< Mithali 20 >
1 Mvinyo ni mdhihaki na kileo ni mgomvi; yeyote apotoshwaye navyo hana hekima.
El vino es mofador, el licor alborotador; nunca será sabio el que a ellos se entrega.
2 Ghadhabu ya mfalme ni kama ngurumo ya simba; yeye amkasirishaye hupoteza uhai wake.
Semejante al rugido de león es el furor del rey; quien provoca su ira peca contra sí mismo.
3 Ni kwa heshima ya mtu kujitenga ugomvi, bali kila mpumbavu ni mwepesi kugombana.
Es honor del hombre abstenerse de altercados; todos los necios se meten en pendencias.
4 Mvivu halimi kwa majira; kwa hiyo wakati wa mavuno hutazama lakini hapati chochote.
A causa del frío no ara el perezoso, por eso mendigará en vano en la siega.
5 Makusudi ya moyo wa mwanadamu ni maji yenye kina, lakini mtu mwenye ufahamu huyachota.
Aguas profundas son los pensamientos del corazón humano, mas el sabio sabe sacarlos.
6 Watu wengi hujidai kuwa na upendo usiokoma, bali mtu mwaminifu ni nani awezaye kumpata?
Muchos se jactan de su bondad, pero un hombre fiel, ¿quién lo hallará?
7 Mtu mwenye haki huishi maisha yasiyo na lawama, wamebarikiwa watoto wake baada yake.
El justo procede sin tacha, bienaventurados sus hijos después de él.
8 Wakati mfalme aketipo katika kiti chake cha enzi kuhukumu, hupepeta ubaya wote kwa macho yake.
El rey, sentado como juez en el trono, con su sola mirada ahuyenta todo lo malo.
9 Ni nani awezaye kusema, “Nimeuweka moyo wangu safi; mimi ni safi na sina dhambi?”
¿Quién podrá decir: “He purificado mi corazón, limpio estoy de mi pecado”?
10 Mawe ya kupimia yaliyo tofauti na vipimo tofauti, Bwana huchukia vyote viwili.
Peso falso y falsa medida son dos cosas abominables ante Yahvé.
11 Hata mtoto hujulikana kwa matendo yake, kama tabia yake ni safi na adili.
Ya el niño muestra por sus acciones si su conducta ha de ser pura y recta.
12 Masikio yasikiayo na macho yaonayo, Bwana ndiye alivifanya vyote viwili.
El oído que oye, y el ojo que ve, ambas son obras de Yahvé.
13 Usiupende usingizi la sivyo utakuwa maskini, uwe macho nawe utakuwa na chakula cha akiba.
Huye el sueño, para que no empobrezcas; abre tus ojos, y te saciarás de pan.
14 “Haifai, haifai!” asema mnunuzi, kisha huondoka akijisifia ununuzi wake.
“Malo, malo”, dice el comprador, pero después de haber comprado se gloría.
15 Dhahabu kunayo, na marijani kwa wingi, lakini midomo inenayo maarifa ni kito cha thamani kilicho adimu.
Hay oro y perlas en abundancia, mas la alhaja más preciosa son los labios instruidos.
16 Chukua vazi la yule awekaye dhamana kwa ajili ya mgeni; lishikilie iwe dhamana kama anafanya hivyo kwa ajili ya mwanamke mpotovu.
Tómate el vestido del que salió fiador por un extraño, y exígele una prenda por lo que debe al extranjero.
17 Chakula kilichopatikana kwa hila ni kitamu kwa mwanadamu, bali huishia na kinywa kilichojaa changarawe.
El pan injustamente adquirido le gusta al hombre, pero después se llena su boca de guijos.
18 Fanya mipango kwa kutafuta mashauri, ukipigana vita, tafuta maelekezo.
Los consejos aseguran el éxito de los proyectos; no hagas la guerra sin previa deliberación.
19 Maneno ya kusengenya husababisha kutokuaminika, kwa hiyo mwepuke mtu anayezungumza kupita kiasi.
No tengas trato con el que revela secretos y es chismoso, ni con aquel cuyos labios siempre se abren.
20 Ikiwa mtu atamlaani baba yake au mama yake, taa yake itazimwa katika giza nene.
Si uno maldice a su padre y a su madre, su antorcha se apagará en densas tinieblas.
21 Urithi upatikanao haraka mwanzoni, hautabarikiwa mwishoni.
Lo que uno comenzó a adquirir apresuradamente, no tiene fin venturoso.
22 Usiseme, “Nitakulipiza kwa ajili ya kosa hili!” Mngojee Bwana, naye atakuokoa.
No digas: “Yo devolveré el mal”; espera en Yahvé, y Él te salvará.
23 Bwana anachukia sana mawe ya kupimia ya udanganyifu, nazo mizani zisizo halali hazimpendezi.
Yahvé abomina las pesas falsas, y falsa balanza es cosa mala.
24 Hatua za mtu huongozwa na Bwana. Anawezaje basi mtu yeyote kuelewa njia yake mwenyewe?
Es Yahvé quien dirige los pasos del hombre; ¿qué sabe el hombre de su destino?
25 Ni mtego kwa mtu kuweka wakfu kitu kwa haraka na baada ya kitambo kidogo kufikiria tena nadhiri zake.
Es un lazo para el hombre decir a la ligera: “Consagrado”, sin meditar antes de hacer el voto.
26 Mfalme mwenye hekima hupepeta waovu, hulipitisha gurudumu la kupuria juu yao.
El rey sabio avienta a los malhechores, y hace pasar sobre ellos la rueda.
27 Taa ya Bwana huchunguza roho ya mwanadamu, huchunguza utu wake wa ndani.
Antorcha de Yahvé es el espíritu del hombre, escudriña todos los secretos del corazón.
28 Upendo na uaminifu humweka mfalme salama, kwa njia ya upendo, kiti chake cha enzi huwa salama.
Bondad y fidelidad guardan al rey, y la clemencia le afirma el trono.
29 Utukufu wa vijana ni nguvu zao, mvi ni fahari ya uzee.
Los jóvenes se glorían de su fuerza, el adorno de los ancianos son las canas.
30 Mapigo na majeraha huusafisha ubaya, nayo michapo hutakasa utu wa ndani.
Los azotes que hieren son medicina contra el mal, como las llagas que penetran hasta el interior del cuerpo.