< Mithali 20 >

1 Mvinyo ni mdhihaki na kileo ni mgomvi; yeyote apotoshwaye navyo hana hekima.
Le vin est un moqueur et la bière un bagarreur. Celui qui se laisse égarer par eux n'est pas sage.
2 Ghadhabu ya mfalme ni kama ngurumo ya simba; yeye amkasirishaye hupoteza uhai wake.
La terreur d'un roi est comme le rugissement d'un lion. Celui qui le provoque à la colère perd sa propre vie.
3 Ni kwa heshima ya mtu kujitenga ugomvi, bali kila mpumbavu ni mwepesi kugombana.
C'est un honneur pour un homme de se tenir à l'écart des querelles, mais tous les fous se disputeront.
4 Mvivu halimi kwa majira; kwa hiyo wakati wa mavuno hutazama lakini hapati chochote.
Le paresseux ne laboure pas à cause de l'hiver; c'est pourquoi il mendiera dans la moisson, et n'aura rien.
5 Makusudi ya moyo wa mwanadamu ni maji yenye kina, lakini mtu mwenye ufahamu huyachota.
Le conseil dans le cœur de l'homme est comme une eau profonde, mais un homme compréhensif l'extraira.
6 Watu wengi hujidai kuwa na upendo usiokoma, bali mtu mwaminifu ni nani awezaye kumpata?
Beaucoup d'hommes prétendent être des hommes d'amour indéfectible, mais qui peut trouver un homme fidèle?
7 Mtu mwenye haki huishi maisha yasiyo na lawama, wamebarikiwa watoto wake baada yake.
L'homme juste marche dans l'intégrité. Bénis soient ses enfants après lui.
8 Wakati mfalme aketipo katika kiti chake cha enzi kuhukumu, hupepeta ubaya wote kwa macho yake.
Un roi qui s'assied sur le trône du jugement disperse tout le mal avec ses yeux.
9 Ni nani awezaye kusema, “Nimeuweka moyo wangu safi; mimi ni safi na sina dhambi?”
Qui peut dire: « J'ai rendu mon cœur pur. Je suis propre et sans péché? »
10 Mawe ya kupimia yaliyo tofauti na vipimo tofauti, Bwana huchukia vyote viwili.
Des poids et des mesures différents, tous deux sont une abomination pour Yahvé.
11 Hata mtoto hujulikana kwa matendo yake, kama tabia yake ni safi na adili.
Même un enfant se fait connaître par ses actions, si son travail est pur, et s'il est juste.
12 Masikio yasikiayo na macho yaonayo, Bwana ndiye alivifanya vyote viwili.
L'oreille qui entend, et l'œil qui voit, Yahvé les a égalisés tous les deux.
13 Usiupende usingizi la sivyo utakuwa maskini, uwe macho nawe utakuwa na chakula cha akiba.
N'aime pas le sommeil, de peur que tu ne deviennes pauvre. Ouvrez vos yeux, et vous serez rassasiés de pain.
14 “Haifai, haifai!” asema mnunuzi, kisha huondoka akijisifia ununuzi wake.
« Ce n'est pas bon, ce n'est pas bon », dit l'acheteur; mais quand il est parti de son côté, alors il se vante.
15 Dhahabu kunayo, na marijani kwa wingi, lakini midomo inenayo maarifa ni kito cha thamani kilicho adimu.
Il y a de l'or et des rubis en abondance, mais les lèvres de la connaissance sont un joyau rare.
16 Chukua vazi la yule awekaye dhamana kwa ajili ya mgeni; lishikilie iwe dhamana kama anafanya hivyo kwa ajili ya mwanamke mpotovu.
Prends le vêtement de celui qui se porte garant pour un étranger; et le garder en gage pour une femme volage.
17 Chakula kilichopatikana kwa hila ni kitamu kwa mwanadamu, bali huishia na kinywa kilichojaa changarawe.
La nourriture frauduleuse est douce pour un homme, mais après, sa bouche est remplie de gravier.
18 Fanya mipango kwa kutafuta mashauri, ukipigana vita, tafuta maelekezo.
Les plans sont établis par des conseils; par des conseils avisés, vous faites la guerre!
19 Maneno ya kusengenya husababisha kutokuaminika, kwa hiyo mwepuke mtu anayezungumza kupita kiasi.
Celui qui se promène comme un conteur révèle des secrets; ne fréquente donc pas celui qui ouvre grand ses lèvres.
20 Ikiwa mtu atamlaani baba yake au mama yake, taa yake itazimwa katika giza nene.
Quiconque maudit son père ou sa mère, sa lampe s'éteindra dans l'obscurité des ténèbres.
21 Urithi upatikanao haraka mwanzoni, hautabarikiwa mwishoni.
Un héritage rapidement acquis au début ne seront pas bénis à la fin.
22 Usiseme, “Nitakulipiza kwa ajili ya kosa hili!” Mngojee Bwana, naye atakuokoa.
Ne dites pas: « Je rembourserai le mal. » Attendez Yahvé, et il vous sauvera.
23 Bwana anachukia sana mawe ya kupimia ya udanganyifu, nazo mizani zisizo halali hazimpendezi.
Yahvé déteste les poids différents, et les balances malhonnêtes ne sont pas agréables.
24 Hatua za mtu huongozwa na Bwana. Anawezaje basi mtu yeyote kuelewa njia yake mwenyewe?
Les pas de l'homme viennent de Yahvé; comment alors l'homme peut-il comprendre son chemin?
25 Ni mtego kwa mtu kuweka wakfu kitu kwa haraka na baada ya kitambo kidogo kufikiria tena nadhiri zake.
C'est un piège pour l'homme que de faire un dévouement irréfléchi, puis plus tard pour considérer ses vœux.
26 Mfalme mwenye hekima hupepeta waovu, hulipitisha gurudumu la kupuria juu yao.
Un roi sage vanne les méchants, et fait passer la roue de battage dessus.
27 Taa ya Bwana huchunguza roho ya mwanadamu, huchunguza utu wake wa ndani.
L'esprit de l'homme est la lampe de Yahvé, en fouillant toutes ses parties les plus intimes.
28 Upendo na uaminifu humweka mfalme salama, kwa njia ya upendo, kiti chake cha enzi huwa salama.
L'amour et la fidélité protègent le roi. Son trône est soutenu par l'amour.
29 Utukufu wa vijana ni nguvu zao, mvi ni fahari ya uzee.
La gloire des jeunes hommes, c'est leur force. La splendeur des vieillards, ce sont leurs cheveux gris.
30 Mapigo na majeraha huusafisha ubaya, nayo michapo hutakasa utu wa ndani.
Les coups qui blessent nettoient le mal, et les coups purgent les parties les plus intimes.

< Mithali 20 >