< Mithali 20 >
1 Mvinyo ni mdhihaki na kileo ni mgomvi; yeyote apotoshwaye navyo hana hekima.
El vino te transforma en un burlador, y el alcohol te vuelve agresivo. Si te dejas engañar por la bebida, eres un tonto.
2 Ghadhabu ya mfalme ni kama ngurumo ya simba; yeye amkasirishaye hupoteza uhai wake.
Cuando un rey se enoja en gran manera, se escuchará como un león rugiente. Quien haya causado su enojo corre el riesgo de ir a la muerte.
3 Ni kwa heshima ya mtu kujitenga ugomvi, bali kila mpumbavu ni mwepesi kugombana.
Evitar el conflicto es hacer lo correcto. Pero los necios se apresuran a iniciar la discusión.
4 Mvivu halimi kwa majira; kwa hiyo wakati wa mavuno hutazama lakini hapati chochote.
Los holgazanes no salen a sembrar cuando deberían. Por eso, cuando llega la cosecha, no tienen nada que recoger.
5 Makusudi ya moyo wa mwanadamu ni maji yenye kina, lakini mtu mwenye ufahamu huyachota.
Descubrir lo que piensan los demás es como mirar en aguas profundas. Pero el que tiene entendimiento los conocerá.
6 Watu wengi hujidai kuwa na upendo usiokoma, bali mtu mwaminifu ni nani awezaye kumpata?
Muchos te dirán que son leales, pero ¿podrás hallar a una persona digna de confianza?
7 Mtu mwenye haki huishi maisha yasiyo na lawama, wamebarikiwa watoto wake baada yake.
El pueblo de Dios vive con honestidad. ¡Cuán felices son sus hijos si siguen tal ejemplo!
8 Wakati mfalme aketipo katika kiti chake cha enzi kuhukumu, hupepeta ubaya wote kwa macho yake.
Cuando el rey se sienta a emitir un juicio, puede ver lo que no está bien.
9 Ni nani awezaye kusema, “Nimeuweka moyo wangu safi; mimi ni safi na sina dhambi?”
¿Quién puede decir: “Estoy seguro de que mi conciencia está limpia y estoy limpio de pecado”?
10 Mawe ya kupimia yaliyo tofauti na vipimo tofauti, Bwana huchukia vyote viwili.
El Señor aborrece el peso falso así como la medida falsa.
11 Hata mtoto hujulikana kwa matendo yake, kama tabia yake ni safi na adili.
Hasta los niños revelan su carácter por lo que hacen, ya sean acciones buenas o malas.
12 Masikio yasikiayo na macho yaonayo, Bwana ndiye alivifanya vyote viwili.
El Señor nos dio orejas para oír y ojos para ver.
13 Usiupende usingizi la sivyo utakuwa maskini, uwe macho nawe utakuwa na chakula cha akiba.
Si te gusta dormir, terminarás pobre. Levántate y trabaja, para que tengas qué comer.
14 “Haifai, haifai!” asema mnunuzi, kisha huondoka akijisifia ununuzi wake.
“Es basura”, dice el que compra, pero luego se jacta delante de otros de haber hecho un buen negocio.
15 Dhahabu kunayo, na marijani kwa wingi, lakini midomo inenayo maarifa ni kito cha thamani kilicho adimu.
Hay oro y muchas piedras preciosas. Pero hablar con sensatez es la joya más valiosa.
16 Chukua vazi la yule awekaye dhamana kwa ajili ya mgeni; lishikilie iwe dhamana kama anafanya hivyo kwa ajili ya mwanamke mpotovu.
Si alguno sirve como codeudor de un extranjero dando su abrigo como garantía de pago, asegúrate de tomarlo. ¡Toma todo lo que haya sido entregado como pago a favor de un extranjero!
17 Chakula kilichopatikana kwa hila ni kitamu kwa mwanadamu, bali huishia na kinywa kilichojaa changarawe.
La comida que es producto del fraude puede tener un dulce sabor, pero después verán sus bocas llenas de gravilla.
18 Fanya mipango kwa kutafuta mashauri, ukipigana vita, tafuta maelekezo.
Con el consejo sabio, los planes son exitosos. Si vas a la guerra, asegúrate de tener la instrucción correcta.
19 Maneno ya kusengenya husababisha kutokuaminika, kwa hiyo mwepuke mtu anayezungumza kupita kiasi.
El chismoso anda de aquí para allá revelando secretos. Aléjate de aquellos que hablan mucho.
20 Ikiwa mtu atamlaani baba yake au mama yake, taa yake itazimwa katika giza nene.
Todo aquél que maldice a su padre o a su madre apaga su luz y terminará en oscuridad absoluta.
21 Urithi upatikanao haraka mwanzoni, hautabarikiwa mwishoni.
La riqueza rápida no te hará bien al final de cuentas.
22 Usiseme, “Nitakulipiza kwa ajili ya kosa hili!” Mngojee Bwana, naye atakuokoa.
No digas: “Me pagarás por este mal que me has hecho”. Déjaselo al Señor, y él te ayudará.
23 Bwana anachukia sana mawe ya kupimia ya udanganyifu, nazo mizani zisizo halali hazimpendezi.
El Señor aborrece el peso incorrecto. No está bien usar peso falso.
24 Hatua za mtu huongozwa na Bwana. Anawezaje basi mtu yeyote kuelewa njia yake mwenyewe?
El Señor nos muestra el camino a seguir, ¿por qué habríamos de decidir nosotros mismos?
25 Ni mtego kwa mtu kuweka wakfu kitu kwa haraka na baada ya kitambo kidogo kufikiria tena nadhiri zake.
Es un error hacerle una promesa al Señor y luego arrepentirnos de lo que hemos prometido.
26 Mfalme mwenye hekima hupepeta waovu, hulipitisha gurudumu la kupuria juu yao.
Un rey sabio separa a los malvados con un aventador y luego los castiga cuando hace el trillado.
27 Taa ya Bwana huchunguza roho ya mwanadamu, huchunguza utu wake wa ndani.
La luz del Señor brilla en la conciencia, revelando nuestros más profundos pensamientos.
28 Upendo na uaminifu humweka mfalme salama, kwa njia ya upendo, kiti chake cha enzi huwa salama.
El amor fiel y la lealtad mantienen al rey a salvo. El amor fiel es el fundamento de su gobierno.
29 Utukufu wa vijana ni nguvu zao, mvi ni fahari ya uzee.
Los jóvenes valoran su fuerza, pero los ancianos estiman más la sabiduría que viene con los años.
30 Mapigo na majeraha huusafisha ubaya, nayo michapo hutakasa utu wa ndani.
Los azotes espantan la maldad; los golpes limpian hasta adentro.