mnyofu huzifikiria njia zake.
A wicked man hardeneth his face: but the iust, he will direct his way.
30 Hakuna hekima, wala akili, wala mpango unaoweza kufaulu dhidi ya Bwana.
There is no wisedome, neither vnderstanding, nor counsell against the Lord.
31 Farasi huandaliwa kwa ajili ya siku ya vita, bali ushindi huwa kwa Bwana.
The horse is prepared against the day of battell: but saluation is of the Lord.

< Mithali 21 >