< Mithali 21 >
1 Moyo wa mfalme uko katika mkono wa Bwana; huuongoza kama mkondo wa maji, popote apendapo.
Jako potůčkové vod jest srdce královo v ruce Hospodinově; kamžkoli chce, nakloňuje ho.
2 Njia zote za mwanadamu huonekana sawa kwake, bali Bwana huupima moyo.
Všeliká cesta člověka přímá se zdá jemu, ale kterýž zpytuje srdce, Hospodin jest.
3 Kufanya yaliyo sawa na haki inakubalika zaidi kwa Bwana kuliko dhabihu.
Vykonávati spravedlnost a soud více se líbí Hospodinu nežli obět.
4 Macho ya kudharau na moyo wa kiburi, ambavyo ni taa ya waovu, vyote ni dhambi!
Vysokost očí, širokost srdce, a orání bezbožných jest hříchem.
5 Mipango ya mwenye bidii huelekeza kwenye faida, kama vile kwa hakika pupa huelekeza kwenye umaskini.
Myšlení bedlivého všelijak ku prospěchu přicházejí, ale každého toho, kdož kvapný jest, toliko k nouzi.
6 Mali iliyopatikana kwa ulimi wa uongo ni mvuke upitao upesi na mtego wa kufisha.
Pokladové jazykem lživým shromáždění jsou marnost pomíjející hledajících smrti.
7 Jeuri ya waovu itawaburuta mbali, kwa kuwa wanakataa kufanya yaliyo sawa.
Zhouba, kterouž činí bezbožníci, bydliti bude u nich; nebo se zpěčují činiti soudu.
8 Njia ya mwenye hatia ni ya upotovu, bali tabia ya mtu asiye na hatia ni nyofu.
Muž, jehož cesta převrácená jest, cizí jest, čistého pak dílo přímé jest.
9 Ni afadhali kuishi pembeni mwa paa la nyumba, kuliko kuishi nyumba moja na mke mgomvi.
Lépe jest bydliti v koutě na střeše, nežli s ženou svárlivou v domě společném.
10 Mtu mwovu hutamani sana ubaya, jirani yake hapati huruma kutoka kwake.
Duše bezbožného žádá zlého, ani přítel jeho jemu příjemný nebývá.
11 Wakati mwenye mzaha ameadhibiwa, mjinga hupata hekima; wakati mtu mwenye hekima afundishwapo, hupata maarifa.
Posměvač když bývá trestán, hloupý bývá moudřejší; a když se uměle nakládá s moudrým, přijímá umění.
12 Mwenye Haki huyajua yanayotendeka katika nyumba za waovu, naye atawaangamiza waovu.
Vyučuje Bůh spravedlivého na domě bezbožného, kterýž vyvrací bezbožné pro zlost.
13 Mtu akiziba masikio asisikie kilio cha maskini, yeye pia atalia, wala hatajibiwa.
Kdo zacpává ucho své k volání chudého, i on sám volati bude, a nebude vyslyšán.
14 Zawadi itolewayo kwa siri hutuliza hasira na rushwa iliyofichwa kwenye nguo hutuliza ghadhabu kali.
Dar skrytý ukrocuje prchlivost, a pocta v klíně hněv prudký.
15 Wakati haki imetendeka, huleta furaha kwa wenye haki, bali kitisho kwa watenda mabaya.
Radostí jest spravedlivému činiti soud, ale hrůzou činitelům nepravosti.
16 Mtu anayepotea kutoka mapito ya ufahamu, hupumzika katika kundi la waliokufa.
Èlověk bloudící z cesty rozumnosti v shromáždění mrtvých odpočívati bude.
17 Mtu apendaye anasa atakuwa maskini, yeyote apendaye mvinyo na mafuta kamwe hatakuwa tajiri.
Muž milující veselost nuzníkem bývá, a kdož miluje víno a masti, nezbohatne.
18 Waovu huwa fidia kwa ajili ya wenye haki, nao wasio waaminifu kwa ajili ya wanyofu.
Výplatou za spravedlivého bude bezbožný, a za upřímé ošemetný.
19 Ni afadhali kuishi jangwani kuliko kuishi na mke mgomvi na mkorofi.
Lépe jest bydliti v zemi pusté než s ženou svárlivou a zlostnou.
20 Katika nyumba ya mwenye hekima kuna akiba ya vyakula vizuri na mafuta, lakini mtu mpumbavu hutafuna vyote alivyo navyo.
Poklad žádostivý a olej jest v příbytku moudrého, bláznivý pak člověk zžírá jej.
21 Yeye afuatiaye haki na upendo hupata uzima, mafanikio na heshima.
Kdo snažně následuje spravedlnosti a milosrdenství, nalézá život, spravedlnost i slávu.
22 Mtu mwenye hekima huushambulia mji wa wenye nguvu, na kuangusha ngome wanazozitegemea.
Do města silných vchází moudrý, a boří pevnost doufání jeho.
23 Yeye alindaye kinywa chake na ulimi wake hujilinda na maafa.
Kdo ostříhá úst svých a jazyka svého, ostříhá od úzkosti duše své.
24 Mtu mwenye kiburi na majivuno, “Mdhihaki” ndilo jina lake; hutenda mambo kwa kiburi kilichozidi.
Hrdého a pyšného jméno jest posměvač, kterýž vše s neochotností a pýchou dělá.
25 Kutamani sana kwa mvivu kutakuwa kifo chake, kwa sababu mikono yake haitaki kufanya kazi.
Žádost lenivého zabijí jej, nebo nechtí ruce jeho dělati.
26 Mchana kutwa hutamani zaidi, lakini mnyofu hutoa pasipo kuzuia.
Každého dne žádostí hoří, spravedlivý pak dává a neskoupí se.
27 Dhabihu ya mtu mwovu ni chukizo, si zaidi sana itolewapo kwa nia mbaya!
Obět bezbožných ohavností jest, ovšem pak jestliže by ji s nešlechetností obětovali.
28 Shahidi wa uongo ataangamia, bali maneno ya mwenye kusikia yatadumu.
Svědek lživý zahyne, ale muž, kterýž co slyší, stále mluviti bude.
29 Mtu mwovu ana uso wa ushupavu, bali mtu mnyofu huzifikiria njia zake.
Muž bezbožný zatvrzuje tvář svou, upřímý pak měří cestu svou.
30 Hakuna hekima, wala akili, wala mpango unaoweza kufaulu dhidi ya Bwana.
Není žádné moudrosti, ani opatrnosti, ani rady proti Hospodinu.
31 Farasi huandaliwa kwa ajili ya siku ya vita, bali ushindi huwa kwa Bwana.
Kůň strojen bývá ke dni boje, ale Hospodinovo jest vysvobození.